Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

1 Corinthiens 14.26
Bible en Swahili de l’est


Objectif et exercice des dons

1 Ufuateni upendo, na kutaka sana karama za rohoni, lakini zaidi kwamba mpate kuhutubu.
1 Corinthiens 12.1 1 Corinthiens 14.39 1 Corinthiens 16.14 Hébreux 12.14 1 Timothée 4.14
2 Maana yeye anenaye kwa lugha, hasemi na watu, bali husema na Mungu; maana hakuna asikiaye; lakini anena mambo ya siri katika roho yake.
1 Corinthiens 13.2 Actes 10.46 Actes 19.6 Marc 16.17 Romains 16.25
3 Bali yeye ahutubuye, asema na watu maneno ya kuwajenga, na kuwafariji, na kuwatia moyo.
1 Corinthiens 14.12 Ephésiens 6.22 2 Timothée 4.2 1 Timothée 4.13 1 Corinthiens 14.4-14.5
4 Yeye anenaye kwa lugha hujijenga nafsi yake; bali ahutubuye hulijenga kanisa.
1 Corinthiens 14.22 1 Corinthiens 14.26 Marc 16.17 1 Corinthiens 14.5 1 Corinthiens 13.2
5 Nami nataka ninyi nyote mnene kwa lugha, lakini zaidi sana mpate kuhutubu, maana yeye ahutubuye ni mkuu kuliko yeye anenaye kwa lugha, isipokuwa afasiri, ili kusudi kanisa lipate kujengwa.
1 Corinthiens 12.10 1 Corinthiens 13.1 Marc 16.17 1 Corinthiens 14.18-14.40 1 Corinthiens 12.28-12.30
6 Ila sasa, ndugu, nikija kwenu na kunena kwa lugha, nitawafaidia nini, isipokuwa nasema nanyi kwa njia ya ufunuo, au kwa njia ya elimu, au kwa njia ya hotuba, au kwa njia ya fundisho?
Ephésiens 1.17 Romains 6.17 Romains 15.14 Philippiens 3.15 Matthieu 11.25
7 Hata vitu visivyo na uhai vitoapo sauti, ikiwa ni filimbi, ikiwa ni kinubi, visipotoa sauti zilizo na tofauti, itatambulikanaje ni wimbo gani unaopigwa kwa filimbi au kwa kinubi?
1 Corinthiens 13.1 Luc 7.32 Nombres 10.2-10.10 1 Corinthiens 14.8 Matthieu 11.17
8 Kwa maana baragumu ikitoa sauti isiyojulikana, ni nani atakayejifanya tayari kwa vita?
Nombres 10.9 Jérémie 4.19 Ezéchiel 33.3-33.6 Josué 6.4-6.20 Esaïe 27.13
9 Vivyo hivyo na ninyi, msipotoa kwa ulimi neno lililo dhahiri, neno lile linenwalo litajulikanaje? Maana mtakuwa mkinena hewani tu.
1 Corinthiens 9.26
10 Yamkini ziko sauti za namna nyingi duniani, wala hakuna moja isiyo na maana.
11 Basi nisipoijua maana ya ile sauti nitakuwa kama mjinga kwake yeye anenaye; naye anenaye atakuwa mjinga kwangu.
Actes 28.2 1 Corinthiens 14.21 Colossiens 3.11 Actes 28.4 Romains 1.14
12 Vivyo hivyo na ninyi, kwa kuwa mnatamani sana kuwa watu wenye karama za roho, takeni kwamba mzidi sana kuwa nazo ili kulijenga kanisa.
1 Corinthiens 14.26 Tite 2.14 1 Corinthiens 12.31 1 Corinthiens 14.3-14.4 1 Corinthiens 12.7
13 Kwa sababu hiyo yeye anenaye kwa lugha na aombe apewe kufasiri.
1 Corinthiens 12.30 Actes 8.15 Jean 14.13-14.14 1 Corinthiens 14.27-14.28 Marc 11.24
14 Maana nikiomba kwa lugha, roho yangu huomba, lakini akili zangu hazina matunda.
1 Corinthiens 14.15-14.16 1 Corinthiens 14.2 1 Corinthiens 14.19
15 Imekuwaje, basi? Nitaomba kwa roho, tena nitaomba kwa akili pia; mtaimba kwa roho, tena nitaimba kwa akili pia.
Colossiens 3.16 Ephésiens 6.18 Jean 4.23-4.24 Psaumes 47.7 1 Corinthiens 10.19
16 Kwa maana wewe ukibariki kwa roho, yeye aketiye katika mahali pa mjinga ataitikaje, Amina, baada ya kushukuru kwako, akiwa hayajui usemayo?
Apocalypse 5.14 Psaumes 106.48 1 Chroniques 16.36 1 Corinthiens 11.24 Deutéronome 27.15-27.26
17 Maana ni kweli, wewe washukuru vema, bali yule mwingine hajengwi.
1 Corinthiens 14.4 1 Corinthiens 14.6
18 Namshukuru Mungu ya kuwa nanena kwa lugha zaidi ya ninyi nyote;
1 Corinthiens 4.7 1 Corinthiens 1.4-1.6
19 lakini katika kanisa napenda kunena maneno matano kwa akili zangu, nipate kuwafundisha wengine, zaidi ya kunena maneno kumi elfu kwa lugha.
1 Corinthiens 14.21-14.22 1 Corinthiens 14.4
20 Ndugu zangu, msiwe watoto katika akili zenu; lakini katika uovu mgeuzwe watoto wachanga, bali katika akili zenu mkawe watu wazima.
Romains 16.19 1 Pierre 2.2 Hébreux 5.12-5.13 Matthieu 18.3 Psaumes 119.99
21 Imeandikwa katika torati, Nitasema na watu hawa kwa watu wa lugha nyingine, na kwa midomo ya wageni, wala hata hivyo hawatanisikia, asema Bwana.
Esaïe 28.11-28.12 Jean 10.34 Deutéronome 28.49 Jérémie 5.15 Romains 3.19
22 Basi, hizi lugha ni ishara, si kwao waaminio, bali kwao wasioamini lakini kuhutubu si kwa ajili yao wasioamini, bali kwa ajili yao waaminio.
Marc 16.17 Actes 2.6-2.12 1 Corinthiens 14.1 1 Timothée 1.9 Actes 2.32-2.36
23 Haya! Ikiwa kanisa lote limekusanyika pamoja, na wote wanene kwa lugha, kisha ikawa wameingia watu wajinga au wasioamini, je! Hawatasema ya kwamba mna wazimu?
Actes 2.13 Jean 10.20 1 Corinthiens 11.18 Osée 9.7 Actes 26.24
24 Lakini wote wakihutubu, kisha akaingia mtu asiyeamini, au mjinga, abainishwa na wote, ahukumiwa na wote;
Hébreux 4.12-4.13 Actes 2.37 1 Corinthiens 2.15 Jean 1.47-1.49 Jean 4.29
25 siri za moyo wake huwa wazi; na hivyo atamwabudu Mungu, akianguka kifudifudi, na kukiri ya kuwa Mungu yu kati yenu bila shaka.
Esaïe 45.14 Zacharie 8.23 Deutéronome 9.18 Luc 17.16 Esaïe 60.14
26 Basi, ndugu, imekuwaje? Mkutanapo pamoja, kila mmoja ana zaburi, ana fundisho, ana ufunuo, ana lugha, ana tafsiri. Mambo yote na yatendeke kwa kusudi la kujenga.
Ephésiens 5.19 Romains 14.19 1 Thessaloniciens 5.11 1 Corinthiens 12.7-12.10 2 Corinthiens 13.10
27 Kama mtu akinena kwa lugha, wanene wawili au watatu, si zaidi, tena zamu kwa zamu, na mmoja na afasiri.
1 Corinthiens 14.26
28 Lakini asipokuwapo mwenye kufasiri na anyamaze katika kanisa; aseme na nafsi yake tena na Mungu.
29 Na manabii wanene wawili, au watatu, na wengine wapambanue.
1 Corinthiens 12.10 1 Jean 4.1-4.3 1 Thessaloniciens 5.19-5.21 1 Corinthiens 14.39
30 Lakini mwingine aliyeketi akifunuliwa neno, yule wa kwanza na anyamaze.
1 Thessaloniciens 5.19-5.20 Job 32.15-32.20 1 Corinthiens 14.6 Job 33.31-33.33 Job 32.11
31 Kwa maana ninyi nyote mwaweza kuhutubu mmoja mmoja, ili wote wapate kujifunza, na wote wafarijiwe.
Ephésiens 4.11-4.12 1 Corinthiens 14.35 1 Corinthiens 14.3 Proverbes 9.9 1 Thessaloniciens 5.11
32 Na roho za manabii huwatii manabii.
1 Jean 4.1 2 Rois 2.3 Jérémie 20.9 1 Corinthiens 14.29-14.30 Actes 4.19-4.20
33 Kwa maana Mungu si Mungu wa machafuko, bali wa amani; vile vile kama ilivyo katika makanisa yote ya watakatifu.
Jacques 3.17-3.18 1 Corinthiens 14.40 Hébreux 13.20 2 Thessaloniciens 3.16 1 Corinthiens 7.15
34 Wanawake na wanyamaze katika kanisa, maana hawana ruhusa kunena bali watii, kama vile inenavyo torati nayo.
Genèse 3.16 1 Timothée 2.11-2.12 1 Corinthiens 11.5 1 Corinthiens 14.35 Esther 1.17-1.20
35 Nao wakitaka kujifunza neno lo lote, na wawaulize waume zao wenyewe nyumbani mwao; maana ni aibu wanawake kunena katika kanisa.
Ephésiens 5.12 Ephésiens 5.25-5.27 1 Corinthiens 11.14 1 Pierre 3.7 1 Corinthiens 14.34
36 Au je! Neno la Mungu lilitoka kwenu? Au kuwafikia ninyi peke yenu?
Actes 18.1-18.17 1 Thessaloniciens 1.8 Zacharie 14.8 Actes 15.35-15.36 Michée 4.1-4.2
37 Mtu akijiona kuwa ni nabii au mtu wa rohoni, na ayatambue hayo ninayowaandikia, ya kwamba ni maagizo ya Bwana.
1 Jean 4.6 2 Corinthiens 10.7 Nombres 24.16 Nombres 24.3-24.4 Luc 10.16
38 Lakini mtu akiwa mjinga, na awe mjinga.
2 Timothée 4.3-4.4 Matthieu 7.6 Osée 4.17 Matthieu 15.14 1 Timothée 6.3-6.5
39 Kwa ajili ya hayo, ndugu, takeni sana kuhutubu, wala msizuie kunena kwa lugha.
1 Corinthiens 12.31 1 Corinthiens 14.1 1 Corinthiens 14.5 1 Thessaloniciens 5.20 1 Corinthiens 14.3
40 Lakini mambo yote na yatendeke kwa uzuri na kwa utaratibu.
Colossiens 2.5 Tite 1.5 1 Corinthiens 11.34 1 Corinthiens 14.26-14.33 Romains 13.13

Cette Bible est dans le domaine public.