Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Apocalypse 19.6
Bible en Swahili de l’est


Les noces de l’Agneau

Louanges et festin de noces

1 Baada ya hayo nikasikia sauti kama sauti ya makutano mengi, sauti kubwa mbinguni, ikisema, Haleluya; wokovu na utukufu na nguvu zina BWANA MUNGU wetu.
Apocalypse 11.15 1 Chroniques 29.11 Apocalypse 7.10-7.12 Apocalypse 19.6 Apocalypse 19.3-19.4
2 kwa kuwa hukumu zake ni za kweli na za haki; maana amemhukumu yule kahaba mkuu aliyeiharibu nchi kwa uasherati wake, na kuipatiliza damu ya watumwa wake mkononi mwake.
Deutéronome 32.43 Apocalypse 6.10 Psaumes 19.9 Apocalypse 15.3 Apocalypse 18.20
3 Wakasema mara ya pili, Haleluya. Na moshi wake hupaa juu hata milele na milele.
Esaïe 34.10 Apocalypse 14.11 Apocalypse 18.9 Genèse 19.28 Apocalypse 18.18
4 Na wale wazee ishirini na wanne, na wale wenye uhai wanne, wakasujudu na kumwabudu Mungu, aketiye katika kile kiti cha enzi, wakisema, Amina, Haleluya.
Apocalypse 5.14 Psaumes 106.48 Apocalypse 4.4-4.10 Néhémie 8.6 Apocalypse 15.7
5 Sauti ikatoka katika kile kiti cha enzi ikisema, Msifuni Mungu wetu, enyi watumwa wake wote, ninyi mnaomcha, wadogo kwa wakuu.
Psaumes 135.1 Psaumes 134.1 Psaumes 148.11-148.13 Psaumes 135.19-135.20 Apocalypse 11.18-11.19
6 Nikasikia sauti kama sauti ya makutano mengi, na kama sauti ya maji mengi, na kama sauti ya radi yenye nguvu, ikisema, Haleluya; kwa kuwa Bwana Mungu wetu, Mwenyezi, amemiliki.
Apocalypse 14.2 Apocalypse 6.1 Apocalypse 1.15 Psaumes 99.1 Psaumes 97.1
7 Na tufurahi, tukashangilie, tukampe utukufu wake; kwa kuwa arusi ya Mwana-Kondoo imekuja, na mkewe amejiweka tayari.
Apocalypse 21.9 Apocalypse 21.2 Matthieu 22.2 Ephésiens 5.32 Jean 3.29
8 Naye amepewa kuvikwa kitani nzuri, ing’arayo, safi; kwa maana kitani nzuri hiyo ni matendo ya haki ya watakatifu.
Esaïe 61.10 Ezéchiel 16.10 Ephésiens 5.26-5.27 Marc 9.3 Luc 24.4
9 Naye akaniambia, Andika, Heri walioalikwa karamu ya arusi ya Mwana-Kondoo. Akaniambia, Maneno haya ni maneno ya kweli ya Mungu.
Apocalypse 22.6 Apocalypse 21.5 Apocalypse 1.19 Apocalypse 19.7-19.8 1 Timothée 4.9
10 Nami nikaanguka mbele ya miguu yake, ili nimsujudie; akaniambia, Angalia, usifanye hivi; mimi ni mjoli wako na wa ndugu zako walio na ushuhuda wa Yesu. Msujudie Mungu. Kwa maana ushuhuda wa Yesu ndio roho ya unabii.
Apocalypse 22.8-22.9 Actes 10.25-10.26 Apocalypse 12.17 Apocalypse 4.10 Jean 5.39

Victoire sur la bête et le prétendu prophète

11 Kisha nikaziona mbingu zimefunuka, na tazama, farasi mweupe, na yeye aliyempanda, aitwaye Mwaminifu na Wa-kweli, naye kwa haki ahukumu na kufanya vita.
Psaumes 96.13 Apocalypse 6.2 Apocalypse 3.14 Esaïe 11.3-11.5 Psaumes 98.9
12 Na macho yake yalikuwa kama mwali wa moto, na juu ya kichwa chake vilemba vingi; naye ana jina lililoandikwa, asilolijua mtu ila yeye mwenyewe.
Apocalypse 19.16 Apocalypse 1.14 Apocalypse 2.17-2.18 Luc 10.22 Apocalypse 3.12
13 Naye amevikwa vazi lililochovywa katika damu, na jina lake aitwa, Neno la Mungu.
Jean 1.1 Jean 1.14 1 Jean 1.1 Psaumes 58.10 Esaïe 63.1-63.6
14 Na majeshi yaliyo mbinguni wakamfuata, wamepanda farasi weupe na kuvikwa kitani nzuri, nyeupe, safi.
Jude 1.14 Apocalypse 19.8 Apocalypse 7.9 Apocalypse 17.14 Apocalypse 14.20
15 Na upanga mkali hutoka kinywani mwake ili awapige mataifa kwa huo. Naye atawachunga kwa fimbo ya chuma, naye anakanyaga shinikizo la mvinyo ya ghadhabu ya hasira ya Mungu Mwenyezi.
Psaumes 2.9 2 Thessaloniciens 2.8 Apocalypse 2.27 Apocalypse 1.16 Esaïe 11.4
16 Naye ana jina limeandikwa katika vazi lake na paja lake, MFALME WA WAFALME, NA Bwana WA MABwana.
Apocalypse 17.14 1 Timothée 6.15 Apocalypse 19.12-19.13 Psaumes 72.11 Apocalypse 2.17
17 Kisha nikaona malaika mmoja amesimama katika jua; akalia kwa sauti kuu, akiwaambia ndege wote warukao katikati ya mbingu, Njoni mkutane kwa karamu ya Mungu iliyo kuu;
Apocalypse 19.21 Apocalypse 8.13 Jérémie 12.9 Ezéchiel 39.17-39.20 Esaïe 56.9
18 mpate kula nyama ya wafalme, na nyama ya majemadari, na nyama ya watu hodari, na nyama ya farasi na ya watu wawapandao, na nyama ya watu wote, waungwana kwa watumwa, wadogo kwa wakubwa.
Apocalypse 13.16 Ezéchiel 39.18-39.20 Jérémie 16.4 1 Samuel 17.46 Deutéronome 28.26
19 Kisha nikamwona huyo mnyama, na wafalme wa nchi, na majeshi yao, wamekutana kufanya vita na yeye aketiye juu ya farasi yule, tena na majeshi yake.
Apocalypse 16.16 Apocalypse 16.14 Apocalypse 13.1-13.10 Apocalypse 18.9 Apocalypse 17.12-17.14
20 Yule mnyama akakamatwa, na yule nabii wa uongo pamoja naye, yeye aliyezifanya hizo ishara mbele yake, ambazo kwa hizo aliwadanganya watu wale walioipokea ile chapa ya huyo mnyama, nao walioisujudia sanamu yake; hao wawili wakatupwa wangali hai katika lile ziwa la moto liwakalo kwa kiberiti;
Apocalypse 20.10 Apocalypse 21.8 Apocalypse 20.14-20.15 Apocalypse 14.10 Esaïe 30.33
21 na wale waliosalia waliuawa kwa upanga wake yeye aliyeketi juu ya yule farasi, upanga utokao katika kinywa chake. Na ndege wote wakashiba kwa nyama zao.
Apocalypse 17.16 Apocalypse 19.11-19.15 Apocalypse 1.16 Apocalypse 19.17-19.19

Cette Bible est dans le domaine public.