Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

2 Pierre 3.14
Bible en Swahili de l’est


Le retour du Seigneur

1 Wapenzi, waraka huu ndio wa pili niwaandikiao ninyi; katika zote mbili naziamsha nia zenu safi kwa kuwakumbusha,
2 Timothée 1.6 2 Pierre 1.12-1.15 1 Pierre 1.1-1.2 1 Timothée 5.22 1 Pierre 1.22
2 mpate kuyakumbuka yale maneno yaliyonenwa zamani na manabii watakatifu, na ile amri ya Bwana na Mwokozi iliyoletwa na mitume wenu.
Jude 1.17 Luc 1.70 Apocalypse 19.10 2 Pierre 2.21 Actes 3.18
3 Mkijua kwanza neno hili ya kwamba katika siku za mwisho watakuja na dhihaka zao watu wenye kudhihaki, wafuatao tamaa zao wenyewe,
Jude 1.18 2 Pierre 2.10 1 Timothée 4.1-4.2 Jude 1.16 2 Pierre 1.20
4 na kusema, Iko wapi ahadi ile ya kuja kwake? Kwa maana, tangu hapo babu zetu walipolala, vitu vyote vinakaa hali iyo hiyo, tangu mwanzo wa kuumbwa.
Malachie 2.17 Jérémie 17.15 Ecclésiaste 8.11 Matthieu 24.48 Ecclésiaste 1.9
5 Maana hufumba macho yao wasione neno hili ya kuwa zilikuwako mbingu tangu zamani, na nchi pia, imefanyizwa kutoka katika maji, na ndani ya maji, kwa neno la Mungu;
Psaumes 24.2 Hébreux 11.3 Genèse 1.6 Genèse 1.9 Psaumes 136.6
6 kwa hayo dunia ile ya wakati ule iligharikishwa na maji, ikaangamia.
2 Pierre 2.5 Genèse 7.10-7.23 Job 12.15 Matthieu 24.38-24.39 Luc 17.27
7 Lakini mbingu za sasa na nchi zimewekwa akiba kwa moto, kwa neno lilo hilo, zikilindwa hata siku ya hukumu, na ya kuangamia kwao wanadamu wasiomcha Mungu.
2 Pierre 3.10 2 Pierre 3.12 Matthieu 24.35 Apocalypse 21.1 2 Thessaloniciens 1.7-1.8
8 Lakini, wapenzi, msilisahau neno hili, kwamba kwa Bwana siku moja ni kama miaka elfu, na miaka elfu ni kama siku moja.
Psaumes 90.4 Romains 11.25
9 Bwana hakawii kuitimiza ahadi yake, kama wengine wanavyokudhani kukawia, bali huvumilia kwenu, maana hapendi mtu ye yote apotee, bali wote wafikilie toba.
1 Timothée 2.4 Habakuk 2.3 Esaïe 30.18 Romains 2.4 Hébreux 10.37
10 Lakini siku ya Bwana itakuja kama mwivi; katika siku hiyo mbingu zitatoweka kwa mshindo mkuu, na viumbe vya asili vitaunguzwa, na kufumuliwa, na nchi na kazi zilizomo ndani yake zitateketea.
Matthieu 24.35 Apocalypse 21.1 1 Thessaloniciens 5.2 2 Pierre 3.7 Apocalypse 16.15
11 Basi, kwa kuwa vitu hivi vyote vitafumuliwa hivyo, imewapasa ninyi kuwa watu wa tabia gani katika mwenendo mtakatifu na utauwa,
1 Pierre 1.15 2 Pierre 3.12 Jacques 3.13 Jacques 1.24 Esaïe 14.31
12 mkitazamia hata ije siku ile ya Mungu, na kuihimiza; ambayo katika hiyo mbingu zitafumuliwa zikiungua, na viumbe vya asili vitateketea na kuyeyuka?
2 Pierre 3.10 Michée 1.4 Tite 2.13 Psaumes 50.3 Esaïe 34.4
13 Lakini, kama ilivyo ahadi yake, mnatazamia mbingu mpya na nchi mpya, ambayo haki yakaa ndani yake.
Esaïe 65.17 Apocalypse 21.1 Esaïe 66.22 Apocalypse 21.27 Esaïe 60.21
14 Kwa hiyo, wapenzi, kwa kuwa mnatazamia mambo hayo, fanyeni bidii ili mwonekane katika amani kuwa hamna mawaa wala aibu mbele yake.
1 Corinthiens 15.58 1 Thessaloniciens 3.13 1 Thessaloniciens 5.23 Philippiens 1.10 1 Jean 3.3
15 Nanyi uhesabuni uvumilivu wa Bwana wetu kuwa ni wokovu, kama vile na ndugu yetu mpenzi Paulo alivyowaandikia kwa hekima aliyopewa;
2 Pierre 3.9 Actes 15.25 1 Timothée 1.16 Romains 2.4 Proverbes 2.6-2.7
16 vile vile kama katika nyaraka zake zote pia, akitoa humo habari za mambo hayo; katika nyaraka hizo yamo mambo ambayo ni vigumu kuelewa nayo; na mambo hayo watu wasio na elimu, wasio imara, huyapotoa, kama vile wayapotoavyo na maandiko mengine, kwa uvunjifu wao wenyewe.
2 Pierre 2.14 Matthieu 15.6 Hébreux 5.11 Jérémie 23.36 Habakuk 1.4
17 Basi, wapenzi mkitangulia kujua hayo, jilindeni nafsi zenu, msije mkachukuliwa na kosa la hao wahalifu mkaanguka na kuuacha uthibitifu wenu.
Hébreux 3.14 Matthieu 7.15 2 Pierre 2.18-2.22 1 Corinthiens 10.12 2 Corinthiens 11.13-11.15
18 Lakini, kueni katika neema, na katika kumjua Bwana wetu na Mwokozi Yesu Kristo. Utukufu una yeye sasa na hata milele.
Colossiens 1.10 Ephésiens 4.15 1 Pierre 2.2 1 Pierre 5.10-5.11 2 Pierre 1.3

Cette Bible est dans le domaine public.