Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

1 Samuel 25
Bible en Swahili de l’est


Méchanceté de Nabal

1 Akafa Samweli; nao Israeli wote wakakusanyika, wakamwomboleza, wakamzika nyumbani mwake huko Rama.
1 Samuel 28.3 Nombres 20.29 Deutéronome 34.8 Genèse 21.21 Nombres 10.12
2 Na huko Maoni kulikuwa na mtu mmoja, ambaye alikuwa na mali yake katika Karmeli; naye yule mtu alikuwa mkuu sana, mwenye kondoo elfu tatu na mbuzi elfu; naye alikuwa akiwakata manyoya kondoo zake huko Karmeli.
Josué 15.55 Genèse 38.13 1 Samuel 23.24 2 Samuel 19.32 Psaumes 17.14
3 Na jina la mtu huyo aliitwa Nabali; na jina la mkewe aliitwa Abigaili, na huyo mwanamke alikuwa mwenye akili njema, mzuri wa uso; bali yule mwanamume alikuwa hana adabu, tena mwovu katika matendo yake; naye alikuwa wa mbari ya Kalebu.
1 Samuel 25.10-25.11 Josué 15.13 1 Samuel 25.17 Esaïe 32.5-32.7 1 Samuel 30.14
4 Basi Daudi akasikia huko nyikani ya kuwa Nabali alikuwa katika kuwakata manyoya kondoo zake.
2 Samuel 13.23 Genèse 38.13
5 Daudi akatuma vijana kumi, Daudi naye akawaambia hao vijana, Kweeni mwende Karmeli, na kumwendea huyu Nabali ili mnisalimie;
1 Samuel 17.22 Genèse 43.23
6 na hivi ndivyo mtakavyomwambia huyu aishiye salama, Amani na iwe kwako, na amani nyumbani mwako, na amani kwao wote ulio nao.
Luc 10.5 1 Chroniques 12.18 1 Timothée 5.6 Psaumes 122.7 Matthieu 10.12-10.13
7 Nami sasa nimesikia ya kuwa una watu wanaokata manyoya kondoo zako; haya! Wachungaji wako wamekuwa pamoja nasi, wala hatukuwadhuru, wala hawakukosa kitu wakati wote walipokuwako huko Karmeli.
1 Samuel 25.21 1 Samuel 25.15-25.16 Esaïe 11.6-11.9 Philippiens 4.8 Luc 3.14
8 Waulize vijana wako, nao watakuambia; basi na wakubaliwe vijana hawa machoni pako; maana tumekujia katika siku ya heri; uwape, nakusihi, cho chote kitakachokujia mkononi, uwape watumwa wako na mwanao Daudi.
Esther 9.19 Néhémie 8.10-8.12 Luc 14.12-14.14 Ecclésiaste 11.2 Luc 11.41
9 Basi walipofika vijana wake Daudi, wakamwambia Nabali sawasawa na maneno hayo yote kwa jina la Daudi, kisha wakanyamaza.
Genèse 8.4 2 Chroniques 14.7 2 Rois 2.15
10 Naye Nabali akawajibu wale watumishi wa Daudi, akasema, Huyu Daudi ni nani? Na mwana wa Yese ni nani? Siku hizi kuna watumwa wengi wanaomtoroka kila mtu bwana wake!
Juges 9.28 Exode 5.2 1 Samuel 20.30 1 Samuel 22.7-22.8 Ecclésiaste 7.10
11 Basi mimi je! Nitwae mkate wangu, na maji yangu, na machinjo yangu niliyowachinjia hao watu wangu wakatao manyoya kondoo zangu, na kuwapa watu ambao siwajui wametoka wapi?
Juges 8.6 Jean 9.29-9.30 1 Samuel 24.13 1 Pierre 4.9 Job 31.17
12 Basi vijana wake Daudi wakageuka, wakaenda zao, wakarudi, nao wakaja wakamwambia sawasawa na maneno hayo yote.
Hébreux 13.17 Esaïe 36.21-36.22 2 Samuel 24.13
13 Kisha Daudi akawaambia watu wake, Haya! Jifungeni kila mtu upanga wake. Nao wakajifunga kila mtu upanga wake; Daudi naye akajifunga upanga wake; nao wakapanda nyuma yake Daudi, wapata kama watu mia nne; na watu mia mbili wakakaa na vyombo vyao.
1 Samuel 23.13 Proverbes 14.29 Josué 9.14 Proverbes 16.32 Romains 12.19-12.21
14 Lakini kijana mmojawapo alimpasha habari Abigaili, mkewe Nabali, kasema, Tazama, Daudi alituma wajumbe kutoka nyikani waje ili kumsalimu bwana wetu, naye akawatukana.
Marc 15.29 1 Samuel 13.10
15 Walakini watu hawa walitutendea mema sana, wala hatukupata dhara, wala sisi hatukupotewa na kitu cho chote, wakati wote tulipofuatana nao, tulipokuwako mavueni;
1 Samuel 25.21 1 Samuel 25.7 Philippiens 2.15
16 watu hao walikuwa boma kwetu usiku na mchana, wakati wote tulipokuwa nao tukiwachunga kondoo.
Job 1.10 Exode 14.22 Zacharie 2.5 Jérémie 15.20
17 Basi sasa ujue na kufikiri utakayotenda; kwa sababu yamekusudiwa mabaya juu ya bwana wetu, na juu ya nyumba yake yote; kwa kuwa yeye ni mtu asiyefaa kabisa, hata mtu hawezi kusema naye.
1 Samuel 20.7 Deutéronome 13.13 1 Samuel 2.12 1 Samuel 25.25 2 Chroniques 13.7
18 Ndipo Abigaili akafanya haraka, akatwaa mikate mia mbili, na viriba viwili vya divai, na kondoo watano waliofanyizwa tayari, na vipimo vitano vya bisi, na vishada mia vya zabibu, na mikate ya tini mia mbili; akavipakia vitu hivi juu ya punda.
2 Samuel 16.1 2 Samuel 17.28-17.29 Proverbes 18.16 Nombres 16.46-16.48 Matthieu 5.25
19 Akawaambia vijana wake, Haya! Tangulieni mbele yangu; angalieni, mimi nawafuata. Ila hakumwambia mumewe, Nabali.
Genèse 32.20 Genèse 32.16 Proverbes 31.27 Proverbes 31.11-31.12
20 Ikawa, alipokuwa amepanda punda wake, na kutelemka penye sitara ya mlima, tazama, Daudi na watu wake walikuwa wakishuka kumkabili; naye akawakuta.
2 Rois 4.24
21 Basi Daudi alikuwa amesema, Hakika ni bure nilivyokuwa nikilinda nyikani yote aliyo nayo mtu huyu, asipotewe na kitu cho chote cha mali yake yote; naye amenilipa mabaya badala ya mema.
Proverbes 17.13 Genèse 44.4 Romains 12.21 Ephésiens 4.26 Psaumes 109.3-109.5
22 Mungu naye awafanyie hivyo adui za Daudi, na kuzidi, nikimwachia katika wote walio wake hata mtoto mume mmoja, kutakapopambazuka asubuhi.
1 Samuel 3.17 1 Rois 14.10 1 Samuel 20.13 1 Rois 21.21 Ruth 1.17
23 Ndipo hapo Abigaili alipomwona Daudi, alifanya haraka kushuka juu ya punda wake, akamwangukia Daudi kifulifuli, akainama mpaka nchi.
1 Samuel 20.41 Juges 1.14 Josué 15.18 1 Samuel 24.8
24 Akamwangukia miguuni pake, akasema, Juu yangu, bwana wangu, juu yangu mimi na uwe uovu; tafadhali mjakazi wako na anene masikioni mwako, nawe uyasikilize maneno ya mjakazi wako.
2 Samuel 14.9 Esther 8.3 Philémon 1.18-1.19 1 Samuel 25.28 2 Rois 4.37
25 Nakusihi, bwana wangu, wewe usimwangalie huyu mtu asiyefaa, yaani, Nabali; kwa maana kama lilivyo jina lake ndivyo alivyo yeye; jina lake ndilo Nabali, na upumbavu anao; lakini mimi, mjakazi wako, sikuwaona hao vijana wa bwana wangu aliowatuma.
1 Samuel 25.17 1 Samuel 25.26 Esaïe 42.25 Malachie 2.2 2 Samuel 13.33
26 Basi sasa, bwana wangu, aishivyo Bwana, na iishivyo nafsi yako, kwa kuwa Bwana amekuzuia usimwage damu, tena usijilipize kisasi mkono wako mwenyewe, basi sasa adui zako, na hao wamtakiao bwana wangu mabaya, wawe kama Nabali.
2 Samuel 18.32 Genèse 20.6 Psaumes 44.3 Hébreux 10.30 Psaumes 18.47-18.48
27 Na sasa zawadi hii, mjakazi wako aliyomletea bwana wangu, na wapewe vijana wamfuatao bwana wangu.
Genèse 33.11 1 Samuel 30.26 2 Rois 5.15 2 Corinthiens 9.5 1 Samuel 25.42
28 Nakuomba ulisamehe kosa lake mjakazi wako, kwa kuwa hakika Bwana atamfanyia bwana wangu nyumba iliyo imara, kwa sababu bwana wangu anavipiga vita vya Bwana; tena uovu hautaonekana ndani yako siku zako zote.
1 Samuel 18.17 2 Samuel 7.11 1 Samuel 24.11 1 Chroniques 17.25 1 Rois 9.5
29 Na hata ijapokuwa binadamu angeinuka akuwinde, na kuitafuta nafsi yako, hiyo nafsi ya bwana wangu itafungwa katika furushi ya uhai pamoja na Bwana, Mungu wako; na nafsi za adui zako ndizo atakazozitupa nje, kama kutoka kati ya teo.
Jérémie 10.18 1 Samuel 2.9 Deutéronome 33.29 Psaumes 66.9 1 Pierre 1.5
30 Tena itakuwa, hapo Bwana atakapokuwa amemtendea bwana wangu sawasawa na mema yote aliyoyanena juu yako, na kukutawaza juu ya Israeli;
1 Samuel 13.14 Psaumes 89.20 1 Samuel 23.17 1 Samuel 15.28
31 hili halitakuwa kwazo, wala chukizo la moyoni kwa bwana wangu, ama ya kuwa umemwaga damu bure, ama ya kuwa bwana wangu amejilipiza kisasi mwenyewe; tena hapo Bwana atakapokuwa amemtendea bwana wangu mema, ndipo umkumbuke mjakazi wako.
Genèse 40.14 1 Samuel 24.15 Psaumes 94.1 1 Samuel 26.23 2 Samuel 22.48
32 Naye Daudi akamwambia Abigaili, Na ahimidiwe Bwana, Mungu wa Israeli, ambaye amekuleta hivi leo kunilaki;
Luc 1.68 Exode 18.10 Psaumes 72.18 Genèse 24.27 Esdras 7.27
33 na ibarikiwe busara yako, na ubarikiwe wewe, uliyenizuia hivi leo nisimwage damu, wala kujilipiza kisasi kwa mkono wangu mwenyewe.
1 Samuel 25.26 Proverbes 25.12 Psaumes 141.5 Proverbes 28.23 1 Samuel 25.31
34 Kwa kuwa ni kweli, aishivyo Bwana, Mungu wa Israeli, aliyenizuia nisikudhuru, kwamba hungefanya haraka kuja kunilaki, hakika huyu Nabali asingaliachiwa hata mtoto mume mmoja, kutakapopambazuka asubuhi.
1 Samuel 25.18 1 Samuel 25.26 Josué 10.6 Josué 10.9 1 Samuel 11.11
35 Basi Daudi akapokea mkononi mwake vitu vile alivyomletea; akamwambia, Haya! Kwea kwa amani kwenda nyumbani kwako; tazama, nimeisikiliza sauti yako, nami nimeukubali uso wako.
1 Samuel 20.42 Genèse 19.21 2 Rois 5.19 Job 34.19 Luc 7.50
36 Kisha Abigaili alimjia Nabali; na tazama, alikuwa amefanya karamu nyumbani mwake, kama karamu ya kifalme; na moyo wake huyo Nabali ukafurahiwa ndani yake, kwa maana amelewa kabisa. Kwa sababu hiyo hakumwambia neno, dogo wala kubwa, hata kulipopambazuka.
2 Samuel 13.28 Proverbes 20.1 1 Samuel 25.19 2 Samuel 13.23 Luc 14.12
37 Ikawa asubuhi, divai ilipokuwa imemtoka Nabali, mkewe alimwambia mambo hayo, na moyo wake ukafa ndani yake, akawa kama jiwe.
1 Samuel 25.22 Deutéronome 28.28 Proverbes 23.29-23.35 Job 15.21-15.22 1 Samuel 25.34
38 Tena ikawa, yapata siku kumi baadaye, Bwana alimpiga huyo Nabali, hata akafa.
1 Samuel 26.10 1 Samuel 6.9 1 Samuel 25.33 2 Chroniques 10.15 Actes 12.23
39 Naye aliposikia ya kwamba Nabali amekufa, Daudi alisema, Na ahimidiwe Bwana ambaye amenitetea teto la shutumu langu mkononi mwa Nabali, na kumzuia mtumwa wake asitende maovu; tena uovu wake Nabali Bwana amemrudishia juu ya kichwa chake mwenyewe. Kisha Daudi akatuma watu, akamposa Abigaili ili amwoe.
1 Samuel 25.34 1 Samuel 25.26 1 Rois 2.44 1 Samuel 25.32 Proverbes 22.23
40 Na hao watumishi wa Daudi walipomjia huyo Abigaili huko Karmeli, walimwambia, wakasema, Daudi ametutuma kwako ili tukutwae uwe mkewe.
Genèse 24.51 Genèse 24.37-24.38
41 Naye akainuka na kujiinamisha kifulifuli mpaka nchi, akasema, Tazama, mjakazi wako ni mtumwa wa kuwaosha miguu watumishi wa bwana wangu.
1 Timothée 5.10 Ruth 2.10 Jean 13.3-13.5 Genèse 18.4 Proverbes 18.12
42 Abigaili akafanya haraka, akainuka, akapanda punda, pamoja na vijakazi watano wake waliofuatana naye, akawafuata hao wajumbe wa Daudi, akawa mkewe.
Genèse 24.61-24.67 Psaumes 45.10-45.11
43 Tena Daudi akamwoa Ahinoamu wa Yezreeli; wakawa wote wawili wakeze.
1 Samuel 27.3 1 Samuel 30.5 Josué 15.56 2 Samuel 3.2 Matthieu 19.5
44 Walakini Sauli alikuwa amempa Palti, mwana wa Laishi, aliyekuwa mtu wa Galimu, Mikali binti yake, aliyekuwa mkewe Daudi.
2 Samuel 3.14 1 Samuel 18.27 1 Samuel 18.20 Esaïe 10.30

Cette Bible est dans le domaine public.