Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Josué 4.4
Bible en Swahili de l’est


Deux monuments de pierres

1 Ikawa, hapo hilo taifa zima lilipokuwa limekwisha vuka Yordani, ndipo Bwana akanena na Yoshua, akamwambia,
Josué 3.17 Deutéronome 27.2
2 Haya, twaeni watu waume kumi na wawili katika hao watu, kila kabila mtu mmoja,
Josué 3.12 Nombres 34.18 1 Rois 18.31 Nombres 1.4-1.15 Matthieu 10.1-10.5
3 kisha uwaamrishe, kusema, Twaeni mawe kumi na mawili, hapo katikati ya Yordani, mahali hapo miguu ya hao makuhani iliposimama imara, mwende nayo mawe hayo, mkayaweke nchi kambini, hapo mtakapolala usiku huu.
Josué 4.19-4.20 Josué 4.8 Josué 3.13 Deutéronome 27.1-27.26 Genèse 28.22
4 Basi Yoshua akawaita hao watu kumi na wawili, aliokuwa amewaweka tayari tangu hapo, katika wana wa Israeli, kila kabila mtu mmoja;
Marc 3.14-3.19 Josué 4.2
5 naye Yoshua akawaambia, Haya, piteni ninyi mtangulie mbele ya sanduku la Bwana, Mungu wenu, mwende pale katikati ya Yordani, mkatwae kila mtu wenu jiwe moja begani mwake, kwa kadiri ya hesabu ya kabila za wana wa Israeli;
6 ili kwamba jambo hili liwe ishara kati yenu, hapo watoto wenu watakapowauliza ninyi katika siku zijazo, wakisema, Ni nini maana yake mawe haya?
Exode 13.14 Josué 4.21 Esaïe 55.13 Deutéronome 11.19 Exode 13.9
7 Ndipo mtakapowaambia, Ni kwa sababu maji ya Yordani yalitindika mbele ya sanduku la agano la Bwana; hapo lilipovuka Yordani, hayo maji ya Yordani yalitindika; na mawe haya yatakuwa ni ukumbusho kwa wana wa Israeli milele.
Exode 12.14 Nombres 16.40 Josué 4.6 Exode 30.16 Exode 28.12
8 Basi wana wa Israeli walifanya vile vile kama Yoshua alivyowaamuru, nao wakatwaa mawe kumi na mawili pale katikati ya Yordani, kama Bwana alivyomwambia Yoshua, sawasawa na hesabu ya kabila za wana wa Israeli; wakayachukua wakavuka nayo hata mahali pale walipolala, nao wakayaweka nchi kuko huko.
Josué 1.16-1.18 Josué 4.20 Josué 4.2-4.5
9 Kisha Yoshua akapanga mawe kumi na mawili katikati ya Yordani, mahali pale miguu ya hao makuhani waliolichukua hilo sanduku la agano iliposimama; nayo yapo pale pale hata hivi leo.
1 Samuel 7.12 Deutéronome 34.6 Genèse 28.18 1 Samuel 30.25 2 Samuel 4.3
10 Kwa kuwa makuhani waliolichukua hilo sanduku walisimama katikati ya Yordani, hata mambo yote Bwana aliyomwamuru Yoshua awambie hao watu yakaisha, sawasawa na hayo yote Musa aliyokuwa amemwamuru Yoshua; kisha hao watu wakafanya haraka wakavuka.
Josué 3.13 Josué 3.16-3.17 Exode 12.39 Ecclésiaste 9.10 Psaumes 119.60
11 Ikawa watu wote walipokuwa wamekwisha vuka kabisa, hilo sanduku la Bwana likavuka, na hao makuhani, mbele ya macho ya hao watu.
Josué 3.8 Josué 3.17 Josué 4.18
12 Na wana wa Reubeni, na wana wa Gadi na hiyo nusu ya kabila ya Manase, wakavuka, hali ya kuvaa silaha mbele ya wana wa Israeli, kama Musa alivyowaambia;
Josué 1.14 Nombres 32.20-32.32
13 walipata kama watu arobaini elfu hesabu yao, wenye kuvaa silaha tayari kwa vita, waliovuka mbele ya Bwana, waende vitani, hata nchi tambarare za Yeriko.
Jérémie 39.5 2 Rois 25.5 Jérémie 52.8 Ephésiens 6.11 Josué 5.10
14 Siku ile Bwana alimtukuza Yoshua mbele ya macho ya Israeli wote; nao wakamcha, kama walivyokuwa wakimcha Musa, siku zote za maisha yake.
Josué 3.7 Josué 1.16-1.18 Romains 13.4 1 Rois 3.28 2 Chroniques 30.12
15 Kisha Bwana akanena na Yoshua, akamwambia,
16 Haya, uwaamuru makuhani, hao waliolichukua sanduku la ushuhuda, kwamba wakwee juu kutoka mle katika Yordani.
Josué 3.3-3.6 Exode 25.16-25.22 Apocalypse 11.19
17 Basi Yoshua akawaamuru hao makuhani, akawaambia, Haya, kweeni mtoke Yordani.
Genèse 8.16-8.18 Daniel 3.26 Actes 16.23 Actes 16.35-16.39
18 Ilikuwa, hapo hao makuhani waliolichukua sanduku la agano la Bwana walipokwea juu kutoka mle kati ya Yordani, na nyayo za miguu yao hao makuhani zilipoinuliwa na kutiwa katika nchi kavu, ndipo maji ya Yordani yaliporudi mahali pake, na kujaa na kuipita mipaka yake, kama yalivyokuwa hapo kwanza.
Josué 3.15 Esaïe 8.8 Josué 3.13 Exode 14.26-14.28 1 Chroniques 12.15
19 Na hao watu wakakwea kutoka Yordani siku ya kumi ya mwezi wa kwanza, wakapiga kambi Gilgali, katika mpaka wa mashariki wa Yeriko.
Josué 5.9 Michée 6.5 1 Samuel 11.14-11.15 1 Samuel 15.33 Exode 12.2-12.3
20 Na yale mawe kumi na mawili waliyoyatwaa katikati ya Yordani Yoshua akayasimamisha Gilgali.
Josué 4.3 Josué 4.8
21 Akawaambia wana wa Israeli, akasema, Watoto wenu watakapowauliza baba zao katika siku zijazo, wakisema, Mawe haya maana yake ni nini?
Josué 4.6 Psaumes 105.2-105.5 Psaumes 145.4-145.7
22 Ndipo mtakapowaarifu watoto wenu mkisema, Israeli walivuka mto huu wa Yordani, kwa njia ya nchi kavu.
Josué 3.17 Psaumes 66.5-66.6 Exode 14.29 Apocalypse 16.12 Esaïe 44.27
23 Kwa sababu Bwana, Mungu wenu aliyakausha maji ya Yordani, mbele yenu, hata mlipokwisha kuvuka kama Bwana, Mungu wenu, alivyoitenda Bahari ya Shamu, aliyoikausha mbele yetu hata tulipokwisha kuvuka;
Exode 14.21 Esaïe 63.12-63.14 Néhémie 9.11 Psaumes 77.16-77.19 Psaumes 78.13
24 watu wote wa duniani wapate kujua mkono wa Bwana, ya kuwa ni mkono wenye uweza, ili wamche Bwana, Mungu wenu, milele.
Psaumes 89.13 Exode 14.31 1 Rois 8.42-8.43 2 Rois 19.19 1 Chroniques 29.12

Cette Bible est dans le domaine public.