Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

2 Rois 3.21
Bible en Swahili de l’est


Règne de Joram sur Israël

1 Basi Yoramu mwana wa Ahabu alianza kutawala juu ya Israeli huko Samaria katika mwaka wa kumi na nane wa Yehoshafati mfalme wa Yuda ,akatawala miaka kumi na miwili.
2 Rois 1.17 2 Rois 8.16 1 Rois 22.51
2 Akafanya yaliyo mabaya machoni pa Bwana; ila si kama baba yake na kama mama yake; maana akaiondoa ile nguzo ya Baali aliyoifanya baba yake.
1 Rois 21.25 2 Rois 10.26-10.28 2 Rois 10.18 Exode 23.24 2 Rois 6.31-6.32
3 Pamoja na hayo alishikamana na dhambi za Yeroboamu mwana wa Nebati, ambazo kwa hizo aliwakosesha Israeli; wala hakuziacha.
1 Rois 14.16 2 Rois 13.11 2 Rois 14.24 1 Rois 14.9 2 Rois 17.22
4 Basi Mesha, mfalme wa Moabu, alikuwa mfuga kondoo; naye alikuwa akimlipa mfalme wa Israeli sufu ya wana-kondoo elfu mia, na ya kondoo waume elfu mia.
2 Samuel 8.2 Psaumes 108.9-108.10 1 Chroniques 18.2 Esaïe 16.1-16.2 Psaumes 60.8
5 Lakini ikawa, Ahabu alipokufa, mfalme wa Moabu akamwasi mfalme wa Israeli.
2 Rois 1.1 2 Rois 8.20 2 Chroniques 21.8-21.10
6 Akatoka wakati ule ule mfalme Yoramu katika Samaria, akawahesabu Israeli wote.
1 Rois 20.27 1 Samuel 15.4 1 Samuel 11.8 2 Samuel 24.1-24.25
7 Akaenda akatuma kwa Yehoshafati mfalme wa Yuda, akasema, Mfalme wa Moabu ameniasi; je! Utakwenda pamoja nami tupigane na Moabu? Akasema, Nitakwenda; mimi ni kama wewe, watu wangu ni kama watu wako, farasi zangu ni kama farasi zako.
1 Rois 22.4 2 Chroniques 22.10-22.12 2 Chroniques 18.29-18.32 1 Rois 22.32-22.33 2 Chroniques 22.3-22.4
8 Akauliza, Njia ipi tuiendee? Akajibu, Njia ya jangwa la Edomu.
Nombres 21.4 Malachie 1.2-1.3
9 Basi mfalme wa Israeli akaenda, na mfalme wa Yuda, na mfalme wa Edomu; wakazunguka mwendo wa siku saba; wala hapakuwa na maji kwa jeshi, wala kwa wanyama waliowafuata.
1 Rois 22.47 Exode 17.1 Nombres 20.4 1 Rois 22.27 Juges 4.10
10 Mfalme wa Israeli akasema, Ole wetu! Kwani Bwana amewakutanisha hawa wafalme watatu, awaue mkononi mwa Moabu.
2 Rois 6.33 Proverbes 19.3 Genèse 4.13 Esaïe 8.21 Psaumes 78.34-78.36
11 Lakini Yehoshafati akasema, Je! Hapana hapa nabii wa Bwana, ili tumwulize Bwana kwa yeye? Akajibu mtumishi mmoja wa mfalme wa Israeli, akasema, Yupo hapa Elisha mwana wa Shafati, aliyekuwa akimimina maji juu ya mikono yake Eliya.
1 Rois 22.7 1 Rois 19.21 Jean 13.13-13.14 Jean 13.4-13.5 Juges 20.26-20.28
12 Yehoshafati akasema, Neno la Bwana analo huyu. Basi mfalme wa Israeli, na Yehoshafati, na mfalme wa Edomu, wakamshukia.
2 Rois 5.15 1 Samuel 3.19-3.21 2 Rois 2.21 2 Rois 5.8-5.9 2 Rois 2.24-2.25
13 Elisha akamwambia mfalme wa Israeli, Nina nini mimi nawe? Uende kwa manabii wa babayo, na manabii wa mamayo. Mfalme wa Israeli akamwambia, La, sivyo; kwa kuwa Bwana amewakutanisha hawa wafalme watatu, awaue mkononi mwa Moabu.
1 Rois 22.6 1 Rois 18.19 2 Rois 3.10 1 Rois 22.22-22.25 1 Rois 22.10-22.11
14 Elisha akasema, Kama Bwana wa majeshi aishivyo, ambaye nimesimama mbele zake, kama singemwangalia uso wake Yehoshafati mfalme wa Yuda, singekutazama, wala kuonana nawe.
2 Rois 5.16 1 Rois 17.1 Daniel 5.17-5.23 Jérémie 1.18 1 Samuel 15.26-15.31
15 Ila sasa niletee mpiga kinanda. Ikawa, mpiga kinanda alipokipiga, mkono wa Bwana ukamjia juu yake.
1 Samuel 16.23 Ezéchiel 1.3 1 Rois 18.46 1 Samuel 10.5 Ezéchiel 3.22
16 Akasema, Bwana asema hivi, Fanyeni bonde hili lijae mahandaki.
2 Rois 4.3 Nombres 2.16-2.18
17 Kwa kuwa Bwana asema hivi, Hamutauona upepo, wala hamtaiona mvua, ila bonde hilo litajaa maji; nanyi mtakunywa, ninyi, na ng’ombe zenu, na wanyama wenu.
Psaumes 107.35 Esaïe 41.17-41.18 Esaïe 48.21 1 Rois 18.36-18.39 Exode 17.6
18 Na jambo hili ni jepesi machoni pa Bwana; pia atawatia Wamoabi mikononi mwenu.
Jérémie 32.27 Jérémie 32.17 2 Rois 20.10 Luc 1.37 Esaïe 49.6
19 Nanyi mtapiga kila mji wenye boma, na kila mji ulio mzuri, na kila mti mwema mtaukata, na chemchemi zote za maji mtaziziba, na kila mahali palipo pema mtapaharibu kwa mawe.
Juges 6.16 1 Samuel 15.3 Nombres 24.17 Deutéronome 20.19-20.20 2 Rois 13.17
20 Ikawa asubuhi, wakati wa kutoa sadaka ya unga, tazama, maji yakaja kwa njia ya Edomu, hata nchi ikajaa maji.
Exode 29.39-29.40 Daniel 9.21 Psaumes 78.20 Esaïe 35.6-35.7 1 Rois 18.36
21 Basi Wamoabi wote waliposikia ya kuwa wafalme hao wamekwea ili kupigana nao, walijikusanya pamoja, wote wawezao kuvaa silaha, na wenye umri zaidi, wakasimama mpakani.
Ephésiens 6.14 1 Rois 20.11
22 Wakaamka asubuhi na mapema, na hilo jua likameta-meta juu ya maji, na Wamoabi wakayaona yale maji yaliyowaelekea kuwa ni mekundu kama damu.
23 Wakasema, Ndiyo damu hii; bila shaka hao wafalme wameharibika, wamepigana kila mtu na mwenziwe; basi sasa, enyi Wamoabi, nyara hizo!
Juges 5.30 Exode 15.9 2 Rois 6.18-6.20 2 Chroniques 20.25 2 Rois 7.6
24 Hata walipokuja matuoni kwa Israeli, Waisraeli wakainuka wakawapiga Wamoabi, hata wakakimbia mbele yao; wakaendelea wakiwapiga-piga Wamoabi hata kwao.
Josué 8.20-8.22 Juges 20.40-20.46 1 Thessaloniciens 5.3-5.4
25 Wakaibomoa ile miji; wakatupa katika kila mahali palipo pema kila mtu jiwe lake, wakapajaza; wakaziziba chemchemi zote za maji, wakaikata miti yote iliyo mizuri; mpaka katika Kir-haresethi tu wakayasaza mawe yake; ila wenye kombeo wakauzunguka wakaupiga.
2 Rois 3.19 Esaïe 16.7 Jérémie 48.31 Jérémie 48.36 Esaïe 16.11
26 Naye mfalme wa Moabu alipoona ya kwamba ameshindwa vitani, alitwaa pamoja naye watu mia saba wenye kufuta panga ili wapenye hata kwa mfalme wa Edomu; wala hawakudiriki.
2 Rois 3.9 Amos 2.1
27 Ndipo akamtwaa mwanawe wa kwanza, yeye ambaye angetawala mahali pake, akamtoa awe sadaka ya kuteketezwa juu ya ukuta. Kukawa hasira kuu juu ya Israeli; basi wakatoka kwake, wakarudi kwenda nchi yao wenyewe.
Michée 6.7 Juges 11.31 Deutéronome 12.31 Amos 2.1 Ezéchiel 16.20

Cette Bible est dans le domaine public.