Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

1 Corinthiens 13.4
Bible en Swahili de l’est


Les dons spirituels et l’amour

1 Nijaposema kwa lugha za wanadamu na za malaika, kama sina upendo, nimekuwa shaba iliayo na upatu uvumao.
1 Timothée 1.5 1 Pierre 4.8 Galates 5.6 Galates 5.22 2 Pierre 2.18
2 Tena nijapokuwa na unabii, na kujua siri zote na maarifa yote, nijapokuwa na imani timilifu kiasi cha kuweza kuhamisha milima, kama sina upendo, si kitu mimi.
1 Corinthiens 13.3 Matthieu 17.20 Matthieu 21.21 1 Corinthiens 16.22 1 Jean 4.8
3 Tena nikitoa mali zangu zote kuwalisha maskini, tena nikijitoa mwili wangu niungue moto, kama sina upendo, hainifaidii kitu.
Jacques 2.14-2.17 Hébreux 13.9 Jérémie 7.8 Daniel 3.16-3.28 Luc 21.3-21.4
4 Upendo huvumilia, hufadhili; upendo hauhusudu; upendo hautakabari; haujivuni;
1 Pierre 4.8 Proverbes 10.12 Colossiens 3.12 1 Thessaloniciens 5.14 1 Jean 4.11
5 haukosi kuwa na adabu; hautafuti mambo yake; hauoni uchungu; hauhesabu mabaya;
1 Corinthiens 10.24 Philippiens 2.21 1 Jean 3.16-3.17 Jacques 1.19 Romains 15.1-15.2
6 haufurahii udhalimu, bali hufurahi pamoja na kweli;
2 Jean 1.4 Proverbes 14.9 2 Thessaloniciens 2.12 Romains 1.32 2 Samuel 4.10-4.12
7 huvumilia yote; huamini yote; hutumaini yote; hustahimili yote.
1 Pierre 4.8 2 Timothée 2.24 1 Corinthiens 13.4 2 Timothée 2.3-2.10 Galates 6.2
8 Upendo haupungui neno wakati wo wote; bali ukiwapo unabii utabatilika; zikiwapo lugha, zitakoma; yakiwapo maarifa, yatabatilika.
Hébreux 8.13 Actes 19.6 1 Corinthiens 12.28-12.30 1 Corinthiens 13.13 Actes 2.4
9 Kwa maana tunafahamu kwa sehemu; na tunafanya unabii kwa sehemu;
1 Corinthiens 8.2 1 Corinthiens 13.12 1 Corinthiens 2.9 Ephésiens 3.18-3.19 Matthieu 11.27
10 lakini ijapo ile iliyo kamili, iliyo kwa sehemu itabatilika.
Apocalypse 22.4-22.5 Apocalypse 21.22-21.23 2 Corinthiens 5.7-5.8 Esaïe 60.19-60.20 1 Corinthiens 13.12
11 Nilipokuwa mtoto mchanga, nalisema kama mtoto mchanga, nalifahamu kama mtoto mchanga, nalifikiri kama mtoto mchanga; tokea hapo nilipokuwa mtu mzima, nimeyabatilisha mambo ya kitoto.
1 Corinthiens 14.20 1 Corinthiens 3.1-3.2 Galates 4.1 Ecclésiaste 11.10
12 Maana wakati wa sasa tunaona kwa kioo kwa jinsi ya fumbo; wakati ule tutaona uso kwa uso; wakati wa sasa nafahamu kwa sehemu; wakati ule nitajua sana kama mimi nami ninavyojuliwa sana.
1 Jean 3.2 2 Corinthiens 3.18 Philippiens 3.12 1 Corinthiens 13.9-13.10 Matthieu 5.8
13 Basi, sasa inadumu imani, tumaini, upendo, haya matatu; na katika hayo lililo kuu ni upendo.
1 Corinthiens 16.14 1 Corinthiens 13.1-13.8 1 Jean 4.7-4.18 Colossiens 3.14 Galates 5.6

Cette Bible est dans le domaine public.