Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Esdras 8.8
Bible en Swahili de l’est


Les compagnons d’Esdras

1 Basi hawa ndio wakuu wa mbari za baba zao, na hii ndiyo nasaba ya wale waliokwea pamoja nami kutoka Babeli, wakati wa kutawala kwake mfalme Artashasta.
Esdras 7.7 1 Chroniques 4.33 2 Chroniques 26.12 Esdras 2.62 1 Chroniques 9.34
2 Wa wana wa Finehasi, Gershoni; wa wana wa Ithamari, Danieli; wa wana wa Daudi, Hatushi, mwana wa Shekania;
1 Chroniques 3.22 1 Chroniques 6.3-6.15 1 Chroniques 3.1 1 Chroniques 24.1-24.6
3 wa wana wa Paroshi, Zekaria; na pamoja naye wakahesabiwa kwa nasaba wanaume mia na hamsini.
Esdras 2.3 Néhémie 7.8 Néhémie 10.14
4 Wa wana wa Pahath-Moabu, Eliehoenai, mwana wa Zerahia; na pamoja naye wanaume mia mbili;
Esdras 2.6 Néhémie 10.14 Néhémie 7.11
5 Wa wana wa Zatu, Shekania, mwana wa Yahazieli; na pamoja naye wanaume mia tatu.
6 Na wa wana wa Adini, Ebedi, mwana wa Yonathani; na pamoja naye wanaume hamsini.
Néhémie 10.16 Esdras 2.15 Néhémie 7.20
7 Na wa wana wa Elamu, Yeshaya, mwana wa Athalia; na pamoja naye wanaume sabini.
Esdras 2.31 Esdras 2.7 Néhémie 7.12 Néhémie 7.34
8 Na wa wana wa Shefatia, Zebadia, mwana wa Mikaeli; na pamoja naye wanaume themanini.
Néhémie 11.4 Néhémie 7.9 Esdras 2.4
9 Wa wana wa Yoabu, Obadia, mwana wa Yehieli; na pamoja naye wanaume mia mbili na kumi na wanane.
Esdras 2.6 Néhémie 7.11
10 Na wa wana wa Binui, Shelomithi, mwana wa Yosifia; na pamoja naye wanaume mia na sitini.
11 Na wa wana wa Bebai, Zekaria, mwana wa Bebai; na pamoja naye wanaume ishirini na wanane.
Esdras 10.28 Néhémie 7.16 Esdras 2.11
12 Na wa wana wa Azgadi, Yohana, mwana wa Hakatani; na pamoja naye wanaume mia na kumi.
Néhémie 7.17 Esdras 2.12
13 Na wa wana wa Adonikamu, hawa waliokuwa wa mwisho, na hayo ndiyo majina yao, Elifeleti, na Yeueli, na Shemaya; na pamoja nao wanaume sitini.
Esdras 2.13 Néhémie 7.18
14 Na wa wana wa Bigwai, Uthai, mwana wa Zabudi; na pamoja naye wanaume sabini.
Néhémie 7.19 Esdras 2.14 Néhémie 10.12
15 Nikawakusanya penye mto ushukao kwenda Ahava; na huko tukapiga kambi yetu muda wa siku tatu; nikawakagua watu, na makuhani, wala sikuona hapo wana wa Lawi hata mmoja.
Esdras 8.31 Esdras 8.21 Esdras 7.7 Ezéchiel 3.15 Psaumes 137.1
16 Ndipo nikatuma watu kwenda kumwita Eliezeri, na Arieli, na Shemaya, na Elnathani, na Yaribu, na Elnathani, na Nathani, na Zekaria, na Meshulamu, waliokuwa wakuu; na Yoyaribu, na Elnathani pia, waliokuwa waalimu.
Proverbes 28.2 Esdras 10.39 1 Jean 5.20 1 Rois 3.11 Esdras 8.18
17 Nikawapeleka kwa Ido, mkuu, huko Kasifia; nikawaambia watakayomwambia Ido, na ndugu zake hao Wanethini, huko Kasifia, kwamba watuletee watu watakaohudumu katika nyumba ya Mungu wetu.
Esdras 2.43 Nombres 8.22-8.26 2 Samuel 14.3 Exode 4.15 Nombres 18.6
18 Na kama mkono mwema wa Mungu wetu ulivyokuwa pamoja nasi, wakamletea Ishekeli, mmoja wa wana wa Mali ,mwana wa Lawi, mwana wa Israeli;na Sherebia ,pamoja na wanawe na ndugu zake ,watu kumi na wanawe.
Esdras 7.28 Jérémie 3.15 Esdras 8.22 1 Chroniques 6.19 Néhémie 2.8
19 na Hashabia, na pamoja naye Yeshaya, wa wana wa Merari, na ndugu zake na wana wao, watu ishirini;
1 Chroniques 6.1 1 Chroniques 6.16 Néhémie 10.11 1 Chroniques 6.19 Néhémie 3.17
20 na katika Wanethini, ambao Daudi, na wakuu, walikuwa wamewaweka kwa ajili ya utumishi wa Walawi, Wanethini mia mbili na ishirini; wote wametajwa kwa majina yao.
Esdras 2.43 Esdras 7.7 1 Chroniques 9.2 Esdras 8.17 Philippiens 4.3
21 Ndipo nikaamuru kufunga, hapo penye mto Ahava, ili tupate kujinyenyekeza mbele za Mungu, na kutafuta kwake njia iliyonyoka, kwa ajili yetu sisi wenyewe, na kwa ajili ya watoto wetu, na kwa mali yetu yote.
2 Chroniques 20.3 Lévitique 16.29 1 Samuel 7.6 Lévitique 23.29 Esdras 8.15
22 Maana naliona haya kumwomba mfalme kikosi cha askari na wapanda farasi, ili kutusaidia juu ya adui njiani; kwa maana tulikuwa tumesema na mfalme, tukinena, Mkono wa Mungu u juu ya watu wote wamtafutao, kuwatendea mema; bali uweza wake na ghadhabu yake ni kinyume cha wote wamwachao.
2 Chroniques 15.2 1 Pierre 3.12 Esdras 7.6 Esdras 7.28 Esdras 7.9
23 Basi tukafunga, tukamsihi Mungu wetu kwa ajili ya hayo; naye akatutakabali.
Jérémie 29.12-29.13 1 Chroniques 5.20 Esdras 8.31 Esther 4.16 Esaïe 19.22
24 Ndipo nikawatenga watu kumi na wawili wa wakuu wa makuhani, nao ni Sherebia, na Hashabia, na watu kumi wa ndugu zao pamoja nao,
Esdras 8.18-8.19
25 nami nikawapimia kwa mizani zile fedha, na dhahabu, na vile vyombo, matoleo kwa ajili ya nyumba ya Mungu wetu, ambayo mfalme, na washauri wake, na wakuu wake, na Israeli wote waliokuwapo, walikuwa wameyatoa;
Esdras 8.33 Esdras 1.8 Esdras 7.14-7.16 2 Corinthiens 8.20-8.21 Philippiens 4.8
26 nami nikawapimia mikononi mwao talanta za fedha mia sita na hamsini na vyombo vya fedha talanta mia; na talanta mia za dhahabu;
Esdras 1.9-1.11
27 na mabakuli ishirini ya dhahabu, thamani yake darkoni elfu; na vyombo viwili vya shaba nzuri iliyong’aa, thamani yake sawa na dhahabu.
Lamentations 4.2
28 Kisha nikawaambia, Ninyi mmekuwa watakatifu kwa Bwana, na hivyo vyombo ni vitakatifu; na fedha na dhahabu ni matoleo ya hiari kwa Bwana, Mungu wa baba zenu.
Lévitique 22.2-22.3 Lévitique 21.6-21.8 Esaïe 52.11 1 Rois 7.48-7.51 Nombres 4.19-4.20
29 Basi, angalieni, na kuvitunza vitu hivi, hata mtakapovipima mbele ya wakuu wa makuhani, na Walawi, na wakuu wa mbari za mababa wa Israeli, huko Yerusalemu, katika vyumba vya nyumba ya Bwana.
Esdras 8.33-8.34 Actes 20.31 1 Chroniques 26.20-26.26 2 Timothée 4.5 Marc 13.34-13.35
30 Hivyo makuhani na Walawi wakaupokea uzani wa fedha, na dhahabu, na vyombo, ili kuvileta Yerusalemu nyumbani kwa Mungu wetu.
1 Chroniques 29.2-29.3 Psaumes 122.9 Esdras 8.22 Esaïe 60.13
31 Ndipo tukasafiri toka mtoni Ahava siku ya kumi na mbili ya mwezi wa kwanza, ili kwenda Yerusalemu; na mkono wa Mungu ulikuwa pamoja nasi, akatuokoa na mkono wa adui, na mtu mwenye kutuvizia njiani.
Esdras 7.9 Esdras 8.21-8.22 Esdras 8.15 Actes 26.22 Esaïe 41.10-41.14
32 Tukafika Yerusalemu, tukakaa huko muda wa siku tatu.
Néhémie 2.11 Esdras 7.8-7.9
33 Hata siku ya nne, hizo fedha na dhahabu na vile vyombo vilipimwa ndani ya nyumba ya Mungu, vikatiwa mikononi mwa Meremothi, mwana wa Uria, kuhani; na pamoja naye alikuwapo Eleazari, mwana wa Finehasi; na pamoja nao Yozabadi, mwana wa Yeshua, na Noadia, mwana wa Binui, Walawi;
Néhémie 3.4 Esdras 8.30 Néhémie 3.21 1 Chroniques 28.14-28.18 Néhémie 3.24
34 vile vyombo vyote kwa hesabu na kwa uzani; tena uzani wake wote uliandikwa wakati ule.
35 Na wana wa uhamisho, waliokuwa wametoka katika uhamisho wakamtolea Mungu wa Israeli sadaka za kuteketezwa, ng’ombe kumi na wawili kwa ajili ya Israeli wote, na kondoo waume tisini na sita, na wana-kondoo sabini na saba, na mbuzi waume kumi na wawili, kuwa sadaka ya dhambi, hao wote pia walikuwa sadaka ya kuteketezwa kwa Bwana.
Esdras 6.17 2 Chroniques 29.31-29.32 Luc 1.74-1.75 Psaumes 116.12-116.19 Psaumes 66.10-66.15
36 Wakawapa manaibu wa mfalme, na maliwali wa ng’ambo ya Mto, maagizo ya mfalme; nao wakawapa watu, na nyumba ya Mungu, msaada.
Esdras 7.21-7.24 Esther 9.3 Esdras 5.6-5.17 Apocalypse 12.16 Esaïe 56.6-56.7

Cette Bible est dans le domaine public.