Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

2 Rois 25.26
Bible en Swahili de l’est


1 Ikawa katika mwaka wa kenda wa kutawala kwake, katika mwezi wa kumi, na siku ya kumi ya mwezi huo, Nebukadreza, mfalme wa Babeli, akaja, yeye na jeshi lake lote, kupigana na Yerusalemu, akapanga hema zake kuukabili; nao wakajenga ngome juu yake pande zote.
Jérémie 52.4-52.11 Jérémie 34.1-34.6 Ezéchiel 24.1-24.14 Daniel 4.1-4.18 Ezéchiel 4.1-4.8
2 Basi mji huo ulihusuriwa hata mwaka wa kumi na moja wa mfalme Sedekia.
3 Siku ya kenda ya mwezi wa nne njaa ilikuwa nzito ndani ya mji, hata hapakuwa na chakula kwa watu wa nchi.
Ezéchiel 5.12 Jérémie 38.2 Ezéchiel 14.21 Deutéronome 28.52-28.53 Lévitique 26.26
4 Ndipo mahali pakabomolewa katika ukuta wa mji, watu wote wa vita wakakimbia usiku kwa njia ya lango lililokuwa kati ya zile kuta mbili, karibu na bustani ya mfalme; (basi wale Wakaldayo walikuwa wakiuzuia mji pande zote;) mfalme akaenda kwa njia ya Araba.
Ezéchiel 33.21 Deutéronome 32.30 Deutéronome 32.24-32.25 Deutéronome 28.25 Lévitique 26.17
5 Lakini jeshi la Wakaldayo wakamfuatia mfalme, wakampata katika nchi tambarare ya Yeriko; na jeshi lake lote walikuwa wametawanyika na kumwacha.
Jérémie 52.8 Jérémie 39.5 Amos 2.14-2.16 Jérémie 24.8 Esaïe 30.16
6 Ndipo wakamkamata mfalme, wakamchukua kwa mfalme wa Babeli huko Ribla; wakatoa hukumu juu yake.
2 Rois 23.33 Jérémie 34.21-34.22 Jérémie 21.7 2 Chroniques 33.11 Jérémie 38.23
7 Wakawaua wana wa Sedekia mbele ya macho yake, wakampofusha macho Sedekia, wakamfunga kwa pingu, wakamchukua mpaka Babeli.
Jérémie 39.6-39.7 Jérémie 32.4-32.5 Jérémie 52.10-52.11 Jérémie 22.30 Genèse 21.16

Destruction de Jérusalem et du temple

8 Hata mwezi wa tano, siku ya saba ya mwezi, ndio mwaka wa kumi na kenda wa mfalme Nebukadreza, mfalme wa Babeli, Nebuzaradani, amiri wa askari walinzi, mtumishi wa mfalme wa Babeli, akaingia Yerusalemu.
Jérémie 52.12-52.16 Lamentations 4.12 2 Rois 24.12 Zacharie 8.19 2 Rois 25.27
9 Akaiteketeza nyumba ya Bwana, na nyumba ya mfalme; na nyumba zote za Yerusalemu, naam, kila nyumba kubwa aliiteketeza kwa moto.
Psaumes 74.3-74.7 Amos 2.5 2 Chroniques 36.19 Michée 3.12 Psaumes 79.1
10 Na jeshi lote la Wakaldayo, waliokuwa pamoja na huyo amiri wa askari walinzi, wakazibomoa kuta za Yerusalemu pande zote.
Néhémie 1.3 Jérémie 5.10 Jérémie 52.14-52.23 Jérémie 39.8
11 Na mabaki ya watu waliosalia katika mji, nao wale walioasi, na kumkimbilia mfalme wa Babeli, na mabaki ya watu wote wengine, watu hao Nebuzaradani, amiri wa askari walinzi, akawachukua mateka.
Jérémie 39.9 Jérémie 15.1-15.2 Ezéchiel 12.15-12.16 Jérémie 52.12 Ezéchiel 5.2
12 Lakini huyo amiri wa askari walinzi akawaacha watu walio maskini ili wawe watunza mizabibu na wakulima.
2 Rois 24.14 Jérémie 40.7 Jérémie 39.10 Jérémie 52.16 Ezéchiel 33.24
13 Na zile nguzo za shaba zilizokuwako nyumbani mwa Bwana, na matako, na ile bahari ya shaba, iliyokuwamo nyumbani mwa Bwana, Wakaldayo wakavivunja vipande vipande, wakaichukua shaba yake yote mpaka Babeli.
2 Chroniques 36.18 1 Rois 7.15 Jérémie 52.17-52.20 2 Rois 20.17 2 Chroniques 4.2-4.6
14 Nayo masufuria, na majembe, na makasi, na miiko, na vyombo vyote vya shaba walivyokuwa wakivitumia, wakavichukua vyote.
Exode 27.3 1 Rois 7.47-7.50 Exode 38.3 2 Chroniques 4.20-4.22 2 Chroniques 24.14
15 Na vyetezo, na mabakuli; vilivyokuwa vya dhahabu katika dhahabu, na vilivyokuwa vya fedha katika fedha, amiri wa askari walinzi akavichukua.
Daniel 5.2-5.3 1 Rois 7.48-7.51 Exode 37.23 2 Chroniques 24.14 Nombres 7.13-7.14
16 Zile nguzo mbili, na ile bahari moja, na yale matako, Sulemani alivyoifanyia nyumba ya Bwana; shaba ya vyombo hivyo vyote haikuwa na uzani.
1 Rois 7.47
17 Urefu wa nguzo moja ulikuwa dhiraa kumi na nane, na kichwa cha shaba kilikuwa juu yake; na urefu wa kichwa ulikuwa dhiraa tatu; na mapambo ya wavu na makomamanga juu ya kichwa hicho kote kote, yote yalikuwa ya shaba. Nayo nguzo ya pili ilikuwa vivyo hivyo, pamoja na ule wavu.
1 Rois 7.15-7.22 Jérémie 52.21-52.23
18 Na amiri wa askari walinzi akamtwaa Seraya, kuhani mkuu, na Sefania, kuhani wa pili, na wale walinzi watu wa mlango;
Esdras 7.1 1 Chroniques 6.14 Jérémie 29.25 Jérémie 21.1 Jérémie 52.24
19 na katika mji akamtwaa towashi mmoja, aliyewasimamia watu wa vita; na watu watano katika wale waliosimama mbele ya mfalme, walioonekana mjini; na katibu wa jemadari wa jeshi, aliyewaandika watu wa nchi; na watu sitini katika watu wa nchi, walioonekana mjini.
Esther 1.14
20 Kisha Nebuzaradani, amiri wa askari walinzi, akawatwaa hao, akawaleta kwa mfalme wa Babeli huko Ribla.
Lamentations 4.16 2 Rois 23.33 Jérémie 52.26-52.27
21 Naye mfalme wa Babeli akawapiga, na kuwaua huko Ribla katika nchi ya Hamathi. Hivyo Yuda wakachukuliwa utumwani kutoka nchi yao.
Deutéronome 28.64 2 Rois 23.27 Deutéronome 28.36 Ezéchiel 24.14 Jérémie 24.9-24.10

Révolte contre le gouverneur de Juda

22 Na kwa habari ya watu waliosalia katika nchi ya Yuda, aliowasaza Nebukadreza, mfalme wa Babeli, akamweka Gedalia mwana wa Ahikamu mwana wa Shafani awe liwali juu yao.
Jérémie 39.14 2 Rois 22.12 2 Chroniques 34.20 Jérémie 40.5-40.12 Jérémie 26.24
23 Kisha, wakuu wote wa majeshi, wao na watu wao, waliposikia kwamba mfalme wa Babeli amemweka Gedalia kuwa liwali, wakamwendea Gedalia huko Mispa; nao ni hawa, Ishmaeli mwana wa Nethania, na Yohana mwana wa Karea, na Seraya mwana wa Tanhumethi Mnetofa, na Yezania mwana wa Mmaaka, wao na watu wao.
Jérémie 40.7-40.9 Josué 18.26 Jérémie 40.11-40.12
24 Na Gedalia akawaapia wao na watu wao, akawaambia, Msiogope kwa ajili ya watumishi wa Wakaldayo; kaeni katika nchi; mkamtumikie mfalme wa Babeli; itakuwa vyema kwenu.
2 Samuel 14.11 Jérémie 40.9-40.10 Jérémie 43.6 2 Samuel 19.23 Ezéchiel 33.24-33.29
25 Lakini ikawa katika mwezi wa saba Ishmaeli mwana wa Nethania, mwana wa Elishama, mmoja wa wazao wa kifalme, na watu kumi pamoja naye, wakamwendea Gedalia, wakampiga hata akafa, na hao Wayahudi na Wakaldayo waliokuwa pamoja naye huko Mispa.
2 Rois 11.1 Zacharie 8.19 Jérémie 40.15-41.15 Zacharie 7.5
26 Wakaondoka watu wote, wadogo kwa wakubwa, pamoja na wakuu wa majeshi, wakainuka kwenda Misri; kwa kuwa waliwaogopa Wakaldayo.
Jérémie 43.4-43.7 Jérémie 41.16-41.18 Jérémie 42.14-42.22

Libération de Jojakin

27 Ikawa katika mwaka wa thelathini na saba wa kuhamishwa kwake Yekonia mfalme wa Yuda ,katika mwezi wa kumi na mbili ,siku ya ishirini na saba ya mwezi ,Evil-merodaki,mfalme wa Babeli ,katika mwaka wa kwanza wa kutawala kwake,akamwinua kichwa Yekonia,mfalme wa Yuda,akamtoa gerezani.
Jérémie 52.31-52.34 Genèse 40.20 Genèse 40.13 2 Rois 24.12 Jérémie 24.5-24.6
28 Akasema naye maneno mazuri, akaweka kiti chake cha enzi juu ya viti vya enzi vya wafalme waliokuwa pamoja naye huko Babeli;
Daniel 2.37 Daniel 5.18-5.19 Jérémie 27.6-27.11
29 naye akambadilishia mavazi yake ya gerezani, akala chakula mbele yake daima, siku zote za maisha yake.
2 Samuel 9.7 Luc 15.22 Zacharie 3.4 Esther 8.15 Esther 4.4
30 Na kwa posho yake, alipewa posho ya daima na mfalme, siku kwa siku sehemu, siku zote za maisha yake.
Néhémie 12.47 Néhémie 11.23 Matthieu 6.11 Genèse 48.15-48.16 Daniel 1.5

Cette Bible est dans le domaine public.