Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Genèse 33
Bible en Swahili de l’est


Réconciliation entre Jacob et Ésaü

1 Yakobo akainua macho yake, akaona, na tazama, Esau anakuja na watu mia nne pamoja naye. Akawagawanyia Lea, na Raheli, na wale vijakazi wawili, wana wao.
Genèse 32.6-32.7 Genèse 32.16 Genèse 27.41-27.42
2 Akawaweka hao vijakazi na wana wao mbele, na Lea na wanawe nyuma yao, na Raheli na Yusufu mwisho.
Malachie 3.17 Genèse 30.22-30.24 Genèse 29.30 Genèse 37.3
3 Akapita mwenyewe mbele yao, akainama mpaka nchi mara saba, hata alipomkaribia ndugu yake.
Genèse 42.6 Genèse 43.26 Genèse 18.2 Ecclésiaste 10.4 Jean 10.11-10.12
4 Esau akaja mbio kumlaki, akamkumbatia, na kumwangukia shingoni, akambusu; nao wakalia.
Genèse 45.14-45.15 Genèse 32.28 Job 2.12 Psaumes 34.4 Genèse 45.2
5 Akainua macho yake, akawaona wale wanawake na watoto, akauliza, Ni nani hawa walio pamoja nawe? Akasema, Ni watoto Mungu aliompa mtumwa wako kwa neema yake.
Psaumes 127.3 Esaïe 8.18 Genèse 48.9 Ruth 4.13 1 Samuel 1.27
6 Ndipo wale vijakazi, na wana wao, wakakaribia wakainama.
7 Lea naye, na wanawe, wakakaribia wakainama. Baadaye Yusufu na Raheli wakakaribia, wakainama.
8 Akasema, Kundi hili lote nililolikuta, maana yake ni nini? Akasema, Kunipatia kibali machoni pa bwana wangu.
Genèse 32.5 Genèse 39.5 Genèse 32.13-32.20 Esther 2.17
9 Esau akasema, Ninayo tele, ndugu yangu, uliyo nayo na yawe yako.
Genèse 27.39 Proverbes 16.7 Philémon 1.16 Philémon 1.7 Genèse 27.41
10 Yakobo akasema, Sivyo; kama nimekubalika machoni pako tafadhali upokee zawadi yangu mkononi mwangu, iwapo nimeona uso wako kama kuona uso wa Mungu, ukapendezwa nami.
Job 33.26 Exode 33.12-33.13 Apocalypse 22.4 2 Samuel 3.13 2 Samuel 14.24
11 Pokea, tafadhali, mbaraka wangu, ulioletewa, kwa sababu Mungu amenineemesha, na kwa sababu ninavyo hivi vyote Akamshurutisha, naye akapokea.
Philippiens 4.18 1 Samuel 25.27 2 Rois 5.23 Genèse 33.9 2 Rois 2.17
12 Kisha Esau akamwambia, Twende zetu, tusafiri, nami nitakutangulia.
13 Akamjibu, Bwana wangu anajua ya kuwa watoto ni wachanga, tena kondoo na ng’ombe nilio nao wanyonyesha. Hao wanyama wakiharakishwa siku moja, watakufa wote.
Esaïe 40.11 Ezéchiel 34.23-34.25 Proverbes 12.10 1 Chroniques 22.5 Ezéchiel 34.15-34.16
14 Tafadhali bwana wangu na apite mbele ya mtumwa wake; nami nitawaongoza polepole kwa kadiri ya mwendo wa wanyama walio mbele yangu, na kwa kadiri ya mwendo wa watoto, hata nitakapofika kwa bwana wangu huko Seiri.
Genèse 32.3 Esaïe 40.11 Marc 4.33 2 Chroniques 20.10 Ezéchiel 25.8
15 Esau akasema, Nikuachie, basi, baadhi ya watu walio pamoja nami. Akasema, Pana haja gani? Na nione kibali tu machoni pa bwana wangu.
Ruth 2.13 Genèse 47.25 Genèse 34.11 1 Samuel 25.8 2 Samuel 16.4
16 Basi Esau akarudi siku ile ile akishika njia yake mpaka Seiri.
17 Yakobo akaendelea mpaka Sukothi. Akajijengea nyumba, akawafanyia makundi yake vibanda. Kwa hiyo jina la mahali pale pakaitwa Sukothi.
Psaumes 60.6 Juges 8.5 Josué 13.27 Juges 8.16 Juges 8.8

La famille de Jacob à Sichem

18 Yakobo akaja kwa amani mpaka mji wa Shekemu, ulio katika nchi ya Kanaani, alipokuja kutoka Padan-aramu; akapiga kambi mbele ya huo mji.
Actes 7.16 Josué 24.1 Juges 9.1 Genèse 25.20 Jean 4.5
19 Akainunua sehemu ya nchi, alipopiga hema yake, kwa mkono wa wana wa Hamori, baba wa Shekemu, kwa vipande mia vya fedha.
Actes 7.16 Josué 24.32 Jean 4.5 Genèse 23.17-23.20 Genèse 34.2-34.31
20 Akajenga huko madhabahu, akaiita, El-elohe-Israeli.
Genèse 13.18 Genèse 12.7-12.8 Genèse 32.28 Genèse 21.33 Genèse 35.7

Cette Bible est dans le domaine public.