Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

2 Samuel 15.12
Bible en Swahili de l’est


Révolte d’Absalom

1 Ikawa baada ya hayo, Absalomu akajiwekea tayari gari na farasi, na watu hamsini wa kupiga mbio mbele yake.
1 Rois 1.5 2 Samuel 12.11 Psaumes 20.7 1 Samuel 8.11 Proverbes 11.2
2 Tena Absalomu huondoka asubuhi na mapema, na kusimama kando ya njia ya lango; kisha ikawa, mtu ye yote aliyekuwa na neno, lililokuwa halina budi kufika kwa mfalme ili kuhukumiwa, Absalomu humwita mtu huyo kwake, na kumwuliza, Wewe u mtu wa mji gani? Naye akasema, Mtumwa wako ni mtu wa kabila fulani ya Israeli.
Exode 18.14 Job 24.14 2 Samuel 19.8 Exode 18.16 Matthieu 27.1
3 Naye Absalomu humwambia, Tazama, maneno yako ni mema yenye haki; lakini hapana mtu aliyeagizwa na mfalme kukusikiliza.
Exode 21.17 Daniel 11.21 Proverbes 12.2 Proverbes 30.17 Matthieu 15.4
4 Tena Absalomu husema, Laiti mimi ningewekwa kuwa mwamuzi katika nchi hii, ili kila mtu mwenye neno au daawa aje kwangu, nimpatie haki yake!
Juges 9.29 Proverbes 27.2 2 Pierre 2.19 Proverbes 25.6 Juges 9.1-9.5
5 Tena ikawa hapo alipokaribia mtu ye yote kumsujudia, hunyosha mkono wake, na kumshika, na kumbusu.
2 Samuel 14.33 Psaumes 10.9-10.10 Proverbes 26.25 Psaumes 55.21
6 Hivyo ndivyo Absalomu alivyowatendea Israeli wote, waliomwendea mfalme ili wapate hukumu; na hivyo Absalomu akawadanganya watu wa Israeli.
Romains 16.18 2 Pierre 2.3 Proverbes 11.9
7 Hata ikawa mwisho wa miaka minne, Absalomu akamwambia mfalme Tafadhali uniache niende nikaondoe nadhiri yangu, niliyomwekea Bwana huko Hebroni.
1 Samuel 16.13 Matthieu 23.13 Proverbes 21.27 2 Samuel 13.38 Esaïe 58.4
8 Maana mimi mtumishi wako naliweka nadhiri hapo nilipokuwa nikikaa Geshuri katika Shamu, nikasema, Kama Bwana akinirudisha Yerusalemu kweli, ndipo nitamtumikia Bwana.
Genèse 28.20-28.21 2 Samuel 13.37-13.38 1 Samuel 1.11 1 Samuel 16.2 2 Samuel 14.23
9 Naye mfalme akamwambia, Enenda na amani. Basi akaondoka, akaenda Hebroni.
10 Lakini Absalomu akapeleka wapelelezi katika kabila zote za Israeli kusema, Mara mtakaposikia sauti ya tarumbeta, ndipo mtakaposema Absalomu anamilikl huko Hebroni.
2 Samuel 14.30 Psaumes 73.18-73.19 2 Samuel 19.10 2 Samuel 2.1 1 Chroniques 12.23
11 Na watu mia mbili walioalikwa wakatoka Yerusalemu pamoja na Absalomu, wakaenda katika ujinga wao wasijue neno lo lote.
1 Samuel 9.13 1 Samuel 22.15 1 Samuel 16.3-16.5 Matthieu 10.16 Proverbes 14.15
12 Absalomu naye akatuma kumwita Ahithofeli Mgiloni, mshauri wake Daudi, kutoka katika mji wake, yaani, Gilo, alipokuwa akitoa dhabihu. Fitina yao ikawa na nguvu; maana watu waliokuwa pamoja na Absalomu wakazidi kuwa wengi.
Josué 15.51 2 Samuel 15.31 Psaumes 41.9 2 Samuel 17.23 Psaumes 55.12-55.14
13 Mjumbe akamfikilia Daudi, akasema, Mioyo ya watu wa Israeli inashikamana na Absalomu.
Juges 9.3 2 Samuel 15.6 Matthieu 21.9 2 Samuel 3.36 Matthieu 27.22
14 Basi Daudi akawaambia watumishi wake wote waliokuwa pamoja naye Yerusalemu, Ondokeni, tukakimbie kwa kuwa tusipokimbia hapana mtu miongoni mwetu atakayeokoka mikononi mwa Absalomu; haya! Fanyeni haraka, tuondoke, asitupate kwa upesi, na kutuletea maovu, na kuupiga mji huu kwa makali ya upanga.
2 Samuel 19.9 Psaumes 3.1-3.8 Psaumes 55.3-55.11 2 Samuel 23.16-23.17 Psaumes 137.5-137.6
15 Hao watumishi wa mfalme wakamwambia mfalme, Angalia, sisi watumishi wako tu tayari kutenda lo lote atakalolichagua bwana wetu mfalme.
Jean 6.66-6.69 Jean 15.14 Luc 22.28-22.29 Proverbes 18.24
16 Basi mfalme akatoka na watu wa nyumbani mwake wote wakafuatana naye. Mfalme akaacha wanawake kumi, masuria, ili kuitunza nyumba.
2 Samuel 16.21-16.22 2 Samuel 20.3 1 Samuel 25.42 2 Samuel 12.11 Juges 4.10
17 Mfalme akatoka, na watu wote wakamfuata; wakakaa kidogo katika Beth-merhaki.
Psaumes 3.1-3.2 Ecclésiaste 10.7 Psaumes 66.12
18 Watumishi wake wote wakapita karibu naye; na Wakerethi wote, na Wapelethi wote, na Wagiti wote, watu mia sita walioandamana naye kutoka Gathi, wakapita mbele ya mfalme.
2 Samuel 8.18 1 Samuel 30.14 1 Chroniques 18.17 2 Samuel 20.7 2 Samuel 20.23
19 Ndipo mfalme akamwambia Itai, Mgiti, Mbona wewe unakwenda pamoja nasi? Rudi, ukakae na mfalme; maana wewe u mgeni, tena u mtu uliyefukuzwa mahali pako mwenyewe.
2 Samuel 18.2 Ruth 1.11-1.13
20 Kwa kuwa umekuja jana tu kwa nini nikusumbue leo, na kukuzungusha huko na huko pamoja nasi nami hapa naenda niwezapo kwenda? Rudi wewe, ukawarudishe na ndugu zako; rehema na kweli ziwe pamoja nawe.
1 Samuel 23.13 2 Samuel 2.6 Jean 1.17 Hébreux 11.37-11.38 Proverbes 14.22
21 Naye Itai akamjibu mfalme akasema, Kama aishivyo Bwana, na bwana wangu mfalme aishivyo, hakika yake kila mahali atakapokuwapo mfalme, bwana wangu, ikiwa ni kwa kufa au ikiwa ni kwa kuishi, ndipo atakapokuwapo na mtumwa wako.
Ruth 1.16-1.17 Proverbes 17.17 2 Corinthiens 7.3 2 Rois 2.4 Proverbes 18.24
22 Basi Daudi akamwambia Itai, Haya, enenda ukavuke. Akavuka Itai, Mgiti na watu wake wote, na watoto wadogo wote waliokuwa pamoja naye.
23 Na nchi yote ikalia kwa sauti kuu, nao watu wote wakavuka, mfalme mwenyewe naye akavuka kile kijito Kidroni, na hao watu wote wakavuka, wakielekea njia ya nyika.
2 Samuel 16.2 1 Rois 2.37 Jean 18.1 2 Chroniques 29.16 Matthieu 3.1
24 Na tazama, Sadoki naye akaja, na Walawi wote pamoja naye, huku wakilichukua sanduku la agano la Mungu; kisha wakalitua hilo sanduku la Mungu; Abiathari naye akapanda juu, hata watu wote walipokwisha kuutoka mji.
2 Samuel 8.17 Nombres 4.15 2 Samuel 20.25 1 Samuel 22.20 Nombres 7.9
25 Naye mfalme akamwambia Sadoki, Rudisha sanduku la Mungu mjini; nikipata kibali machoni pa Bwana atanirudisha, na kunionyesha tena sanduku hili, na maskani yake;
Exode 15.13 Jérémie 25.30 Psaumes 42.1-42.2 Psaumes 122.1 Psaumes 26.8
26 lakini akisema kama hivi, Mimi si radhi nawe kabisa; basi, mimi hapa, na anitendee kama aonavyo kuwa vyema.
1 Samuel 3.18 2 Samuel 22.20 1 Rois 10.9 2 Chroniques 9.8 Nombres 14.8
27 Kisha mfalme akamwambia Sadoki, kuhani, Angalia, rudini mjini kwa amani, na wana wenu wawili pamoja nanyi,Ahimaasi,mwana wako, na Yonathani,mwana wa Abiathari.
2 Samuel 17.17 1 Samuel 9.9 2 Samuel 15.36 2 Samuel 24.11 2 Samuel 15.34
28 Angalia, mimi nitangoja penye vivuko vya jangwani, hata litakaponifikilia neno la kunipasha habari kutoka kwenu.
2 Samuel 17.16 2 Samuel 15.23 2 Samuel 17.1 2 Samuel 16.2
29 Basi Sadoki na Abiathari wakalichukua sanduku la Mungu, wakalirudisha Yerusalemu; wakakaa huko.
30 Daudi akapanda akishika njia ya kuupandia mlima wa Mizeituni, akilia alipokuwa akipanda; naye alikuwa amejifunika kichwa chake, akaenda hana viatu; na watu wote waliokuwa pamoja naye wakajifunika vichwa vyao, kila mmoja wao, wakapanda juu, wakilia walipopanda.
Esther 6.12 2 Samuel 19.4 Jérémie 14.3-14.4 Esaïe 20.2-20.4 Ezéchiel 24.17
31 Mtu mmoja akamwambia Daudi ya kwamba, Ahithofeli yu katika hao waliopatana na Absalomu; Daudi akasema, Ee Bwana, nakusihi, uligeuze shauri la Ahithofeli liwe ubatili.
2 Samuel 17.14 2 Samuel 17.23 2 Samuel 16.23 Psaumes 3.1 Psaumes 41.9
32 Ikawa, Daudi alipofika juu, hapo Mungu alipoabudiwa, tazama, Hushai, Mwarki, akaja kumlaki na joho lake limeraruliwa, tena ana udongo kichwani mwake.
Josué 16.2 2 Samuel 1.2 Psaumes 4.1-4.3 1 Rois 11.7 1 Rois 8.44-8.45
33 Daudi akamwambia, Ukienda mbele pamoja nami, utakuwa mzigo kwangu;
2 Samuel 19.35
34 lakini ukirudi mjini, na kumwambia Absalomu, Nitakuwa mtumishi wako, Ee mfalme; kama vile nilivyokuwa mtumishi wa baba yako tokea zamani, ndivyo nitakavyokuwa mtumishi wako sasa; ndipo utayavunja mashauri ya Ahithofeli kwa ajili yangu.
Matthieu 10.16 Josué 8.2 2 Samuel 17.5-17.14 2 Samuel 16.16-16.19 2 Samuel 15.20
35 Je! Hawako Sadoki na Abiathari, makuhani, pamoja nawe huko? Basi itakuwa, kila neno utakalolisikia katika jumba la mfalme, utawaambia Sadoki na Abiathari, makuhani.
2 Samuel 17.15-17.16
36 Angalia, wanao huko pamoja nao wana wao wawili, Ahimaasi, mwana wa Sadoki, na Yonathani, mwana wa Abiathari; nanyi kwa mikono yao mtanipelekea habari ya kila neno mtakalolisikia.
2 Samuel 17.17 2 Samuel 15.27 2 Samuel 18.19-18.33
37 Basi Hushai, rafiki wa Daudi, akaingia ndani ya mji; naye Absalomu akafika akaingia Yerusalemu.
2 Samuel 16.15-16.16 1 Chroniques 27.33

Cette Bible est dans le domaine public.