Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

1 Chroniques 26.28
Bible en Swahili de l’est


Portiers du temple et intendants

1 Kwa zamu zao mabawabu; wa Wakora; Meshelemia mwana wa Kore, wa wana wa Ebiasafu.
Psaumes 49.1 1 Chroniques 6.37 1 Chroniques 9.17-9.27 Nombres 26.9-26.11 1 Chroniques 15.18
2 Naye Meshelemia alikuwa na wana; Zekaria mzaliwa wa kwanza, Yediaeli wa pili, Zebadia wa tatu, Yathnieli wa nne;
1 Chroniques 9.21
3 Elamu wa tano, Yohana wa sita, Elioenai wa saba.
4 Naye Obed-edomu alikuwa na wana; Shemaya mzaliwa wa kwanza, Yehozabadi wa pili, Yoa wa tatu, na Sakari wa nne, na Nethaneli wa tano;
1 Chroniques 16.38 1 Chroniques 15.24 1 Chroniques 15.18 1 Chroniques 15.21 1 Chroniques 16.5
5 Amieli wa sita, Isakari wa saba, Peulethai wa nane; kwa jinsi Mungu alivyombariki.
Psaumes 128.1
6 Naye mwanawe Shemaya akazaliwa wana, waliomiliki juu ya mbari ya baba yao; kwa kuwa walikuwa waume mashujaa.
Néhémie 11.14 2 Chroniques 26.17 1 Chroniques 12.28 2 Samuel 2.7 2 Timothée 2.3
7 Wana wa Shemaya; Othni, na Refaeli, na Obedi, na Elzabadi, nduguze walikuwa mashujaa, Elihu, na Semakia.
8 Hao wote walikuwa wana wa Obed-edomu; wao na wana wao na ndugu zao, watu hodari wawezao huo utumishi; watu wa Obed-edomu sitini na wawili.
Matthieu 25.15 2 Corinthiens 3.6 1 Corinthiens 12.4-12.11 1 Pierre 4.11
9 Naye Meshelemia alikuwa na wana na nduguze, watu mashujaa, kumi na wanane.
1 Chroniques 26.1 1 Chroniques 26.14
10 Hosa naye, wa wana wa Merari, alikuwa na wana; Shimri mkuu wao; (kwani ajapokuwa yeye si mzaliwa wa kwanza, babaye alimweka mkuu);
1 Chroniques 16.38 1 Chroniques 5.1-5.2
11 Hilkia wa pili, Tebalia wa tatu, Zekaria wa nne; wana wote wa Hosa pamoja na nduguze walikuwa watu kumi na watatu.
12 Katika hao zilikuwa zamu za mabawabu, yaani, katika hao wakuu, wenye ulinzi sawasawa na ndugu zao, wa kutumika katika nyumba ya Bwana.
1 Chroniques 25.8
13 Nao wakatupiwa kura kwa ajili ya kila lango, wadogo sawasawa na wakubwa, kwa kadiri ya mbari za baba zao.
1 Chroniques 25.8 1 Chroniques 24.31 1 Chroniques 24.5
14 Kura ya mashariki ya lango ikamwangukia Meshelemia. Ndipo wakamtupia kura Zekaria mwanawe, mshauri mwenye busara; na kura yake ikamtokea ya kaskazini.
15 Ya Obed-edomu ya kusini; na ya wanawe nyumba ya akiba.
2 Chroniques 25.24 1 Chroniques 26.17
16 Ya Shupimu na Hosa upande wa magharibi, langoni pa Shalekethi, hapo penye daraja ya kupandia, ulinzi kwa ulinzi.
1 Chroniques 26.10-26.12 Néhémie 12.24 1 Rois 10.5 1 Chroniques 25.8 2 Chroniques 9.4
17 Upande wa mashariki walikuwapo Walawi sita, kaskazini wanne kila siku, kusini wanne kila siku, na wa nyumba ya akiba wawili wawili.
2 Chroniques 8.14 1 Chroniques 9.24
18 Penye Parbari upande wa magharibi, walikuwapo wanne darajani, na wawili huko Parbari.
2 Rois 23.11
19 Hizo ndizo zamu za mabawabu; wa wana wa Wakora, na wa wana wa Merari.
Nombres 16.11
20 Na katika Walawi; Ahia alikuwa juu ya hazina za nyumba ya Mungu, na juu ya hazina za vitu vilivyowekwa wakfu.
1 Chroniques 26.22 1 Chroniques 28.12-28.19 1 Rois 14.26 1 Chroniques 26.24 1 Chroniques 22.14-22.16
21 Wana wa Ladani; wana wa Wagershoni waliokuwa wa Ladani; wakuu wa mbari za mababa waliokuwa wa Ladani, Mgershoni; Yehieli.
1 Chroniques 23.7 1 Chroniques 29.8 1 Chroniques 6.17
22 Wana wa Yehieli; Zethamu, na Yoeli nduguye, juu ya hazina za nyumba ya Bwana.
1 Chroniques 23.8 Néhémie 10.38 1 Chroniques 26.20 1 Chroniques 29.8
23 Wa Waamramu, wa Waishari, wa Wahebroni, wa Wauzieli;
1 Chroniques 23.12 Nombres 3.27 Nombres 3.19
24 na Shebueli, mwana wa Gershomu, mwana wa Musa, alikuwa mtawala hazina zote.
1 Chroniques 24.20 1 Chroniques 23.15-23.16
25 Na nduguze; wa Eliezeri, Rehabia mwanawe, na Ishia mwanawe, na Yoramu mwanawe, na Zikri mwanawe, na Shelomothi mwanawe.
1 Chroniques 23.17-23.18 Exode 18.4 1 Chroniques 23.15
26 Huyo Shelomothi na ndugu zake walikuwa juu ya hazina zote za vitu vilivyowekwa wakfu, alivyoviweka wakfu mfalme Daudi, na hao wakuu wa mbari za mababa, na maakida wa maelfu na wa mamia, na maakida wa jeshi.
2 Samuel 8.11 1 Chroniques 29.2-29.9 1 Chroniques 22.14 1 Chroniques 18.11 Nombres 31.30-31.52
27 Katika nyara zilizopatikana vitani, waliweka wakfu sehemu, ili kuitengeneza nyumba ya Bwana.
2 Rois 12.14 Néhémie 10.32-10.34 Josué 6.19
28 Na vyote alivyoviweka wakfu Samweli mwonaji, na Sauli mwana wa Kishi, na Abneri mwana wa Neri, na Yoabu mwana wa Seruya; na mtu ye yote aliyekiweka wakfu kitu cho chote, kilikuwa chini ya mkono wa Shelomothi na nduguze.
1 Samuel 9.9 2 Samuel 10.9-10.14 1 Samuel 17.55 1 Samuel 14.47-14.51

Magistrats et surveillants en Israël

29 Katika Waishari, Kenania na wanawe walikuwa kwa ajili ya kazi ya nje juu ya Israeli, kuwa maakida na makadhi.
Néhémie 11.16 1 Chroniques 23.4 2 Chroniques 19.8-19.11 1 Chroniques 23.12 1 Chroniques 26.23
30 Katika Wahebroni, Hashabia na nduguze, mashujaa, elfu na mia saba, walikuwa na usimamizi juu ya Israeli ng’ambo ya Yordani upande wa magharibi; kwa ajili ya kazi zote za Bwana, na kwa utumishi wa mfalme.
1 Chroniques 27.17 1 Chroniques 23.19 1 Chroniques 23.12
31 Katika Wahebroni Yeria alikuwa mkuu, yaani, wa hao Wahebroni kwa kufuata vizazi vyao kwa mbari za mababa. Katika mwaka arobaini wa kutawala kwake Daudi wakatafutwa, wakaonekana huko Yazeri ya Gileadi miongoni mwao waume mashujaa.
1 Chroniques 23.19 Josué 21.39 1 Rois 2.11 1 Chroniques 29.27 1 Chroniques 6.81
32 Na nduguze, mashujaa, walikuwa elfu mbili na mia saba, wakuu wa mbari za mababa, ambao mfalme Daudi aliwaweka wawe wasimamizi juu ya Wareubeni, na Wagadi, na nusu kabila ya Wamanase, kwa ajili ya kila neno lililomhusu Mungu, na kwa mambo ya mfalme.
2 Chroniques 19.11 1 Chroniques 23.24 1 Chroniques 12.37 1 Chroniques 24.31 1 Chroniques 15.12

Cette Bible est dans le domaine public.