Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Deutéronome 15.19
Bible en Swahili de l’est


L’année de relâche

1 Kila miaka saba, mwisho wake, fanya maachilio.
Deutéronome 31.10 Exode 23.10-23.11 Lévitique 25.2-25.4 Jérémie 36.8-36.18 Exode 21.2
2 Na jinsi ya maachilio ni hii, kila mkopeshaji na akiache alichomkopesha mwenziwe, wala asimlipize mwenziwe wala nduguye; kwa kuwa imepigwa mbiu ya maachilio ya Bwana.
Néhémie 5.7-5.11 Esaïe 58.3 Amos 8.4-8.6 Luc 6.34-6.38 Luc 7.42
3 Waweza kumtoza mgeni; lakini kila uwiacho kwa nduguyo mkono wako utamwachilia.
Deutéronome 23.20 Galates 6.10 1 Corinthiens 6.6-6.7 Matthieu 17.25-17.26 Exode 22.25
4 Lakini hawatakuwako maskini kwenu; (kwa kuwa Bwana atakubarikia kweli katika nchi akupayo Bwana, Mungu wako, uimiliki, iwe urithi wako;)
Esaïe 58.10-58.11 Proverbes 11.24-11.25 Deutéronome 14.29 Deutéronome 28.1-28.8 Deutéronome 28.11
5 kwamba utaisikiza tu kwa bidii sauti ya Bwana, Mungu wako, uyatunze maagizo haya yote nikuagizayo leo, kuyafanya.
Philippiens 1.27 Josué 1.7 Deutéronome 11.13-11.15 Psaumes 19.11 Deutéronome 4.9
6 Kwani Bwana, Mungu wako, atakubarikia, kama alivyokuahidi; nawe utakopesha mataifa mengi, lakini hutakopa; tena utayatawala mataifa mengi, usitawaliwe na wao.
Deutéronome 28.12-28.13 Deutéronome 28.44 1 Rois 4.24 Esdras 4.20 Proverbes 22.7
7 Kama akiwapo mtu maskini pamoja nawe, nduguzo mmojawapo, ndani ya malango yako mojawapo, katika nchi yako akupayo Bwana, Mungu wako, usifanye moyo wako kuwa mgumu, wala usimfumbie mkono wako nduguyo maskini;
Proverbes 21.13 Jacques 2.15-2.16 Deutéronome 15.9 1 Jean 3.16-3.17 Matthieu 18.30
8 lakini mfumbulie mkono wako kwa kweli, umkopeshe kwa kweli yatoshayo haja yake katika ahitajiayo.
Luc 6.34 Matthieu 5.42
9 Jitunze, msiwe na neno lisilofaa moyoni mwako, kusema, Umekaribia mwaka wa saba, mwaka wa maachilio; jicho lako likawa ovu juu ya nduguyo usimpe kitu; naye akamlilia Bwana juu yako, ikawa ni dhambi kwako.
Deutéronome 24.15 Matthieu 20.15 Proverbes 23.6 Jacques 5.4 Proverbes 28.22
10 Mpe kwa kweli, wala moyo wako usisikitike utakapompa; kwa kuwa atakubarikia Bwana, Mungu wako, kwa neno hili katika kazi yako yote, na katika kila utakalotia mkono wako.
Deutéronome 14.29 Deutéronome 24.19 Proverbes 22.9 2 Corinthiens 9.5-9.11 1 Pierre 4.11
11 Kwa maana maskini hawatakoma katika nchi milele; ndipo ninakuamuru na kukuambia, Mfumbulie kwa kweli mkono wako nduguyo, mhitaji wako, maskini wako, katika nchi yako.
Marc 14.7 Matthieu 26.11 Jean 12.8 Deutéronome 15.8 2 Corinthiens 8.2-8.9
12 Ikiwa nduguyo, mume wa Kiebrania, au mwanamke wa Kiebrania, akiuzwa kwako, naye amekutumikia miaka sita; basi mwaka wa saba mwache huru aondoke kwako.
Jérémie 34.14 Lévitique 25.39-25.41 Exode 21.2-21.6 Deutéronome 15.1 Jean 8.35-8.36
13 Nawe utakapomwacha huru aondoke kwako, usimwache aende zake mikono mitupu;
Proverbes 3.27-3.28 Genèse 31.42 Jérémie 22.13 Exode 3.21 Malachie 3.5
14 umwangalie kwa wema katika kundi lako, na sakafu yako ya nafaka, na kinu chako cha divai; mpe kama alivyokubarikia Bwana, Mungu wako.
Proverbes 10.22 Psaumes 68.10 Néhémie 8.10 1 Corinthiens 16.2 Actes 20.35
15 Nawe kumbuka kwamba ulikuwa mtumwa katika nchi ya Misri, akakukomboa Bwana, Mungu wako; kwa hiyo mimi nakuamuru neno hili hivi leo.
Deutéronome 16.12 Matthieu 6.14-6.15 Ephésiens 1.7 Ephésiens 2.12 1 Jean 3.16
16 Hata itakuwa, akikuambia, Siondoki kwako; kwa sababu akupenda wewe na nyumba yako, kwa kuwa yu hali njema kwako;
Exode 21.5-21.6 Psaumes 40.6 Psaumes 40.8
17 ndipo utwae uma, uupenyeze katika sikio lake uingie katika ubao wa mlango, naye atakuwa mtumishi wako milele. Na kijakazi chako naye mfanye vivyo.
Lévitique 25.39-25.42 1 Samuel 1.22
18 Wala usione ugumu, utakapomwacha huru kuondoka kwako; kwani amekutumikia miaka sita kwa ujira mara mbili wa mwajiriwa; na Bwana, Mungu wako, atakubarikia kwa yote utakayofanya.
Luc 17.7-17.8 Esaïe 16.14 Esaïe 21.16

Les premiers-nés des animaux

19 Wazaliwa wa kwanza waume wote wazaliwao katika kundi lako la ng’ombe na la kondoo, uwatakase kwa Bwana, Mungu wako; usifanye kazi kwa mzaliwa wa kwanza wa ng’ombe wako, wala usimkate manyoya mzaliwa wa kwanza wa kundi lako la kondoo.
Exode 13.2 Exode 13.12 Lévitique 27.26 Deutéronome 16.14 Deutéronome 12.17
20 Utamla mbele za Bwana, Mungu wako, mwaka hata mwaka mahali atakapochagua Bwana, wewe na nyumba yako.
Deutéronome 14.23 Deutéronome 12.5-12.7 Deutéronome 12.17
21 Lakini akiwa na kilema, akichechea, au akiwa kipofu, au mwenye kilema kibaya cho chote, usimsongezee Bwana, Mungu wako, sadaka.
Deutéronome 17.1 Lévitique 22.19-22.25 Malachie 1.7-1.8
22 Utamla ndani ya malango yako; wasio tohara na wenye tohara pia watakula, kama unavyokula paa na kulungu.
Deutéronome 12.21-12.22 Deutéronome 12.15-12.16
23 Pamoja na haya usile damu yake; uimwage nchi kama maji.
Deutéronome 12.16 Deutéronome 12.23 Lévitique 7.26 Ezéchiel 33.25 1 Samuel 14.32

Cette Bible est dans le domaine public.