Les dons spirituels et l’amour
 1  Nijaposema kwa lugha za wanadamu na za malaika, kama sina upendo, nimekuwa shaba iliayo na upatu uvumao. 
1 Pierre 4.8  1 Timothée 1.5  Galates 5.6  Galates 5.22  2 Pierre 2.18  
 2  Tena nijapokuwa na unabii, na kujua siri zote na maarifa yote, nijapokuwa na imani timilifu kiasi cha kuweza kuhamisha milima, kama sina upendo, si kitu mimi. 
1 Corinthiens 13.3  Matthieu 17.20  Matthieu 21.21  1 Corinthiens 16.22  1 Jean 4.8  
 3  Tena nikitoa mali zangu zote kuwalisha maskini, tena nikijitoa mwili wangu niungue moto, kama sina upendo, hainifaidii kitu. 
Jacques 2.14-2.17  Hébreux 13.9  Jean 13.37  Philippiens 1.15-1.18  Jean 6.63  
 4  Upendo huvumilia, hufadhili; upendo hauhusudu; upendo hautakabari; haujivuni; 
1 Pierre 4.8  Proverbes 10.12  Colossiens 3.12  1 Thessaloniciens 5.14  1 Jean 4.11  
 5  haukosi kuwa na adabu; hautafuti mambo yake; hauoni uchungu; hauhesabu mabaya; 
1 Corinthiens 10.24  Philippiens 2.21  1 Jean 3.16-3.17  Jacques 1.19  Esaïe 3.5  
 6  haufurahii udhalimu, bali hufurahi pamoja na kweli; 
2 Jean 1.4  Proverbes 14.9  2 Thessaloniciens 2.12  Romains 1.32  Jérémie 13.17  
 7  huvumilia yote; huamini yote; hutumaini yote; hustahimili yote. 
1 Pierre 4.8  2 Timothée 2.24  1 Corinthiens 13.4  2 Timothée 2.3-2.10  1 Corinthiens 9.12  
 8  Upendo haupungui neno wakati wo wote; bali ukiwapo unabii utabatilika; zikiwapo lugha, zitakoma; yakiwapo maarifa, yatabatilika. 
Hébreux 8.13  Actes 19.6  1 Corinthiens 13.13  Actes 2.4  1 Corinthiens 12.28-12.30  
 9  Kwa maana tunafahamu kwa sehemu; na tunafanya unabii kwa sehemu; 
1 Corinthiens 8.2  1 Corinthiens 13.12  Ephésiens 3.8  1 Jean 3.2  Romains 11.34  
 10  lakini ijapo ile iliyo kamili, iliyo kwa sehemu itabatilika. 
Apocalypse 22.4-22.5  Apocalypse 21.22-21.23  2 Corinthiens 5.7-5.8  Esaïe 60.19-60.20  1 Corinthiens 13.12  
 11  Nilipokuwa mtoto mchanga, nalisema kama mtoto mchanga, nalifahamu kama mtoto mchanga, nalifikiri kama mtoto mchanga; tokea hapo nilipokuwa mtu mzima, nimeyabatilisha mambo ya kitoto. 
1 Corinthiens 14.20  1 Corinthiens 3.1-3.2  Galates 4.1  Ecclésiaste 11.10  
 12  Maana wakati wa sasa tunaona kwa kioo kwa jinsi ya fumbo; wakati ule tutaona uso kwa uso; wakati wa sasa nafahamu kwa sehemu; wakati ule nitajua sana kama mimi nami ninavyojuliwa sana. 
1 Jean 3.2  2 Corinthiens 3.18  Jacques 1.23  Philippiens 3.12  1 Corinthiens 13.9-13.10  
 13  Basi, sasa inadumu imani, tumaini, upendo, haya matatu; na katika hayo lililo kuu ni upendo. 
1 Corinthiens 16.14  1 Corinthiens 13.1-13.8  1 Jean 4.7-4.18  Colossiens 3.14  Galates 5.6