Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Nombres 5.10
Bible en Swahili de l’est


Lois sur la pureté, le vol, la jalousie conjugale

1 Kisha Bwana akanena na Musa, na kumwambia,
2 Waamrishe wana wa Israeli kwamba wamtoe kila mwenye ukoma maragoni, na kila mtu aliye na kisonono, na kila aliye najisi kwa ajili ya wafu;
Lévitique 21.1 Lévitique 13.46 Nombres 12.14 Nombres 9.6-9.10 Nombres 31.19
3 mtawatoa nje wote, waume kwa wake, mtawaweka nje ya marago; ili wasiyatie unajisi marago yao, ambayo mimi naketi katikati yake.
Deutéronome 23.14 Lévitique 26.11-26.12 Nombres 35.34 Tite 3.10 Aggée 2.13-2.14
4 Wana wa Israeli wakafanya vivyo, wakawatoa na kuwaweka nje ya marago; kama Bwana alivyonena na Musa, ndivyo walivyofanya wana wa Israeli.
5 Kisha Bwana akanena na Musa, na kumwambia,
6 Uwaambie wana wa Israeli, Mtu mume au mke atakapofanya dhambi yo yote, ifanywayo na binadamu, kumwasi Bwana, na mtu huyo akawa na hatia;
Lévitique 5.14-6.7 Lévitique 5.1-5.4
7 ndipo watakapoungama dhambi yao waliyoifanya; naye atarudisha kwa hatia yake, kwa utimilifu wake, tena ataongeza juu yake sehemu ya tano, na kumpa huyo aliyemkosa.
Lévitique 5.5 Lévitique 26.40 Josué 7.19 Proverbes 28.13 Luc 19.8
8 Lakini kwamba mtu huyo hana jamaa ya karibu ambaye inampasa kurudishiwa kwa ajili ya hiyo hatia, kile kitakachorudishwa kwa Bwana kwa hiyo hatia kitakuwa cha kuhani, pamoja na kondoo mume wa upatanisho, ambaye kwa huyo utafanywa upatanisho kwa ajili yake.
Lévitique 6.6-6.7 Lévitique 7.7 Lévitique 25.25-25.26
9 Tena kila sadaka ya kuinuliwa, ya vitu vitakatifu vya wana wa Israeli, watakavyosongeza kwa kuhani, itakuwa ni yake.
Exode 29.28 Nombres 18.19 Lévitique 7.6-7.14 Deutéronome 18.3-18.4 Lévitique 6.17-6.18
10 Tena vitu vilivyowekwa wakfu na mtu awaye yote, vitakuwa ni vya kuhani; kitu cho chote mtu atakachompa kuhani, kitakuwa chake.
Lévitique 10.13
11 Kisha Bwana akanena na Musa, na kumwambia,
12 Nena na wana wa israeli, uwaambie, kama mke wa mtu ye yote akikengeuka, na kumkosa mumewe,
Nombres 5.19-5.20 Proverbes 2.16-2.17
13 na mtu mume akalala naye kwa uasherati, na jambo hilo likamfichamania mumewe, likawa jambo lisilojulikana, na huyo mwanamke akawa najisi, wala hapana shahidi aliyeshuhudia juu yake, wala hakufumaniwa;
Lévitique 18.20 Lévitique 20.10 Proverbes 30.20 Proverbes 7.18-7.19
14 kisha mumewe akashikwa na roho ya wivu, akamwonea wivu mkewe, naye akawa najisi huyo mwanamke; au kama akiingiwa na roho ya wivu, akamwonea wivu mkewe, naye hakuwa na unajisi huyo mke;
Proverbes 6.34 Cantique 8.6 Nombres 5.30 1 Corinthiens 10.22 Sophonie 3.8
15 ndipo huyo mume atamchukua mkewe, aende naye kwa kuhani, naye ataleta sadaka yake kwa ajili yake, yaani, sehemu ya kumi ya efa ya unga wa shayiri; asitie mafuta juu yake, wala asitie ubani juu yake; maana, ni sadaka ya unga ya wivu, ni sadaka ya unga ya ukumbusho ya kukumbukia uovu.
Ezéchiel 29.16 1 Rois 17.18 Lévitique 5.11 Hébreux 10.3 Osée 3.2
16 Basi kuhani atamleta mwanamke akaribie, na kumweka mbele za Bwana;
Jérémie 17.10 Lévitique 1.3 Apocalypse 2.22-2.23 Hébreux 13.4
17 kisha kuhani atatwaa maji matakatifu katika chombo cha udongo; kisha kuhani atatwaa katika vumbi lililo pale chini ya maskani, na kulitia katika hayo maji;
Job 2.12 Exode 30.18 Jean 8.8 Nombres 19.2-19.9 Jérémie 17.13
18 kisha kuhani atamweka mwanamke mbele za Bwana, naye atazifungua nywele za kichwani mwa huyo mwanamke, kisha atampa hiyo sadaka ya unga ya ukumbusho mikononi mwake, ambayo ni sadaka ya unga ya wivu, naye kuhani atakuwa na hayo maji ya uchungu yaletayo laana mkononi mwake;
1 Samuel 15.32 Hébreux 4.12-4.13 Lévitique 13.45 Ecclésiaste 7.26 Apocalypse 2.19-2.23
19 tena kuhani atamwapisha huyo mwanamke, naye atamwambia mwanamke, Kwamba hakulala mtu mume pamoja nawe, tena kwamba hukukengeuka kuandama uchafu, uli chini ya mumeo, maji haya ya uchungu yaletayo laana yasikudhuru;
Matthieu 26.63 Romains 7.2 Nombres 5.12
20 lakini kwamba umekengeuka uli chini ya mumeo, na kwamba u hali ya unajisi, na mtu mume amelala nawe, asiyekuwa mumeo;
Nombres 5.12
21 hapo ndipo kuhani atamwapisha mwanamke kwa kiapo cha kuapiza, kisha kuhani atamwambia huyo mwanamke maneno haya, Bwana na akufanye wewe uwe laana na kiapo kati ya watu wako, hapo Bwana akufanyapo paja lako kupooza, na tumbo lako kuvimba;
Néhémie 10.29 Josué 6.26 1 Samuel 14.24 Jérémie 29.22 Matthieu 26.74
22 na maji yaletayo laana yatakuingia matumboni mwako, na kukuvimbisha tumbo, na kukupoozesha paja lako; na mwanamke ataitika, Amina, Amina.
Psaumes 109.18 Deutéronome 27.15-27.26 Jean 3.3 Psaumes 41.13 Job 31.39-31.40
23 Kisha kuhani ataziandika laana hizo ndani ya kitabu, na kuzifuta katika maji ya uchungu;
Exode 17.14 2 Chroniques 34.24 Deutéronome 31.19 Job 31.35 Apocalypse 20.12
24 kisha atamnywesha mwanamke hayo maji ya uchungu yaletayo laana; nayo maji yaletayo laana yataingia ndani yake, nayo yatageuka kuwa uchungu.
Malachie 3.5 Zacharie 5.3-5.4
25 Kisha kuhani ataitwaa hiyo sadaka ya unga ya wivu, kwa kuiondoa mkononi mwa huyo mwanamke, naye ataitikisa sadaka ya unga mbele ya Bwana, na kuisongeza pale madhabahuni;
Lévitique 8.27 Nombres 5.18 Nombres 5.15 Exode 29.24
26 kisha kuhani atatwaa konzi moja ya sadaka ya unga, kuwa ni ukumbusho wake, na kuuteketeza madhabahuni, baadaye atamnywesha mwanamke hayo maji.
Lévitique 2.9 Lévitique 2.2 Lévitique 5.12 Lévitique 6.15
27 Kisha hapo atakapokwisha kumnywesha maji, ndipo itakapokuwa, kama amekuwa hali ya unajisi na kumkosa mumewe, hayo maji yaletayo laana yatamwingia ndani yake, nayo yatakuwa uchungu, na tumbo lake litavimba, na paja lake litapooza; na huyo mwanamke atakuwa laana kati ya watu wake.
Jérémie 29.18 Jérémie 42.18 Zacharie 8.13 Jérémie 44.12 Esaïe 65.15
28 Na kama mwanamke hakuwa na unajisi lakini yu safi; ndipo ataachiliwa, naye atazaa wana.
Michée 7.7-7.10 1 Pierre 1.7 Psaumes 113.9 Nombres 5.19 2 Corinthiens 4.17
29 Hii ndiyo sheria ya wivu, mwanamke, ambaye yu chini ya mumewe, akikengeuka, na kupata unajisi;
Nombres 5.19 Nombres 5.12 Lévitique 11.46 Esaïe 5.7-5.8 Lévitique 13.59
30 au, roho ya wivu ikimwingia mtu mume, naye akamwonea wivu mkewe; ndipo atakapomweka huyo mwanamke mbele za Bwana, na kuhani atatenda juu yake sheria hii yote.
31 Na huyo mume atakuwa hana uovu, na mwanamke atauchukua uovu wake.
Lévitique 20.10 Romains 2.8-2.9 Nombres 9.13 Ezéchiel 18.4 Psaumes 37.6

Cette Bible est dans le domaine public.