Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

2 Rois 10.4
Bible en Swahili de l’est


1 Basi Ahabu alikuwa na wana sabini katika Samaria. Yehu akaandika barua, akazipeleka Samaria kwa wakuu wa Yezreeli, yaani, wazee na hao walezi wa wana wa Ahabu, kusema,
1 Rois 16.28 1 Rois 13.32 Juges 8.30 2 Rois 5.3 Juges 12.14
2 Barua hii mara ikiwawasilia, kwa kuwa mna wana wa bwana wenu pamoja nanyi, tena kwenu kuna magari na farasi, na mji wenye boma, na silaha;
2 Rois 5.6
3 basi mtazameni yeye aliye mwema na hodari miongoni mwa wana wa bwana wenu, mkamweke kitini mwa babaye, mkaipiganie nyumba ya bwana wenu.
Deutéronome 17.14-17.15 2 Samuel 2.8-2.9 1 Samuel 10.24 1 Rois 1.24-1.25 2 Samuel 2.12-2.17
4 Lakini wao wakaogopa mno, wakasema, Tazama, wafalme wawili hawakusimama mbele yake; tupateje sisi kusimama?
2 Rois 9.24 2 Rois 9.27 Nahum 1.6 Luc 14.31 Esaïe 27.4
5 Kisha yeye aliyekuwa juu ya nyumba, na yeye aliyekuwa juu ya mji, na wazee, na walezi, wakatuma ujumbe kwa Yehu, wakisema, Sisi tu watumwa wako, kila neno utakalotuambia, tutalifanya; hatutamfanya mtu awaye yote kuwa mfalme; ufanye yaliyo mema machoni pako.
1 Rois 20.4 1 Rois 20.32 Josué 9.11 Josué 9.8 2 Rois 18.14
6 Ndipo akawaandikia barua ya pili, kusema, Mkiwa upande wangu, na sauti yangu mkiisikia, vitwaeni vichwa vyao hao watu, wana wa bwana wenu, mkanijie kama wakati huu kesho hapa Yezreeli. Na hao wana wa mfalme, watu sabini, walikuwako kwa wakuu wa mji waliowalea.
Job 21.19 2 Rois 9.32 Matthieu 12.30 Luc 9.50 Josué 7.24-7.25
7 Ikawa, barua ilipowawasilia, waliwatwaa hao wana wa mfalme, wakawaua, watu sabini, wakatia vichwa vyao katika makapu, wakampelekea huko Yezreeli.
1 Rois 21.21 2 Rois 11.1 Matthieu 14.8-14.11 Juges 9.5-9.57 2 Rois 10.9
8 Akaja mjumbe, akamwambia, akasema, Wamevileta vile vichwa vya wana wa mfalme. Akasema, Viwekeni chungu mbili penye maingilio ya lango hata asubuhi.
2 Samuel 11.18-11.21 Deutéronome 21.23 1 Rois 21.14 Marc 6.28
9 Ikawa asubuhi, akatoka, akasimama, akawaambia watu wote, Ninyi ni wenye haki; tazameni, mimi nalifanya fitina juu ya bwana wangu, nikamwua; ila ni nani aliyewapiga hawa wote?
2 Rois 9.14-9.24 Osée 1.4 Esaïe 5.3 1 Samuel 12.3
10 Jueni basi ya kwamba halianguki chini lo lote la neno la Bwana, alilolinena Bwana juu ya nyumba ya Ahabu; kwa maana Bwana ameyafanya hayo aliyoyanena kwa kinywa cha mtumishi wake Eliya.
1 Rois 21.29 1 Rois 21.19 2 Rois 9.7-9.10 1 Rois 21.21-21.24 1 Samuel 3.19
11 Hivyo Yehu akawapiga wote waliosalia wa nyumba ya Ahabu katika Yezreeli, na hao wakuu wake wote, na rafiki zake, na makuhani wake, hata hakumwachia aliyesalia hata mmoja.
Job 18.19 1 Rois 22.6 Psaumes 109.13 Psaumes 125.5 1 Rois 15.29
12 Akaondoka, akashika njia akaenda Samaria. Hata njiani karibu na nyumba ya kukatia manyoya kondoo, ya wachungaji.
13 Yehu akakutana na ndugu za Ahazia mfalme wa Yuda, akawauliza, Ni nani ninyi? Wakamjibu, Sisi tu ndugu zake Ahazia; tunashuka kuwasalimu wana wa mfalme na wana wa malkia.
2 Rois 8.29 2 Rois 8.24 2 Chroniques 21.17 2 Chroniques 22.1-22.10 2 Rois 9.21-9.27
14 Akasema, Wakamateni wa hai. Wakawakamata wa hai, wakawaua penye birika ya nyumba ya kukatia manyoya kondoo, watu arobaini na wawili; wala hakumsaza mtu wao awaye yote.
2 Rois 10.10-10.11 2 Rois 10.6 2 Chroniques 22.8 2 Rois 8.18 2 Rois 11.1
15 Alipotoka huko akamkuta Yehonadabu mwana wa Rekabu akija kumlaki; akamsalimu akamwambia, Je! Moyo wako umenyoka, kama moyo wangu ulivyo pamoja na moyo wako? Akajibu Yehonadabu, Ndio. Yehu akamwambia, Kama ndio, nipe mkono wako. Akampa mkono, akamkalisha pamoja naye garini.
Esdras 10.19 1 Chroniques 2.55 Ezéchiel 17.18 Jérémie 35.14-35.19 Galates 2.9
16 Akasema, Fuatana nami, ukaone wivu wangu kwa Bwana. Wakampandisha garini mwake.
1 Rois 19.10 Nombres 24.13-24.16 Matthieu 6.5 Nombres 23.4 Proverbes 27.2
17 Naye alipofika Samaria, aliwapiga wote waliomsalia Ahabu katika Samaria, hata akamwangamiza, sawasawa na neno la Bwana alilomwambia Eliya.
2 Rois 9.8 2 Chroniques 22.8 1 Rois 21.21 Malachie 4.1 2 Rois 10.10-10.11

Politique religieuse de Jéhu

18 Yehu akawakusanya watu wote, akawaambia, Ahabu alimtumikia Baali kidogo; bali Yehu atamtumikia sana.
1 Rois 16.31-16.32 1 Rois 18.40 1 Rois 18.22 Philippiens 4.8 1 Rois 18.19
19 Basi niitieni manabii wote wa Baali, wote wamwabuduo, na makuhani wake wote; mtu asikose kuwapo hata mmoja. Maana ninayo dhabihu kubwa ya kumtolea Baali; ye yote atakayekosa kuwapo hataishi. Lakini Yehu alifanya hayo kwa hila, ili awaharibu waliomwabudu Baali.
1 Rois 22.6 1 Rois 18.19 1 Thessaloniciens 2.3 2 Corinthiens 11.13-11.15 Job 13.7
20 Yehu akasema, Takaseni kusanyiko la dini kwa Baali. Wakalitangaza.
Joël 1.14 Exode 32.5 1 Rois 21.12 1 Rois 18.19-18.20
21 Yehu akatuma wajumbe katika Israeli yote, nao wote waliomwabudu Baali wakaja, wala hakusalia mtu ye yote asiyekuja. Wakaingia nyumbani mwa Baali; ikajaa nyumba ya Baali tangu mlango hata mlango.
1 Rois 16.32 Apocalypse 16.16 Joël 3.11-3.14 Juges 16.27 Joël 3.2
22 Akamwambia yule aliyekuwa juu ya hazina ya mavazi, Uwatolee mavazi wote wanaomwabudu Baali. Akawatolea mavazi.
Matthieu 22.11-22.12 Exode 28.2
23 Akaingia Yehu na Yehonadabu mwana wa Rekabu nyumbani mwa Baali, akawaambia waliomwabudu Baali, Tafuteni mkaangalie, asiwepo hapa pamoja nanyi mtu amtumikiaye Bwana, ila wamwabuduo Baali peke yao.
Matthieu 25.32-25.33 Matthieu 13.30 Matthieu 13.41
24 Wakaingia ili watoe dhabihu na sadaka za kuteketezwa. Basi Yehu alikuwa amejiwekea nje watu themanini, akasema, Mtu mmoja akiokoka wa watu niliowatia mikononi mwenu, amwachaye huyo, roho yake itakuwa badala ya roho yake.
1 Rois 20.30-20.42
25 Ikawa mara alipokwisha kutoa sadaka ya kuteketezwa, Yehu akawaambia walinzi na maakida, Ingieni mwapige; mtu awaye yote asitoke. Basi wakawapiga kwa makali ya upanga; walinzi na maakida wakawatupa nje, wakaenda mpaka mji wa nyumba ya Baali.
1 Rois 18.40 Apocalypse 16.6-16.7 Deutéronome 13.6-13.11 Ezéchiel 9.5-9.7 Exode 32.27
26 Wakazitoa nguzo zilizokuwamo nyumbani mwa Baali, wakaziteketeza.
1 Rois 14.23 2 Rois 19.18 2 Samuel 5.21 2 Rois 3.2
27 Wakaibomoa nguzo ya Baali, na kuiangusha nyumba ya Baali, wakaifanya choo hata leo.
Daniel 3.29 Daniel 2.5 Esdras 6.11 1 Rois 16.32 2 Rois 23.7-23.14
28 Ndivyo Yehu alivyomharibu Baali katika Israeli.
29 Walakini katika makosa yake Yeroboamu mwana wa Nebati, ambayo kwa hayo aliwakosesha Israeli, Yehu hakutoka katika kuyafuata, yaani, ndama za dhahabu zilizokuwako katika Betheli na Dani.
1 Rois 12.28-12.30 1 Rois 14.16 1 Rois 13.33-13.34 2 Rois 15.18 Osée 13.2
30 Bwana akamwambia Yehu, Kwa kuwa umetenda vema kwa kufanya vilivyo haki machoni pangu, kuitendea nyumba ya Ahabu sawasawa na yote yaliyomo moyoni mwangu, wana wako wa kizazi cha nne watakaa kitini mwa Israeli.
2 Rois 10.35 2 Rois 13.1 2 Rois 13.10 2 Rois 14.23 1 Rois 21.22
31 Lakini Yehu hakuangalia, aende katika sheria ya Bwana, Mungu wa Israeli, kwa moyo wake wote; hakutoka katika makosa ya Yeroboamu, ambayo kwa hayo aliwakosesha Israeli.
2 Rois 10.29 Proverbes 4.23 Hébreux 2.1 Deutéronome 4.23 2 Rois 3.3
32 Siku zile Bwana akaanza kupunguza Israeli. Hazaeli akawapiga mipakani mwote mwa Israeli;
2 Rois 8.12 1 Rois 19.17 2 Rois 13.25 2 Rois 13.22 2 Rois 14.25
33 kutoka Yordani upande wa mashariki, nchi yote ya Gileadi, na ya Wagadi, na Wareubeni, na Wamanase, kutoka Aroeri iliopo karibu na bonde la Arnoni, yaani, Gileadi, na Bashani.
Amos 1.3-1.4 Deutéronome 2.36 Nombres 32.33-32.42 Deutéronome 3.12-3.17 Josué 13.9-13.12
34 Basi mambo yote ya Yehu yaliyosalia, na yote aliyoyafanya, na ushujaa wake, je! Hayakuandikwa katika kitabu-cha-tarehe cha wafalme wa Israeli?
2 Rois 12.19 1 Rois 14.19 1 Rois 11.41 1 Rois 14.29 2 Rois 13.8
35 Yehu akalala na babaze; wakamzika katika Samaria. Na Yehoahazi mwanawe akatawala mahali pake.
1 Rois 14.20 2 Rois 13.1 1 Rois 14.31 2 Samuel 7.12 1 Rois 2.10
36 Na muda Yehu aliotawala juu ya Israeli katika Samaria ulikuwa miaka ishirini na minane.

Cette Bible est dans le domaine public.