Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

1 Jean 5.2
Bible en Swahili de l’est


La foi en Christ et ses effets

1 Kila mtu aaminiye kwamba Yesu ni Kristo amezaliwa na Mungu. Na kila mtu ampendaye mwenye kuzaa, ampenda hata yeye aliyezaliwa na yeye.
Jean 8.42 Jean 1.12-1.13 1 Jean 2.22-2.23 1 Jean 5.4 1 Jean 2.29
2 Katika hili twajua kwamba twawapenda watoto wa Mungu, tumpendapo Mungu, na kuzishika amri zake.
1 Jean 2.5 1 Jean 3.22-3.24 Jean 13.34-13.35 1 Jean 4.21 Jean 15.17
3 Kwa maana huku ndiko kumpenda Mungu, kwamba tuzishike amri zake; wala amri zake si nzito.
Jean 14.15 2 Jean 1.6 Jean 14.21-14.24 Jean 15.10 1 Jean 2.3
4 Kwa maana kila kitu kilichozaliwa na Mungu huushinda ulimwengu; na huku ndiko kushinda kuushindako ulimwengu, hiyo imani yetu.
1 Corinthiens 15.57 1 Jean 4.4 Apocalypse 12.11 1 Jean 3.9 Romains 8.35-8.37
5 Mwenye kuushinda ulimwengu ni nani, isipokuwa ni yeye aaminiye ya kwamba Yesu ni Mwana wa Mungu?
1 Jean 4.15 1 Jean 5.1
6 Huyu ndiye aliyekuja kwa maji na damu, Yesu Kristo; si katika maji tu, bali katika maji na katika damu. Naye Roho ndiye ashuhudiaye, kwa sababu Roho ndiye kweli.
Jean 15.26 Jean 16.13 Jean 14.17 Apocalypse 7.14 Ephésiens 5.25-5.27
7 Kwa maana wako watatu washuhudiao [mbinguni, Baba, na Neno, na Roho Mtakatifu, na watatu hawa ni umoja.
Matthieu 28.19 2 Corinthiens 13.14 1 Jean 1.1 Apocalypse 19.13 Apocalypse 1.4-1.5
8 Kisha wako watatu washuhudiao duniani], Roho, na maji, na damu; na watatu hawa hupatana kwa habari moja.
1 Pierre 3.21 Matthieu 26.26-26.28 Actes 2.2-2.4 Jean 15.26 Hébreux 13.12
9 Tukiupokea ushuhuda wa wanadamu, ushuhuda wa Mungu ni mkuu zaidi; kwa maana ushuhuda wa Mungu ndio huu, kwamba amemshuhudia Mwanawe.
Matthieu 3.16-3.17 Jean 10.38 Actes 17.31 Jean 5.39 Jean 8.17-8.19
10 Yeye amwaminiye Mwana wa Mungu anao huo ushuhuda ndani yake. Asiyemwamini Mungu amemfanya kuwa mwongo, kwa kuwa hakuuamini huo ushuhuda ambao Mungu amemshuhudia Mwanawe.
Romains 8.16 Jean 3.33 Galates 4.6 1 Jean 1.10 Jean 5.38
11 Na huu ndio ushuhuda, ya kwamba Mungu alitupa uzima wa milele; na uzima huu umo katika Mwanawe.
1 Jean 2.25 Jean 1.4 1 Jean 4.9 Jean 3.36 1 Jean 5.20
12 Yeye aliye naye Mwana, anao huo uzima; asiye naye Mwana wa Mungu hana huo uzima.
Jean 3.36 Jean 5.24 Jean 1.12 Jean 3.15 Galates 2.20
13 Nimewaandikia ninyi mambo hayo, ili mjue ya kuwa mna uzima wa milele, ninyi mnaoliamini Jina la Mwana wa Mungu.
Jean 20.31 Jean 1.12 1 Jean 3.23 Galates 4.6 Romains 8.15-8.17
14 Na huu ndio ujasiri tulio nao kwake, ya kuwa, tukiomba kitu sawasawa na mapenzi yake, atusikia.
1 Jean 3.21-3.22 Jean 14.13 Jean 16.24 Jacques 4.3 Ephésiens 3.12
15 Na kama tukijua kwamba atusikia, tuombacho chote, twajua kwamba tunazo zile haja tulizomwomba.
Marc 11.24 Proverbes 15.29 Luc 11.9-11.10 Jérémie 15.12-15.13
16 Mtu akimwona ndugu yake anatenda dhambi isiyo ya mauti, ataomba, na Mungu atampa uzima kwa ajili ya hao watendao dhambi isiyo ya mauti. Iko dhambi iliyo ya mauti. Sisemi ya kwamba ataomba kwa ajili ya hiyo.
Hébreux 6.4-6.6 1 Samuel 2.25 Jérémie 7.16 Jérémie 11.14 Nombres 15.30
17 Kila lisilo la haki ni dhambi, na dhambi iko isiyo ya mauti.
1 Jean 3.4 Jacques 1.15 1 Jean 5.16 Ezéchiel 18.26-18.32 Deutéronome 12.32
18 Twajua ya kuwa kila mtu aliyezaliwa na Mungu hatendi dhambi; bali yeye aliyezaliwa na Mungu hujilinda, wala yule mwovu hamgusi.
Jude 1.21 1 Jean 3.9 Jacques 1.27 Psaumes 18.23 1 Jean 4.6
19 Twajua ya kuwa sisi tu wa Mungu; na dunia yote pia hukaa katika yule mwovu.
Galates 1.4 Apocalypse 12.9 1 Jean 4.4-4.6 2 Corinthiens 4.4 Jean 16.11
20 Nasi twajua kwamba Mwana wa Mungu amekwisha kuja, naye ametupa akili kwamba tumjue yeye aliye wa kweli, nasi tumo ndani yake yeye aliye wa kweli, yaani, ndani ya Mwana wake Yesu Kristo. Huyu ndiye Mungu wa kweli, na uzima wa milele.
Jean 17.3 Luc 24.45 Jean 14.9 Apocalypse 3.7 Romains 9.5
21 Watoto wadogo, jilindeni nafsi zenu na sanamu.
1 Corinthiens 10.14 1 Corinthiens 10.7 1 Jean 2.1 1 Thessaloniciens 1.9 Apocalypse 14.11

Cette Bible est dans le domaine public.