Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Apocalypse 22.20
Bible en Swahili de l’est


1 Kisha akanionyesha mto wa maji ya uzima, wenye kung’aa kama bilauri, ukitoka katika kiti cha enzi cha Mungu, na cha Mwana-Kondoo,
Apocalypse 7.17 Zacharie 14.8 Psaumes 46.4 Psaumes 36.8-36.9 Jean 4.14
2 katikati ya njia kuu yake. Na upande huu na upande huu wa ule mto, ulikuwapo mti wa uzima, uzaao matunda, aina kumi na mbili, wenye kutoa matunda yake kila mwezi; na majani ya mti huo ni ya kuwaponya mataifa.
Apocalypse 2.7 Apocalypse 22.14 Genèse 2.9 Proverbes 3.18 Ezéchiel 47.8-47.12
3 Wala hapatakuwa na laana yo yote tena. Na kiti cha enzi cha Mungu na cha Mwana-Kondoo kitakuwamo ndani yake. Na watumwa wake watamtumikia;
Matthieu 25.21 Jean 12.26 Zacharie 14.11 Apocalypse 7.15-7.17 Ezéchiel 37.27
4 nao watamwona uso wake, na jina lake litakuwa katika vipaji vya nyuso zao.
Matthieu 5.8 Apocalypse 14.1 Apocalypse 3.12 1 Jean 3.2-3.3 Job 33.26
5 Wala hapatakuwa na usiku tena; wala hawana haja ya taa wala ya nuru ya jua; kwa kuwa Bwana Mungu huwatia nuru, nao watatawala hata milele na milele.
Daniel 7.18 Daniel 7.27 1 Pierre 1.3-1.4 Apocalypse 20.4 Romains 5.17

Conclusion

6 Kisha akaniambia, Maneno haya ni amini na kweli. Naye Bwana, Mungu wa roho za manabii, alimtuma malaika wake kuwaonyesha watumwa wake mambo ambayo hayana budi kuwako upesi.
Apocalypse 1.1 Apocalypse 21.5 Apocalypse 19.9 Genèse 41.32 1 Pierre 1.11-1.12
7 Na tazama, naja upesi; heri yeye ayashikaye maneno ya unabii wa kitabu hiki.
Apocalypse 3.11 Apocalypse 1.3 Apocalypse 22.12 Apocalypse 22.9-22.10 Apocalypse 22.20
8 Nami Yohana ndimi niliyeyasikia na kuyaona mambo hayo. Na hapo nilipoyasikia na kuyaona nalianguka, ili nisujudu mbele ya miguu ya malaika yule mwenye kunionyesha hayo.
Apocalypse 19.10 Apocalypse 1.1 Apocalypse 19.19
9 Naye akaniambia, Angalia, usifanye hivi; mimi ni mjoli wako, na wa ndugu zako manabii, na wa wale wayashikao maneno ya kitabu hiki. Msujudie Mungu.
Apocalypse 19.10 Colossiens 2.18-2.19 1 Jean 5.20 Apocalypse 9.20 Exode 34.14
10 Akaniambia, Usiyatie muhuri maneno ya unabii wa kitabu hiki, kwa maana wakati huo umekaribia.
Apocalypse 10.4 Apocalypse 1.3 Daniel 8.26 Ezéchiel 12.23 Matthieu 10.27
11 Mwenye kudhulumu na azidi kudhulumu; na mwenye uchafu na azidi kuwa mchafu; na mwenye haki na azidi kufanya haki; na mtakatifu na azidi kutakaswa.
Daniel 12.10 Ezéchiel 3.27 Proverbes 4.18 2 Timothée 3.13 Matthieu 5.6
12 Tazama, naja upesi, na ujira wangu u pamoja nami, kumlipa kila mtu kama kazi yake ilivyo.
Matthieu 16.27 Esaïe 62.11 Esaïe 40.10 Apocalypse 22.7 1 Corinthiens 3.8
13 Mimi ni Alfa na Omega, mwanzo na mwisho, wa kwanza na wa mwisho.
Apocalypse 21.6 Apocalypse 1.8 Apocalypse 1.17 Esaïe 44.6 Esaïe 48.12
14 Heri wazifuao nguo zao, wawe na amri kuuendea huo mti wa uzima, na kuingia mjini kwa milango yake.
Apocalypse 21.27 Apocalypse 2.7 Apocalypse 22.2 Psaumes 119.1-119.6 1 Jean 5.3
15 Huko nje wako mbwa, na wachawi, na wazinzi, na wauaji, na hao waabuduo sanamu, na kila mtu apendaye uongo na kuufanya.
Apocalypse 21.8 Galates 5.19-5.21 Philippiens 3.2 Apocalypse 21.27 Colossiens 3.6
16 Mimi Yesu nimemtuma malaika wangu kuwashuhudia ninyi mambo hayo katika makanisa. Mimi ndimi niliye Shina na Mzao wa Daudi, ile nyota yenye kung’aa ya asubuhi.
Apocalypse 5.5 Apocalypse 1.4 Apocalypse 1.1 Nombres 24.17 2 Pierre 1.19
17 Na Roho na Bibi-arusi wasema, Njoo! Naye asikiaye na aseme, Njoo! Naye mwenye kiu na aje; na yeye atakaye, na ayatwae maji ya uzima bure.
Jean 4.14 Apocalypse 21.6 Esaïe 55.1-55.3 Apocalypse 21.2 Apocalypse 21.9
18 Namshuhudia kila mtu ayasikiaye maneno ya unabii wa kitabu hiki, Mtu ye yote akiyaongeza, Mungu atamwongezea hayo mapigo yaliyoandikwa katika kitabu hiki.
Deutéronome 4.2 Proverbes 30.6 Deutéronome 12.32 Ephésiens 4.17 Apocalypse 22.16
19 Na mtu ye yote akiondoa lo lote katika maneno ya unabii wa kitabu hiki, Mungu atamwondolea sehemu yake katika ule mti wa uzima, na katika ule mji mtakatifu, ambao habari zake zimeandikwa katika kitabu hiki.
Apocalypse 22.2 Psaumes 69.28 Apocalypse 21.22-21.27 Deutéronome 4.2 Apocalypse 13.8
20 Yeye mwenye kuyashuhudia haya asema, Naam; naja upesi. Amina; na uje, Bwana Yesu.
Apocalypse 22.7 2 Timothée 4.8 Apocalypse 22.12 1 Corinthiens 16.22 Apocalypse 22.10
21 Neema ya Bwana Yesu na iwe pamoja nanyi nyote. Amina.
2 Thessaloniciens 3.18 Romains 16.20 2 Corinthiens 13.14 Ephésiens 6.23-6.24

Cette Bible est dans le domaine public.