Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Genèse 9.13
Bible en Swahili de l’est


Noé et ses fils

1 Mungu akambariki Nuhu na wanawe, akawaambia, Zaeni, mkaongezeke, mkaijaze nchi.
Genèse 1.28 Genèse 8.17 Genèse 9.7 Genèse 1.22 Psaumes 128.3-128.4
2 Kila mnyama wa katika nchi atawaogopa ninyi na kuwahofu, na kila ndege wa angani: pamoja na vitu vyote vilivyojaa katika ardhi, na samaki wote wa baharini; vimetiwa mikononi mwenu.
Jacques 3.7 Job 5.22-5.23 Genèse 2.19 Genèse 1.28 Ezéchiel 34.25
3 Kila kiendacho kilicho hai kitakuwa chakula chenu, kama nilivyowapa mboga za majani, kadhalika nawapeni hivi vyote.
Deutéronome 12.15 Romains 14.14 Colossiens 2.16 Romains 14.3 Psaumes 104.14-104.15
4 Bali nyama pamoja na uhai, yaani, damu yake, msile.
Deutéronome 12.23 Deutéronome 12.16 Actes 15.20 Actes 15.29 Lévitique 17.10-17.14
5 Hakika damu yenu ya uhai wenu nitaitaka; na kwa mkono wa kila mnyama nitaitaka; na kwa mkono wa mwanadamu, kwa mkono wa ndugu ya mtu nitataka uhai wa mwanadamu.
Exode 21.28-21.29 Genèse 4.9-4.10 Exode 21.12 Matthieu 23.35 Lévitique 19.16
6 Atakayemwaga damu ya mwanadamu, damu yake huyo itamwagwa na mwanadamu, maana kwa mfano wake Mungu alimfanya mwanadamu.
Lévitique 24.17 Matthieu 26.52 Exode 21.12-21.14 Apocalypse 13.10 Genèse 1.26-1.27
7 Nanyi zaeni, mkaongezeke; zaeni sana katika nchi, mkaongezeke ndani yake.
Genèse 9.1 Genèse 1.28 Genèse 8.17 Genèse 9.19
8 Mungu akamwambia Nuhu, na wanawe pamoja naye, akisema,
9 Mimi, tazama, nalithibitisha agano langu nanyi; tena na uzao wenu baada yenu;
Genèse 6.18 Genèse 22.17 Genèse 17.7-17.8 Jérémie 31.35-31.36 Romains 1.3
10 tena na kila kiumbe hai kilichoko pamoja nanyi, ndege, na mnyama wa kufugwa, na kila mnyama wa mwitu katika nchi pamoja nanyi; wote wanaotoka katika safina, hata kila kilicho hai katika nchi.
Psaumes 36.5-36.6 Job 41.1-41.34 Jonas 4.11 Psaumes 145.9 Job 38.1-38.41
11 Na agano langu nitalithibitisha nanyi; wala kila chenye mwili hakitafutwa tena kwa maji ya gharika; wala hakutakuwa tena gharika, baada ya hayo, kuiharibu nchi.
Esaïe 54.9 Genèse 8.21-8.22 Genèse 7.21-7.23 2 Pierre 3.11 2 Pierre 3.7
12 Mungu akasema, Hii ndiyo ishara ya agano nifanyalo kati yangu na ninyi, na kila kiumbe hai kilichoko pamoja nanyi, kwa vizazi vyote hata milele;
Genèse 17.11 Josué 2.12 Exode 13.16 1 Corinthiens 11.23-11.25 Matthieu 26.26-26.28
13 Mimi nauweka upinde wangu winguni, nao utakuwa ni ishara ya agano kati yangu na nchi.
Ezéchiel 1.28 Apocalypse 10.1 Apocalypse 4.3
14 Hata itakuwa nikitanda mawingu juu ya nchi, upinde utaonekana winguni,
15 nami nitalikumbuka agano langu, lililoko kati yangu na ninyi, na kila kiumbe hai katika wote wenye mwili, wala maji hayatakuwa gharika tena kuwaharibu wote wenye mwili.
Ezéchiel 16.60 Deutéronome 7.9 1 Rois 8.23 Lévitique 26.42-26.45 Exode 28.12
16 Basi huo upinde utakuwa winguni; nami nitauangalia nipate kulikumbuka agano la milele lililoko kati ya Mungu na kila kiumbe hai katika wote wenye mwili kilichoko katika nchi.
Genèse 17.13 Genèse 17.19 Esaïe 54.8-54.10 2 Samuel 23.5 Genèse 9.9-9.11
17 Mungu akamwambia Nuhu, Hii ndiyo ishara ya agano nililoliweka kati yangu na wote wenye mwili walioko katika nchi.
18 Wana wa Nuhu waliotoka katika safina, ni Shemu, na Hamu, na Yafethi; na Hamu ndiye baba wa Kanaani.
Genèse 10.1 Genèse 10.6 1 Chroniques 1.4 Genèse 9.23 Genèse 9.25-9.27
19 Hawa watatu walikuwa wana wa Nuhu na kwa hao nchi yote ikaenea watu.
1 Chroniques 1.4-1.28 Genèse 5.32 Genèse 8.17 Genèse 10.2-10.32
20 Nuhu akaanza kuwa mkulima, akapanda mizabibu;
Genèse 5.29 Genèse 3.18-3.19 Genèse 4.2 Deutéronome 28.30 1 Corinthiens 9.7
21 akanywa divai, akalewa; akawa uchi katika hema yake.
Proverbes 20.1 Proverbes 23.31-23.32 Habakuk 2.15-2.16 Galates 5.21 1 Corinthiens 10.12
22 Hamu, baba wa Kanaani, akauona uchi wa baba yake, akawaeleza ndugu zake wawili waliokuwa nje.
Matthieu 18.15 Psaumes 40.15 Psaumes 70.3 1 Corinthiens 13.6 Proverbes 25.9
23 Shemu na Yafethi wakatwaa vazi, wakalitanda mabegani mwao wote wawili, wakaenda kinyumenyume, wakaufunika uchi wa baba yao; na nyuso zao zilielekea nyuma, wala hawakuuona uchi wa baba yao.
1 Timothée 5.19 1 Pierre 4.8 Lévitique 19.32 Romains 13.7 1 Timothée 5.17
24 Nuhu akalevuka katika ulevi wake, akajua mwana wake mdogo alivyomtendea.
25 Akasema,Na alaaniwe Kaanani;Atakuwa mtumwa kabisa kwa ndugu zake.
Josué 9.23 Deutéronome 27.16 Jean 8.34 1 Rois 9.20-9.21 Genèse 4.11
26 Akasema,Na atukuzwe Bwana,Mungu wa Shemu;Na kaanani awe mtumwa wake.
Genèse 10.10-10.26 Romains 9.5 Genèse 27.37 Genèse 27.40 Hébreux 11.16
27 Mungu akamnafisishe Yafethi,Na akae katika hema za Shemu; Na kaanani awe mtumwa wake.
Romains 11.12 Romains 15.12 Malachie 1.11 Ephésiens 2.19 Esaïe 11.10
28 Na Nuhu akaishi baada ya ile gharika miaka mia tatu na hamsini.
29 Siku zote za Nuhu zilikuwa miaka mia kenda na hamsini, akafa.
Genèse 5.5 Genèse 5.27 Genèse 11.11-11.25 Genèse 5.20 Genèse 5.32

Cette Bible est dans le domaine public.