Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Romains 14.15
Bible en Swahili de l’est


1 Yeye aliye dhaifu wa imani, mkaribisheni, walakini msimhukumu mawazo yake.
Romains 15.1 Romains 15.7 1 Corinthiens 9.22 Luc 17.2 Romains 14.21
2 Mtu mmoja anayo imani, anakula vyote; lakini yeye aliye dhaifu hula mboga.
Romains 14.14 1 Timothée 4.4 Genèse 9.3 Tite 1.15 Genèse 1.29
3 Yeye alaye asimdharau huyo asiyekula, wala yeye asiyekula asimhukumu huyo alaye; kwa maana Mungu amemkubali.
Luc 18.9 Romains 14.10 Romains 14.13 Matthieu 7.1-7.2 Colossiens 2.16-2.17
4 Wewe u nani unayemhukumu mtumishi wa mwingine? Kwa bwana wake mwenyewe yeye husimama au huanguka. Naam, atasimamishwa, kwa kuwa Bwana aweza kumsimamisha.
Jacques 4.11-4.12 Romains 9.20 Romains 14.3 Romains 8.31-8.39 Jean 10.28-10.30
5 Mtu mmoja afanya tofauti kati ya siku na siku, mwingine aona siku zote kuwa sawasawa. Kila mtu na athibitike katika akili zake mwenyewe.
Romains 14.23 Romains 14.14 1 Corinthiens 8.7 Galates 4.9-4.10 1 Corinthiens 8.11
6 Yeye aadhimishaye siku, huiadhimisha kwa Bwana; naye alaye, hula kwa Bwana, kwa maana amshukuru Mungu; tena asiyekula, hali kwa Bwana, naye pia amshukuru Mungu.
1 Corinthiens 10.30-10.31 1 Timothée 4.3-4.5 Matthieu 15.36 Matthieu 14.19 Esaïe 58.5
7 Kwa sababu hakuna mtu miongoni mwetu aishiye kwa nafsi yake, wala hakuna afaye kwa nafsi yake.
2 Corinthiens 5.15 1 Thessaloniciens 5.10 1 Pierre 4.2 Galates 2.19-2.20 Romains 14.9
8 Kwa maana kama tukiishi, twaishi kwa Bwana, au kama tukifa, twafa kwa Bwana. Basi kama tukiishi au kama tukifa, tu mali ya Bwana.
Philippiens 1.20 Philippiens 2.30 1 Corinthiens 3.22-3.23 Actes 21.13 Jean 21.19
9 Maana Kristo alikufa akawa hai tena kwa sababu hii, awamiliki waliokufa na walio hai pia.
Apocalypse 1.18 Matthieu 28.18 1 Pierre 4.5 Hébreux 12.2 Actes 10.42
10 Lakini wewe je! Mbona wamhukumu ndugu yako? Au wewe je! Mbona wamdharau ndugu yako? Kwa maana sisi sote tutasimama mbele ya kiti cha hukumu cha Mungu.
2 Corinthiens 5.10 Romains 2.16 1 Corinthiens 4.5 Romains 14.3-14.4 Ecclésiaste 12.14
11 Kwa kuwa imeandikwa, Kama niishivyo, anena Bwana, kila goti litapigwa mbele zangu; Na kila ulimi utamkiri Mungu.
Esaïe 45.22-45.25 Philippiens 2.10-2.11 Romains 10.9 Esaïe 49.18 Psaumes 72.11
12 Basi ni hivyo, kila mtu miongoni mwetu atatoa habari zake mwenyewe mbele za Mungu.
1 Pierre 4.5 Matthieu 12.36 Matthieu 16.27 Luc 16.2 Galates 6.5
13 Basi tusizidi kuhukumiana, bali afadhali toeni hukumu hii, mtu asitie kitu cha kumkwaza ndugu au cha kumwangusha.
Luc 12.57 Jacques 4.11 Matthieu 7.1 Jacques 2.4 2 Corinthiens 6.3
14 Najua, tena nimehakikishwa sana katika Bwana Yesu, ya kuwa hakuna kitu kilicho najisi kwa asili yake, lakini kwake yeye akionaye kitu kuwa najisi, kwake huyo kitu kile ni najisi.
1 Corinthiens 8.7 Romains 14.2 Romains 14.20 1 Corinthiens 8.10 Actes 10.28
15 Na ndugu yako akiingia huzuni kwa sababu ya chakula, umeacha kwenda katika upendo. Kwa chakula chako usimharibu mtu yule ambaye Kristo alikufa kwa ajili yake.
Ephésiens 5.2 Galates 5.13 1 Corinthiens 8.11-8.12 Philippiens 2.2-2.4 Romains 13.10
16 Basi, huo wema wenu usitajwe kwa ubaya.
Romains 12.17 2 Corinthiens 8.20-8.21 1 Corinthiens 10.29-10.30 1 Thessaloniciens 5.22
17 Maana ufalme wa Mungu si kula wala kunywa, bali ni haki na amani na furaha katika Roho Mtakatifu.
Romains 15.13 Matthieu 6.33 1 Corinthiens 8.8 Galates 5.22 1 Corinthiens 4.20
18 Kwa kuwa yeye amtumikiaye Kristo katika mambo hayo humpendeza Mungu, tena hukubaliwa na wanadamu.
2 Corinthiens 8.21 Romains 16.18 Ecclésiaste 9.7 Jacques 2.18-2.26 1 Timothée 5.4
19 Basi kama ni hivyo, na mfuate mambo ya amani na mambo yafaayo kwa kujengana.
Romains 15.2 Psaumes 34.14 Hébreux 12.14 Ephésiens 4.29 Romains 12.18
20 Kwa ajili ya chakula usiiharibu kazi ya Mungu. Kweli, vyote ni safi; bali ni vibaya kwa mtu alaye na kujikwaza.
Romains 14.14-14.15 Actes 10.15 Tite 1.15 1 Timothée 4.3-4.5 Matthieu 18.6
21 Ni vyema kutokula nyama wala kunywa divai wala kutenda neno lo lote ambalo kwa hilo ndugu yako hukwazwa.
1 Corinthiens 8.13 Romains 14.13 Philippiens 1.10 Matthieu 18.7-18.10 Romains 15.1-15.2
22 Ile imani uliyo nayo uwe nayo nafsini mwako mbele za Mungu. Heri mtu yule asiyejihukumu nafsi yake katika neno lile analolikubali.
1 Jean 3.21 Romains 14.23 Romains 14.5 Galates 6.1 Romains 7.15
23 Lakini aliye na shaka, kama akila, amehukumiwa kuwa ana hatia, kwa maana hakula kwa imani. Na kila tendo lisilotoka katika imani ni dhambi.
1 Corinthiens 11.29-11.31 Romains 13.2 Romains 14.5 1 Corinthiens 8.7 Tite 1.15

Cette Bible est dans le domaine public.