Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Actes 1.17
Bible en Swahili de l’est


Témoignage à Jérusalem

Ascension de Christ

1 Kitabu kile cha kwanza nalikiandika, Theofilo, katika habari ya mambo yote aliyoanza Yesu kufanya na kufundisha,
Luc 1.3 Matthieu 11.5 Jean 10.32-10.38 Luc 24.19 Jean 18.19-18.21
2 hata siku ile alipochukuliwa juu, alipokuwa amekwisha kuwaagiza kwa Roho Mtakatifu wale mitume aliowachagua;
Actes 1.9 Jean 20.21 Jean 13.18 Actes 10.38 Matthieu 10.1-10.4
3 wale aliowadhihirishia nafsi yake, kwa dalili nyingi, baada ya kuteswa kwake, ya kwamba yu hai, akiwatokea muda wa siku arobaini, na kuyanena mambo yaliyouhusu ufalme wa Mungu.
1 Corinthiens 15.5-15.7 Jean 20.26 Actes 13.31 Matthieu 28.9 Daniel 2.44-2.45
4 Hata alipokuwa amekutana nao aliwaagiza wasitoke Yerusalemu, bali waingoje ahadi ya Baba, ambayo mlisikia habari zake kwangu;
Luc 24.49 Jean 14.16 Actes 2.33 Jean 15.26 Matthieu 10.20
5 ya kwamba Yohana alibatiza kwa maji, bali ninyi mtabatizwa katika Roho Mtakatifu baada ya siku hizi chache.
Matthieu 3.11 Luc 3.16 Actes 2.1-2.4 1 Corinthiens 12.13 Actes 11.15-11.16
6 Basi walipokutanika, wakamwuliza, wakisema, Je! Bwana, wakati huu ndipo unapowarudishia Israeli ufalme?
Matthieu 17.11 Genèse 49.10 Zacharie 9.9 Luc 19.11 Abdias 1.17-1.21
7 Akawaambia, Si kazi yenu kujua nyakati wala majira, Baba aliyoyaweka katika mamlaka yake mwenyewe.
Matthieu 24.36 Marc 13.32 Marc 10.40 Deutéronome 29.29 Daniel 2.21
8 Lakini mtapokea nguvu, akiisha kuwajilia juu yenu Roho Mtakatifu; nanyi mtakuwa mashahidi wangu katika Yerusalemu, na katika Uyahudi wote, na Samaria, na hata mwisho wa nchi.
Actes 10.38-10.41 Actes 4.33 Romains 15.19 Marc 16.15 Matthieu 28.19
9 Akiisha kusema hayo, walipokuwa wakitazama, akainuliwa, wingu likampokea kutoka machoni pao.
Daniel 7.13 Actes 1.2 Luc 24.50-24.51 Exode 19.9 Marc 16.19
10 Walipokuwa wakikaza macho mbinguni, yeye alipokuwa akienda zake, tazama, watu wawili wakasimama karibu nao, wenye nguo nyeupe,
Jean 20.12 Luc 24.4 Marc 16.5 Matthieu 28.3 Daniel 7.9
11 wakasema, Enyi watu wa Galilaya, mbona mmesimama mkitazama mbinguni? Huyu Yesu aliyechukuliwa kutoka kwenu kwenda juu mbinguni, atakuja jinsi iyo hiyo mlivyomwona akienda zake mbinguni.
Actes 2.7 Jean 14.3 Actes 13.31 Apocalypse 1.7 1 Thessaloniciens 4.16
12 Kisha wakarudi kwenda Yerusalemu kutoka mlima ulioitwa wa Mizeituni, ulio karibu na Yerusalemu, wapata mwendo wa sabato.
Luc 24.52 Matthieu 21.1 Luc 24.50 Jean 11.18 Matthieu 24.3
13 Hata walipoingia, wakapanda orofani, walipokuwa wakikaa; Petro, na Yohana, na Yakobo, na Andrea, Filipo na Tomaso, Bartholomayo na Mathayo, Yakobo wa Alfayo, na Simoni Zelote, na Yuda wa Yakobo.
Actes 20.8 Matthieu 10.2-10.4 Luc 22.12 Marc 2.14 Marc 14.15
14 Hawa wote walikuwa wakidumu kwa moyo mmoja katika kusali, pamoja nao wanawake, na Mariamu mama yake Yesu, na ndugu zake.
Actes 6.4 Actes 2.42 Matthieu 12.46 Ephésiens 6.18 Romains 12.12

Matthias désigné à la place de Judas

15 Siku zile akasimama Petro kati ya hao ndugu (jumla ya majina ilipata mia na ishirini), akasema,
1 Corinthiens 15.6 Apocalypse 11.13 Jean 14.12 Apocalypse 3.4 Actes 21.20
16 Ndugu, ilipasa andiko litimizwe, alilolinena Roho Mtakatifu zamani kwa kinywa cha Daudi, katika habari za Yuda aliyewaongoza wao waliomkamata Yesu;
Psaumes 41.9 Jean 13.18 Psaumes 55.12-55.15 Matthieu 26.47 Jean 12.38-12.40
17 kwa sababu alikuwa amehesabiwa pamoja na sisi, akapata sehemu ya huduma hii.
Actes 1.25 Jean 6.70-6.71 Actes 20.24 Actes 21.19 2 Corinthiens 4.1
18 (Basi mtu huyu alinunua konde kwa ijara ya udhalimu; akaanguka kwa kasi akapasuka matumbo yake yote yakatoka.
Matthieu 27.3-27.10 Matthieu 25.15 Job 20.12-20.15 Josué 7.21-7.26 2 Rois 5.20-5.27
19 Ikajulikana na watu wote wakaao Yerusalemu; hata konde lile likaitwa kwa lugha yao Akeldama, maana yake, konde la damu.)
Matthieu 28.15 2 Samuel 2.16 Actes 2.22 Actes 21.40
20 Kwa maana imeandikwa katika chuo cha Zaburi, Kikao chake na kiwe ukiwa, Wala asiwepo mtu mwenye kukaa humo;
Psaumes 69.25 Psaumes 109.8-109.15 Luc 24.44 Luc 20.42 Actes 1.25
21 Basi katika watu waliofuatana nasi wakati wote Bwana Yesu alipokuwa akiingia na kutoka kwetu,
Jean 15.27 Nombres 27.17 Deutéronome 31.2 Luc 10.1-10.2 1 Rois 3.7
22 kuanza tangu ubatizo wa Yohana, hata siku ile alipochukuliwa kwetu kwenda juu, inapasa mmoja wao awe shahidi wa kufufuka kwake pamoja nasi.
Actes 1.2 Actes 4.33 Actes 1.8-1.9 Luc 3.1-3.18 Actes 13.24-13.25
23 Wakaweka wawili, Yusufu, aitwaye Barsaba, aliyekuwa na jina la pili Yusto, na Mathiya.
Actes 15.22 Actes 1.26
24 Kisha wakaomba, wakasema, Wewe, Bwana, ujuaye mioyo ya watu wote, tuonyeshe ni nani uliyemchagua katika hawa wawili,
1 Samuel 16.7 Jérémie 17.10 Actes 15.8 Apocalypse 2.23 Actes 6.6
25 ashike mahali katika huduma hii na utume huu, alioukosa Yuda, aende zake mahali pake mwenyewe.
1 Corinthiens 9.2 Jean 6.70-6.71 Romains 1.5 Jean 17.12 1 Chroniques 10.13-10.14
26 Wakawapigia kura; kura ikamwangukia Mathiya; naye akahesabiwa kuwa pamoja na mitume kumi na mmoja.
Lévitique 16.8 Josué 18.10 1 Chroniques 24.5 1 Samuel 14.41-14.42 Jonas 1.7

Cette Bible est dans le domaine public.