Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Job 12.18
Bible en Swahili de l’est


Intervention n° 4 de Job

1 Ndipo Ayubu akajibu, na kusema,
2 Hapana shaka ninyi ndinyi watu halisi, Nanyi mtakapokufa, ndipo na hekima itakoma.
Job 8.8-8.10 1 Corinthiens 6.5 Proverbes 28.11 Job 20.3 1 Corinthiens 4.10
3 Lakini mimi pia, nina fahamu kama ninyi; Mimi si duni yenu ninyi; Naam, ni nani asiyejua mambo kama hayo?
Job 13.2-13.5 2 Corinthiens 11.21-11.23 Job 26.2-26.3 2 Corinthiens 11.5 Proverbes 26.4
4 Mimi ni mtu wa kuchekwa na jirani yake, Ni mtu niliyemwita Mungu, naye akanijibu; Huyo mwenye haki, aliye mtimilifu, amekuwa ni kicheko.
Job 30.1 Psaumes 91.15 Job 21.3 Job 17.6 Job 16.10
5 Katika mawazo yake huyo aliye na raha mna kudharau mashaka; Tayari kwa ajili ya wenye kuteleza miguu.
Proverbes 13.9 Psaumes 123.3-123.4 Job 6.5 Job 16.4 Psaumes 94.18
6 Hema za wapokonyi hufanikiwa, Na hao wamkasirishao Mungu hukaa salama; Mikononi mwao Mungu huleta vitu vingi.
Job 9.24 Job 21.7-21.15 Psaumes 73.11-73.12 Jérémie 5.27 Psaumes 37.35
7 Lakini sasa waulize hao wanyama, nao watakufundisha; Na nyuni wa angani, nao watakuambia;
Proverbes 6.6 Job 21.29-21.30 Esaïe 1.3 Jérémie 8.7
8 Au nena na nchi, nayo itakufundisha; Nao samaki wa baharini watakutangazia.
9 Katika hawa wote ni yupi asiyejua, Kwamba ni mkono wa Bwana uliofanya haya?
Esaïe 41.20 Job 12.3 1 Samuel 2.7 Job 22.18 Jérémie 27.5-27.6
10 Ambaye nafsi ya kila kilicho hai i mkononi mwake, Na pumzi zao wanadamu wote.
Actes 17.28 Nombres 16.22 Job 27.3 Job 33.4 Psaumes 146.3-146.4
11 Je! Sikio silo lijaribulo maneno, Kama vile kaakaa lionjavyo chakula?
Job 34.3 1 Corinthiens 10.15 1 Pierre 2.3 Job 6.30 Philippiens 1.10
12 Wazee ndio walio na hekima, Na katika kuishi siku nyingi iko fahamu.
Job 32.7 Job 15.10 Job 8.8
13 Hekima na amri zina yeye [Mungu]; Yeye anayo mashauri na fahamu.
Job 9.4 Job 36.5 Proverbes 8.14 Job 11.6 Ephésiens 1.8
14 Tazama, yuavunja, wala haiwezekani kujenga tena; Humfunga mtu, wala haiwezekani kumfungua.
Apocalypse 3.7 Esaïe 22.22 Job 37.7 Job 16.11 Job 19.10
15 Tazama, yuayazuia maji, nayo yakatika; Tena, huyapeleka, nayo yaipindua dunia.
1 Rois 17.1 Job 12.10 Psaumes 104.7-104.9 Apocalypse 11.6 Nahum 1.4
16 Kwake yeye ziko nguvu, na makusudi kufanikiwa; Huyo adanganywaye, na mdanganyi pia ni wake.
Ezéchiel 14.9 Job 13.7 Job 12.13 1 Rois 22.22-22.23 Job 13.9
17 Yeye huwaondoa washauri hali wametekwa nyara, Naye huwafanya waamuzi kuwa ni wapumbavu.
Esaïe 29.14 2 Samuel 17.23 Job 9.24 2 Samuel 17.14 Job 3.14
18 Yeye hulegeza kifungo cha wafalme, Na kuwafunga viuno vyao kwa mshipi.
Daniel 2.21 Psaumes 116.16 2 Chroniques 33.11-33.14 Jérémie 52.31-52.34 Apocalypse 19.16
19 Yeye huwaondoa makuhani hali wametekwa nyara. Na kuwapindua mashujaa.
Josué 10.24 Job 34.28 Esaïe 45.1 Esaïe 37.36-37.38 Apocalypse 19.19-19.21
20 Huondoa matamko ya hao walioaminiwa, Na kuondoa fahamu za wazee.
Job 32.9 Job 17.4 Proverbes 12.22 Esaïe 3.1-3.3 Proverbes 12.19
21 Humwaga aibu juu ya hao wakuu, Na kulegeza mshipi wa wenye nguvu.
Psaumes 107.40 Esaïe 22.21 2 Rois 9.34-9.37 Daniel 4.32-4.33 Exode 16.24
22 Huvumbua mambo ya siri tokea gizani, Na hicho kilicho giza tupu huleta mwangani.
Daniel 2.22 1 Corinthiens 4.5 Job 3.5 1 Corinthiens 2.10 Job 34.22
23 Huyaongeza mataifa, na kuyaangamiza; Huyaeneza mataifa mbali, na kuyaacha.
Esaïe 26.15 Esaïe 9.3 Psaumes 107.38 Esaïe 60.22 Esaïe 51.2
24 Huwaondolea moyo wakuu wa watu wa nchi, Na kuwapoteza nyikani pasipokuwa na njia.
Psaumes 107.40 Job 12.20 Esaïe 19.1 Psaumes 107.4 Daniel 4.16
25 Wao hupapasa gizani pasipokuwa na mwanga, Naye huwafanya kupepesuka kama vile mlevi.
Job 5.14 Psaumes 107.27 Esaïe 19.14 Esaïe 24.20 Actes 13.11

Cette Bible est dans le domaine public.