Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

2 Timothée 4.11
Bible en Swahili de l’est


1 Nakuagiza mbele za Mungu, na mbele za Kristo Yesu, atakayewahukumu walio hai na waliokufa; kwa kufunuliwa kwake na kwa ufalme wake;
Actes 10.42 1 Timothée 5.21 2 Timothée 2.14 Matthieu 16.27 2 Timothée 4.8
2 lihubiri neno, uwe tayari, wakati ukufaao na wakati usiokufaa, karipia, kemea, na kuonya kwa uvumilivu wote na mafundisho.
Tite 2.15 Tite 1.13 1 Timothée 5.20 1 Timothée 4.13 Apocalypse 3.19
3 Maana utakuja wakati watakapoyakataa mafundisho yenye uzima; ila kwa kuzifuata nia zao wenyewe watajipatia waalimu makundi makundi, kwa kuwa wana masikio ya utafiti;
2 Timothée 3.1-3.6 Jérémie 6.16-6.17 2 Pierre 2.1-2.3 Michée 2.11 1 Corinthiens 2.1
4 nao watajiepusha wasisikie yaliyo kweli, na kuzigeukia hadithi za uongo.
1 Timothée 1.4 Tite 1.14 1 Timothée 4.7 2 Pierre 1.16 Zacharie 7.11
5 Bali wewe, uwe na kiasi katika mambo yote, vumilia mabaya, fanya kazi ya mhubiri wa Injili, timiliza huduma yako.
2 Timothée 1.8 2 Timothée 2.3 Actes 21.8 Colossiens 4.17 2 Timothée 3.10-3.12
6 Kwa maana, mimi sasa namiminwa, na wakati wa kufariki kwangu umefika.
Philippiens 1.23 Philippiens 2.17 Josué 23.14 Nombres 27.12-27.17 2 Pierre 1.14-1.15
7 Nimevipiga vita vilivyo vizuri, mwendo nimeumaliza, Imani nimeilinda;
1 Timothée 6.12 Actes 20.24 1 Corinthiens 9.24-9.27 1 Timothée 1.18 Philippiens 3.13-3.14
8 baada ya hayo nimewekewa taji ya haki, ambayo Bwana, mhukumu mwenye haki, atanipa siku ile; wala si mimi tu, bali na watu wote pia waliopenda kufunuliwa kwake.
Jacques 1.12 Colossiens 1.5 2 Timothée 1.12 2 Timothée 4.1 2 Timothée 2.5

Dernières informations et salutations

9 Jitahidi kuja kwangu upesi.
2 Timothée 1.4 2 Timothée 4.21
10 Maana Dema aliniacha, akiupenda ulimwengu huu wa sasa, akasafiri kwenda Thesalonike; Kreske amekwenda Galatia; Tito amekwenda Dalmatia.
Philémon 1.24 Actes 16.6 2 Timothée 1.15 2 Corinthiens 7.6 Luc 14.26-14.27
11 Luka peke yake yupo hapa pamoja nami. Umtwae Marko, umlete pamoja nawe, maana anifaa kwa utumishi.
Actes 12.12 Actes 15.39 Colossiens 4.10 Philémon 1.24 Colossiens 4.14
12 Lakini Tikiko nalimpeleka Efeso.
Actes 20.4 Ephésiens 6.21 Colossiens 4.7 Tite 3.12 Actes 20.16-20.17
13 Lile joho nililoliacha kwa Karpo huko Troa, ujapo ulilete, na vile vitabu, hasa vile vya ngozi.
Actes 16.8 1 Corinthiens 4.11 2 Corinthiens 11.27 Actes 20.5-20.12 Actes 16.11
14 Iskanda, mfua shaba, alionyesha ubaya mwingi kwangu; Bwana atamlipa sawasawa na matendo yake.
1 Timothée 1.20 Psaumes 28.4 1 Samuel 24.12 Apocalypse 18.6 Jérémie 18.19-18.23
15 Nawe ujihadhari na huyo, kwa sababu aliyapinga sana maneno yetu.
2 Timothée 3.8 Matthieu 10.16-10.17 Philippiens 3.2
16 Katika jawabu langu la kwanza hakuna mtu aliyesimama upande wangu, bali wote waliniacha; naomba wasihesabiwe hatia kwa jambo hilo.
Actes 7.60 2 Timothée 1.15 2 Corinthiens 7.11 Actes 25.16 Philippiens 1.7
17 Lakini Bwana alisimama pamoja nami akanitia nguvu, ili kwa kazi yangu ule ujumbe utangazwe kwa utimilifu, hata wasikie Mataifa yote; nami nikaokolewa katika kinywa cha simba.
Psaumes 22.21 Actes 9.15 Daniel 6.22 1 Pierre 5.8 Actes 23.11
18 Bwana ataniokoa na kila neno baya, na kunihifadhi hata nifike ufalme wake wa mbinguni. Utukufu una Yeye milele na milele. Amina.
Romains 11.36 Psaumes 121.7 Matthieu 6.13 Jude 1.24-1.25 Psaumes 37.28
19 Nisalimie Priska na Akila, na wale wa nyumbani mwa Onesiforo.
Actes 18.2 Actes 18.26 1 Corinthiens 16.19 Actes 18.18 Romains 16.3-16.4
20 Erasto alikaa Korintho. Trofimo nalimwacha huko Mileto, hawezi.
Actes 20.4 Actes 21.29 Actes 19.22 Actes 20.15 Romains 16.23
21 Jitahidi kuja kabla ya wakati wa baridi. Eubulo akusalimu, na Pude, na Lino, na Klaudia, na ndugu wote pia.
2 Timothée 4.9 2 Timothée 4.13 1 Corinthiens 16.20 3 Jean 1.14 2 Timothée 1.4
22 Bwana na awe pamoja na roho yako. Neema na iwe pamoja nanyi.
Colossiens 4.18 Galates 6.18 Philémon 1.25 Ephésiens 6.24 Romains 16.20

Cette Bible est dans le domaine public.