Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Romains 15.9
Bible en Swahili de l’est


1 Basi imetupasa sisi tulio na nguvu kuuchukua udhaifu wao wasio na nguvu, wala haitupasi kujipendeza wenyewe.
Romains 14.1 Galates 6.1-6.2 1 Thessaloniciens 5.14 1 Corinthiens 9.22 1 Corinthiens 12.22-12.24
2 Kila mtu miongoni mwetu na ampendeze jirani yake, apate wema, akajengwe.
1 Corinthiens 10.24 Romains 14.19 1 Corinthiens 13.5 Philippiens 2.4-2.5 1 Corinthiens 9.19-9.22
3 Kwa maana Kristo naye hakujipendeza mwenyewe; bali kama ilivyoandikwa, Malaumu yao waliokulaumu wewe yalinipata mimi.
Psaumes 69.9 Jean 5.30 Philippiens 2.8 Jean 6.38 Jean 12.27-12.28
4 Kwa kuwa yote yaliyotangulia kuandikwa yaliandikwa ili kutufundisha sisi; ili kwa saburi na faraja ya maandiko tupate kuwa na tumaini.
1 Corinthiens 10.11 2 Timothée 3.16-3.17 Romains 4.23-4.24 2 Pierre 1.20-1.21 1 Corinthiens 9.9-9.10
5 Na Mungu mwenye saburi na faraja awajalie kunia mamoja ninyi kwa ninyi, kwa mfano wa Kristo Yesu;
Romains 12.16 1 Pierre 3.8 Philippiens 2.4-2.5 Ephésiens 5.2 1 Corinthiens 1.10
6 ili kwa moyo mmoja na kwa kinywa kimoja mpate kumtukuza Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo.
2 Corinthiens 11.31 1 Pierre 1.3 Ephésiens 1.3 Jean 20.17 Actes 4.32
7 Kwa hiyo mkaribishane ninyi kwa ninyi, kama naye Kristo alivyotukaribisha, ili Mungu atukuzwe.
Jean 13.34 2 Thessaloniciens 1.10-1.12 Ephésiens 1.6-1.8 Romains 14.1-14.3 Jean 6.37
8 Kwa maana nasema, ya kwamba Kristo amefanyika mhudumu wa agano la kutahiriwa kwa ajili ya kweli ya Mungu, kusudi azithibitishe ahadi walizopewa baba zetu;
Matthieu 15.24 2 Corinthiens 1.20 Actes 3.25-3.26 Jean 1.11 Romains 9.4-9.5
9 tena ili Mataifa wamtukuze Mungu kwa ajili ya rehema zake; kama ilivyoandikwa, Kwa hiyo nitakushukuru kati ya Mataifa, Nami nitaliimbia jina lako.
2 Samuel 22.50 Psaumes 18.49 Romains 3.29 Matthieu 9.8
10 Na tena anena, Furahini,Mataifa,pamoja na watu wake.
Deutéronome 32.43 Psaumes 66.1-66.4 Esaïe 42.10-42.12 Psaumes 138.4-138.5 Psaumes 97.1
11 Na tena, Enyi Mataifa yote,msifuni Bwana; Enyi watu wote,mhimidini.
Psaumes 117.1
12 Na tena Isaya anena, Litakuwako shina la Yese, Naye aondokeaye kuwatawala Mataifa; Ndiye Mataifa watakayemtumaini.
Matthieu 12.21 Esaïe 11.10 Apocalypse 22.16 Esaïe 11.1 Apocalypse 5.5
13 Basi Mungu wa tumaini na awajaze ninyi furaha yote na amani katika kuamini, mpate kuzidi sana kuwa na tumaini, katika nguvu za Roho Mtakatifu.
Romains 14.17 2 Thessaloniciens 2.16-2.17 Romains 12.12 Romains 5.4-5.5 1 Corinthiens 2.4

Ministère et projets de Paul

14 Ndugu zangu, nimehakikishwa mimi mwenyewe kwa habari zenu ya kuwa ninyi nanyi mmejaa wema, mmejazwa elimu yote, tena mwaweza kuonyana.
1 Corinthiens 8.7 1 Corinthiens 8.1 2 Pierre 1.12 1 Jean 2.21 1 Corinthiens 8.10
15 Lakini nawaandikia, kwa ujasiri zaidi katika sehemu za waraka huu, kana kwamba kuwakumbusha, kwa neema ile niliyopewa na Mungu,
Romains 12.3 Romains 1.5 2 Pierre 3.15 1 Corinthiens 15.10 Jude 1.3-1.5
16 ili niwe mhudumu wa Kristo Yesu kati ya watu wa Mataifa, niifanyie Injili ya Mungu kazi ya ukuhani, kusudi Mataifa wawe sadaka yenye kibali, ikiisha kutakaswa na Roho Mtakatifu.
Philippiens 2.17 Romains 11.13 Romains 1.1 Actes 9.15 Esaïe 66.19-66.20
17 Basi, nina sababu ya kuona fahari katika Kristo Yesu mbele za Mungu.
Hébreux 5.1 Hébreux 2.17 Philippiens 3.3 2 Corinthiens 12.11-12.21 2 Corinthiens 2.14-2.16
18 Maana sitathubutu kutaja neno asilolitenda Kristo kwa kazi yangu, Mataifa wapate kutii, kwa neno au kwa tendo,
Romains 1.5 Actes 21.19 Actes 15.12 Proverbes 25.14 Galates 2.8
19 kwa nguvu za ishara na maajabu, katika nguvu za Roho Mtakatifu; hata ikawa tangu Yerusalemu, na kando kando yake, mpaka Iliriko nimekwisha kuihubiri Injili ya Kristo kwa utimilifu;
2 Corinthiens 12.12 1 Corinthiens 12.4-12.11 Galates 3.5 Actes 22.17-22.21 2 Timothée 4.17
20 kadhalika nikijitahidi kuihubiri Injili, nisihubiri hapo ambapo jina la Kristo limekwisha kutajwa, nisije nikajenga juu ya msingi wa mtu mwingine;
2 Corinthiens 10.13-10.16 1 Corinthiens 3.9-3.15 Ephésiens 2.20-2.22
21 bali kama ilivyoandikwa, Wale wasiohubiriwa habari zake wataona, Na wale wasiojasikia watafahamu.
Esaïe 52.15 Esaïe 65.1
22 Ndiyo sababu nalizuiwa mara nyingi nisije kwenu.
Romains 1.13 1 Thessaloniciens 2.17-2.18
23 Lakini sasa, kwa kuwa sina wasaa tena pande hizi, tena tangu miaka mingi nina shauku kuja kwenu;
Romains 15.32 Romains 15.29 Actes 19.21 Romains 1.10-1.12 1 Thessaloniciens 3.10
24 wakati wo wote nitakaosafiri kwenda Spania [nitakuja kwenu.] Kwa maana nataraji kuwaona ninyi katika kusafiri kwangu, na kusafirishwa nanyi, moyo wangu ushibe kwenu kidogo.
Romains 15.28 Actes 15.3 Romains 1.12 Actes 21.5 3 Jean 1.6
25 Ila sasa ninakwenda Yerusalemu, nikiwahudumu watakatifu;
Actes 24.17 Actes 19.21 Actes 20.22 1 Corinthiens 16.1-16.3 Galates 2.10
26 maana imewapendeza watu wa Makedonia na Akaya kufanya changizo kwa ajili ya watakatifu huko Yerusalemu walio maskini.
Actes 11.27-11.30 2 Corinthiens 8.1-8.9 Galates 6.6-6.10 2 Corinthiens 9.12 Matthieu 26.11
27 Naam, imewapendeza, tena wamekuwa wadeni wao. Kwa maana ikiwa Mataifa wameyashiriki mambo yao ya roho, imewabidi kuwahudumu kwa mambo yao ya mwili.
1 Corinthiens 9.11 Galates 6.6 Romains 11.17 Philémon 1.19
28 Basi nikiisha kuimaliza kazi hiyo, na kuwatilia muhuri tunda hilo, nitapitia kwenu, kwenda Spania.
Romains 15.24 Proverbes 19.21 Jacques 4.13-4.15 Lamentations 3.37 Colossiens 1.6
29 Nami najua ya kuwa nikija kwenu nitakuja kwa utimilifu wa baraka ya Kristo.
Psaumes 16.11 Romains 1.10-1.12 Ephésiens 4.13 Ezéchiel 34.26 Ephésiens 3.19
30 Ndugu zangu, nawasihi kwa Bwana wetu Yesu Kristo, na kwa upendo wa Roho, jitahidini pamoja nami katika maombi yenu kwa ajili yangu mbele za Mungu;
Colossiens 4.12 2 Corinthiens 1.11 Colossiens 2.1 Philippiens 2.1 2 Corinthiens 12.10
31 kwamba niokolewe na wale wasioamini katika Uyahudi, na tena huduma yangu niliyo nayo huko Yerusalemu ikubalike kwa watakatifu;
2 Thessaloniciens 3.2 2 Corinthiens 8.4 2 Corinthiens 9.1 Romains 15.25 Actes 25.24
32 nipate kufika kwenu kwa furaha, kama apendavyo Mungu, nikapate kupumzika pamoja nanyi.
1 Corinthiens 16.18 Actes 18.21 Philémon 1.7 Philémon 1.20 2 Corinthiens 7.13
33 Mungu wa amani na awe pamoja nanyi nyote. Amina.
2 Corinthiens 13.11 1 Thessaloniciens 5.23 Philippiens 4.9 Romains 16.20 Hébreux 13.20

Cette Bible est dans le domaine public.