Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Ezéchiel 41.11
Bible en Swahili de l’est


Vision de l’intérieur du temple

1 Akanileta mpaka hekaluni, akaipima miimo, upana wake dhiraa sita upande mmoja, na upana wake dhiraa sita upande wa pili, ambao ulikuwa ni upana wa maskani.
Ezéchiel 40.17 Ezéchiel 41.23 Ezéchiel 40.2-40.3 Ezéchiel 40.9 Apocalypse 11.1-11.2
2 Na upana wa maingilio yake ulikuwa dhiraa kumi; na mbavu za maingilio zilikuwa dhiraa tano upande huu, na dhiraa tano upande huu; akaupima urefu wake, dhiraa arobaini, na upana wake, dhiraa ishirini.
1 Rois 6.17 1 Rois 6.2 2 Chroniques 3.3 Jean 10.9 2 Chroniques 29.7
3 Kisha akaingia ndani, akapima kila mwimo wa maingilio, dhiraa mbili; nayo maingilio, dhiraa sita; na upana wa maingilio dhiraa saba.
Ezéchiel 40.16
4 Akaupima urefu wake; dhiraa ishirini, na upana wake, dhiraa ishirini, mbele ya hekalu; akaniambia, Hapa ndipo mahali patakatifu kuliko kila mahali.
1 Rois 6.20 Hébreux 9.3-9.8 2 Chroniques 3.8 Exode 26.33-26.34 Apocalypse 21.16
5 Kisha akaupima ukuta wa nyumba, dhiraa sita; na upana wa kila chumba cha mbavuni, dhiraa nne, kuizunguka nyumba pande zote.
1 Rois 6.5-6.6 Ezéchiel 42.3-42.14 Ezéchiel 41.6-41.9
6 Na vile vyumba vya mbavuni vilikuwa na orofa tatu, moja juu ya mwenziwe; vilikuwa thelathini, safu baada ya safu; navyo viliingia ndani ya ukuta uliokuwa wa nyumba, kwa vile vyumba vya mbavuni pande zote vipate kushikamana nao, wala visishikamane na ukuta wa nyumba.
1 Rois 6.10 1 Pierre 1.5 Ezéchiel 40.17 1 Rois 6.5-6.6
7 Na vile vyumba vya mbavuni vilizidi kuwa vipana, kwa kadiri vilivyoizunguka nyumba juu kwa juu; maana kule kuzunguka kwake kulikwenda juu kwa juu, kuizunguka nyumba; basi upana wa nyumba ulikuwa ule ule hata juu; basi hupanda juu toka chumba cha chini hata chumba cha juu, kwa njia ya kile chumba cha katikati.
1 Rois 6.8 Hébreux 6.1 Matthieu 13.32
8 Tena, nikaona ya kwamba nyumba ile ilikuwa na sakafu ya mawe, iliyoinuliwa pande zote; nayo misingi ya vyumba vya mbavuni ilikuwa mwanzi mzima wa dhiraa sita.
Ezéchiel 40.5 Apocalypse 21.16
9 Unene wa ukuta uliokuwa wa vile vyumba vya mbavuni, upande wa nje, ulikuwa dhiraa tano; nayo nafasi iliyobaki ilikuwa dhiraa tano; na kati ya vyumba vya mbavuni vya nyumba,
Ezéchiel 41.11 Ezéchiel 42.1 Ezéchiel 42.4
10 na vyumba vya walinzi, upana wa dhiraa ishirini, kuizunguka nyumba pande zote.
Ezéchiel 40.17
11 Na milango ya vile vyumba vya mbavuni iliielekea nafasi ile iliyobaki, mlango mmoja ulielekea upande wa kaskazini, na mlango mmoja upande wa kusini; na upana wa nafasi iliyobaki ulikuwa dhiraa tano pande zote.
Ezéchiel 41.9 Ezéchiel 42.4
12 Nalo jengo lililokabili mahali palipotengeka upande wa magharibi, upana wake dhiraa sabini; na ukuta wa lile jengo, unene wake dhiraa tano pande zote, na urefu wake dhiraa tisini.
Ezéchiel 42.13 Ezéchiel 42.10 Ezéchiel 42.1 Ezéchiel 41.13-41.15 Apocalypse 21.27
13 Basi akaipima nyumba, urefu wake dhiraa mia; na mahali pale palipotengeka na jengo lile, pamoja na kuta zake, urefu wake dhiraa mia;
Ezéchiel 40.47
14 tena upana wa uso wa nyumba, na wa mahali palipotengeka upande wa mashariki, dhiraa mia.
15 Akaupima urefu wa jengo lile lililokabili mahali palipotengeka, palipokuwa nyuma yake, na baraza zake upande huu na upande huu, dhiraa mia; na hekalu la ndani, na kumbi za ua;
Ezéchiel 42.3 Ezéchiel 42.1 Ezéchiel 41.12 Ezéchiel 42.15 Ezéchiel 42.5
16 na vizingiti, na madirisha yaliyofungwa, na baraza za pande zote za orofa zile tatu, zilizokikabili kizingiti, zilitiwa mabamba ya mti pande zote; na toka chini hata madirishani; (nayo madirisha yamefunikwa);
1 Rois 6.4 Ezéchiel 40.25 Ezéchiel 40.16 1 Rois 6.15 Ezéchiel 42.3
17 na mpaka juu ya mlango hata nyumba ya ndani, na nje, na juu ya kuta zote pande zote, katika nyumba ya ndani, na ya nje,
Ezéchiel 42.15
18 kulipambwa kwa makerubi na mitende; mtende mmoja kati ya kerubi na kerubi, na kila kerubi lilikuwa na nyuso mbili;
1 Rois 7.36 Ezéchiel 40.16 Ezéchiel 10.21 2 Chroniques 3.7 Ezéchiel 40.22
19 basi palikuwa na uso wa mwanadamu kuelekea mtende mmoja, na uso wa mwana-simba kuelekea mtende wa pili; ndivyo vilivyofanyika katika nyumba nzima pande zote.
Ezéchiel 10.14 Ezéchiel 1.10
20 Toka chini hata juu ya mlango makerubi yamefanyika, na mitende, na vivi hivi ukuta wa hekalu.
Ezéchiel 41.18
21 Na hilo hekalu, miimo ya milango yake ilikuwa ya miraba; na mbele ya patakatifu kuonekana kwake palionekana kama hapo kwanza.
Ezéchiel 41.1 Ezéchiel 40.14 1 Rois 6.33
22 Madhabahu ilikuwa ni ya miti, kimo chake dhiraa tatu, na urefu wake dhiraa mbili; na pembe zake, na msingi wake, na kuta zake zilikuwa za miti; akaniambia, Hii ndiyo meza iliyo mbele za Bwana.
Ezéchiel 44.16 Malachie 1.7 Malachie 1.12 Ezéchiel 23.41 Exode 30.1-30.3
23 Nalo hekalu na patakatifu palikuwa na milango miwili.
1 Rois 6.31-6.35 Ezéchiel 41.1 2 Chroniques 4.22
24 Na milango hiyo, kila mmoja ulikuwa na mbao mbili; mbao mbili zigeukazo; mbao mbili za mlango mmoja, na mbao mbili za mlango wa pili.
1 Rois 6.34 Ezéchiel 40.48
25 Na milango ya hekalu ilifanyiziwa makerubi na mitende vile vile, kama zile kuta zilivyofanyiziwa; tena palikuwa na boriti nene juu ya uso wa ukumbi, nje.
Ezéchiel 41.18
26 Tena palikuwa na madirisha yaliyofungwa, na mitende, upande huu na upande huu, katika pande za ukumbi; ndiyo habari ya vyumba vya mbavuni vya nyumba hiyo, na vya boriti zile nene.
Ezéchiel 41.16 Ezéchiel 40.16 Ezéchiel 41.5

Cette Bible est dans le domaine public.