Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Hébreux 6.13
Bible en Swahili de l’est


1 Kwa sababu hiyo, tukiacha kuyanena mafundisho ya kwanza ya Kristo, tukaze mwendo ili tuufikilie utimilifu; tusiweke msingi tena wa kuzitubia kazi zisizo na uhai, na wa kuwa na imani kwa Mungu,
Hébreux 5.12-5.14 Hébreux 9.14 Ezéchiel 18.30-18.32 2 Corinthiens 7.10 1 Corinthiens 3.10-3.12
2 na wa mafundisho ya mabatizo, na kuwekea mikono, na kufufuliwa wafu, na hukumu ya milele.
Actes 6.6 Actes 17.31-17.32 Actes 17.18 Jude 1.14-1.15 Actes 8.12-8.18
3 Na hayo tutafanya Mungu akitujalia.
Actes 18.21 1 Corinthiens 16.7 1 Corinthiens 4.19 Jacques 4.15 Romains 15.32
4 Kwa maana hao waliokwisha kupewa nuru, na kukionja kipawa cha mbinguni, na kufanywa washirika wa Roho Mtakatifu,
2 Pierre 2.20-2.22 Hébreux 10.26-10.29 Hébreux 10.32 Galates 3.2 Ephésiens 2.8
5 na kulionja neno zuri la Mungu, na nguvu za zamani zijazo,
Hébreux 2.5 2 Pierre 2.20 1 Pierre 2.3 Matthieu 13.20-13.21 Marc 6.20
6 wakaanguka baada ya hayo, haiwezekani kuwafanya upya tena hata wakatubu; kwa kuwa wamsulibisha Mwana wa Mungu mara ya pili kwa nafsi zao, na kumfedhehi kwa dhahiri.
Hébreux 10.29 Esaïe 1.28 2 Pierre 2.21 Hébreux 6.4 1 Jean 5.16
7 Maana nchi inayoinywa mvua inayoinyeshea mara kwa mara, na kuzaa mboga zenye manufaa kwa hao ambao kwa ajili yao yalimwa, hushiriki baraka zitokazo kwa Mungu;
Ezéchiel 34.26 Genèse 27.27 Joël 2.21-2.26 Jacques 5.7 Esaïe 55.10-55.13
8 bali ikitoa miiba na magugu hukataliwa na kuwa karibu na laana; ambayo mwisho wake ni kuteketezwa.
Genèse 3.17-3.18 Esaïe 5.1-5.7 Luc 13.7-13.9 Jérémie 44.22 Jean 15.6
9 Lakini, wapenzi, ijapokuwa twanena hayo, katika habari zenu tumesadiki mambo yaliyo mazuri zaidi, na yaliyo na wokovu.
Hébreux 6.4-6.6 Galates 5.22-5.23 1 Corinthiens 10.14 Hébreux 2.3 Hébreux 10.34
10 Maana Mungu si dhalimu hata aisahau kazi yenu, na pendo lile mlilolidhihirisha kwa jina lake, kwa kuwa mmewahudumia watakatifu, na hata hivi sasa mngali mkiwahudumia.
Matthieu 10.42 Proverbes 14.31 1 Thessaloniciens 1.3 Actes 10.4 Matthieu 25.35-25.40
11 Nasi twataka sana kila mmoja wenu aidhihirishe bidii ile ile, kwa utimilifu wa matumaini hata mwisho;
Hébreux 3.6 Hébreux 3.14 1 Corinthiens 15.58 Hébreux 10.22 Romains 5.2-5.5
12 ili msiwe wavivu, bali mkawe wafuasi wa hao wazirithio ahadi kwa imani na uvumilivu.
Hébreux 13.7 Hébreux 10.36 Proverbes 24.30-24.34 1 Jean 2.25 Hébreux 5.11
13 Kwa maana Mungu, alipompa Ibrahimu ahadi, kwa sababu alikuwa hana mkubwa kuliko yeye mwenyewe wa kumwapa, aliapa kwa nafsi yake,
Luc 1.73 Genèse 22.15-22.18 Ezéchiel 32.13 Psaumes 105.9-105.10 Michée 7.20
14 akisema, Hakika yangu kubariki nitakubariki, na kuongeza nitakuongeza.
Genèse 22.17 Genèse 48.4 Exode 32.13 Néhémie 9.23 Genèse 17.2
15 Na hivyo kwa kuvumilia akaipata ile ahadi.
Hébreux 6.12 Genèse 21.2-21.7 Genèse 12.2-12.3 Habakuk 2.2-2.3 Exode 1.7
16 Maana wanadamu huapa kwa yeye aliye mkuu kuliko wao; na kwao ukomo wa mashindano yote ya maneno ni kiapo, kwa kuyathibitisha.
Exode 22.11 Genèse 21.23 Matthieu 23.20-23.22 2 Samuel 21.2 Josué 9.15-9.20
17 Katika neno hilo Mungu, akitaka kuwaonyesha zaidi sana warithio ile ahadi, jinsi mashauri yake yasivyoweza kubadilika, alitia kiapo katikati;
Hébreux 11.9 Hébreux 6.18 Proverbes 19.21 Psaumes 110.4 Genèse 26.28
18 ili kwa vitu viwili visivyoweza kubadilika, ambavyo katika hivyo Mungu hawezi kusema uongo, tupate faraja iliyo imara, sisi tuliokimbilia kuyashika matumaini yale yawekwayo mbele yetu;
Tite 1.2 Nombres 23.19 Esaïe 27.5 1 Samuel 15.29 Zacharie 9.12
19 tuliyo nayo kama nanga ya roho, yenye salama, yenye nguvu, yaingiayo hata mle mlimo ndani ya pazia,
Lévitique 16.2 Romains 8.28-8.39 Hébreux 9.7 Lévitique 16.15 Hébreux 9.3
20 alimoingia Yesu kwa ajili yetu, mtangulizi wetu, amekuwa kuhani mkuu hata milele kwa mfano wa Melkizedeki.
Hébreux 4.14 Hébreux 5.6 Hébreux 8.1 Hébreux 9.24 Hébreux 12.2

Cette Bible est dans le domaine public.