Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Ezéchiel 33.8
Bible en Swahili de l’est


Perspectives de restauration

Le rôle de sentinelle du prophète

1 Neno la Bwana likanijia, kusema,
2 Mwanadamu, sema na wana wa watu wako, uwaambie, Hapo nitakapoleta upanga juu ya nchi, watu wa nchi hiyo wakimtwaa mtu mmoja miongoni mwao, na kumweka awe mlinzi wao;
Ezéchiel 3.11 Ezéchiel 33.30 Ezéchiel 33.17 Jérémie 12.12 Ezéchiel 14.17
3 ikiwa, aonapo upanga unakuja juu ya nchi hiyo, apiga tarumbeta na kuwaonya watu;
Osée 8.1 Néhémie 4.20 Esaïe 58.1 Néhémie 4.18 Joël 2.1
4 basi mtu awaye yote aisikiaye sauti ya tarumbeta, wala haonywi, upanga ukija na kumwondoa, damu yake itakuwa juu ya kichwa chake mwenyewe.
Ezéchiel 18.13 2 Chroniques 25.16 Actes 18.6 Jérémie 6.17 Ezéchiel 33.9
5 Aliisikia sauti ya tarumbeta, wala hakuonywa; damu yake itakuwa juu yake; lakini kama angalionywa, angalijiokoa roho yake.
Exode 9.19-9.21 Hébreux 11.7 Jean 8.39 Psaumes 95.7 Actes 2.37-2.41
6 Bali mlinzi akiona upanga unakuja, kama hapigi tarumbeta, wala watu hawakuonywa, na upanga ukaja ukamwondoa mtu awaye yote miongoni mwao; ameondolewa huyo katika uovu wake, lakini damu yake nitaitaka mkononi mwa mlinzi huyo.
Ezéchiel 3.18-3.20 2 Samuel 4.11 Ezéchiel 33.8-33.9 Ezéchiel 18.20 Ezéchiel 18.24
7 Basi wewe, mwanadamu, nimekuweka kuwa mlinzi kwa nyumba ya Israeli; basi ulisikie neno hili kinywani mwangu, ukawape maonyo yangu.
Jérémie 26.2 Actes 5.20 Jérémie 1.17 Ezéchiel 3.17-3.21 Ezéchiel 2.7-2.8
8 Nimwambiapo mtu mbaya, Ewe mtu mbaya, hakika utakufa, nawe husemi neno la kumwonya mtu huyo, aiache njia yake, mtu mbaya huyo atakufa katika uovu wake, lakini damu yake nitaitaka mkononi mwako.
Ezéchiel 18.4 Ezéchiel 33.14 Ezéchiel 33.6 Ezéchiel 18.18 Esaïe 3.11
9 Walakini ukimwonya mtu mbaya kwa sababu ya njia yake, kusudi aiache; wala yeye asiiache; atakufa huyo katika uovu wake, lakini wewe umejiokoa roho yako.
Ezéchiel 3.19 Actes 13.40 Actes 13.46 Ezéchiel 3.21 Actes 20.26
10 Na wewe, mwanadamu, sema na nyumba ya Israeli; Ninyi mwasema hivi, kwamba, Makosa yetu na dhambi zetu ni juu yetu, nasi tumedhoofika katika dhambi hizo; basi tungewezaje kuwa hai?
Ezéchiel 24.23 Lévitique 26.39 Ezéchiel 37.11 Esaïe 49.14 Ezéchiel 4.17
11 Waambie, Kama mimi niishivyo, asema Bwana MUNGU, sikufurahii kufa kwake mtu mwovu; bali aghairi mtu mwovu, na kuiacha njia yake mbaya, akaishi. Ghairini, ghairini, mkaache njia zenu mbaya; mbona mnataka kufa, Enyi nyumba ya Israeli?
Ezéchiel 18.23 1 Timothée 2.4 2 Pierre 3.9 Esaïe 55.6-55.7 Ezéchiel 18.30-18.32
12 Na wewe, mwanadamu, waambie wana wa watu wako, Haki yake mwenye haki haitamwokoa, katika siku ya kukosa kwake; na kwa habari ya uovu wake mtu mwovu, hataanguka kwa ajili ya uovu huo, siku ile atakapoghairi na kuuacha uovu wake; wala yeye aliye mwenye haki hataweza kuishi kwa haki yake, siku ile atakapotenda dhambi.
2 Chroniques 7.14 Romains 3.25 Ezéchiel 18.21 Ezéchiel 33.18-33.19 Ezéchiel 33.2
13 Nimwambiapo mwenye haki, ya kwamba hakika ataishi; kama akiitumainia haki yake, akatenda uovu, basi katika matendo yake ya haki, hata mojawapo halitakumbukwa; bali katika uovu wake alioutenda, atakufa katika uovu huo.
Ezéchiel 18.24 Hébreux 10.38 Ezéchiel 3.20 Luc 18.9-18.14 Philippiens 3.9
14 Tena, nimwambiapo mtu mwovu, Hakika utakufa; kama akighairi, na kuiacha dhambi yake, na kutenda yaliyo halali na haki;
Ezéchiel 18.27 Esaïe 55.7 Osée 14.1 Ezéchiel 33.8 Jérémie 18.7-18.8
15 kama mtu mwovu akirudisha rehani, na kumrudishia mtu mali yake aliyomnyang’anya, akizifuata sheria za uzima, asitende uovu wo wote; hakika ataishi, hatakufa.
Ezéchiel 20.11 Luc 19.8 Exode 22.1-22.4 Ezéchiel 18.7 Lévitique 6.2-6.5
16 Katika dhambi zake zote alizozitenda, hata mojawapo haitakumbukwa juu yake; ametenda yaliyo halali na haki; hakika ataishi.
Ezéchiel 18.22 Esaïe 43.25 Esaïe 1.18 Michée 7.18-7.19 Romains 5.21
17 Walakini wana wa watu wako husema, Njia ya Bwana si sawa; lakini watu hao, njia yao si sawa.
Ezéchiel 18.25 Ezéchiel 18.29 Job 35.2 Luc 19.21-19.22 Ezéchiel 33.20
18 Mwenye haki ageukapo, na kuiacha haki yake, na kutenda maovu, atakufa katika maovu hayo.
Ezéchiel 33.12-33.13 Ezéchiel 18.26-18.27 2 Pierre 2.20-2.22 Hébreux 10.38 Ezéchiel 3.20
19 Na mtu mbaya ageukapo, na kuuacha ubaya wake, na kutenda yaliyo halali na haki, ataishi kwa matendo hayo.
Ezéchiel 33.14 Ezéchiel 18.27-18.28
20 Lakini ninyi husema, Njia ya Bwana si sawa. Ee nyumba ya Israeli, nitawahukumu ninyi; kila mtu kwa kadiri ya njia zake.
Ezéchiel 18.25 Jean 5.29 Proverbes 19.3 Apocalypse 20.12-20.15 Apocalypse 22.12

Raisons de la prise de Jérusalem

21 Ikawa, katika mwaka wa kumi na mbili wa kuhamishwa kwetu, mwezi wa kumi, siku ya tano ya mwezi, mtu mmoja aliyekuwa ametoroka toka Yerusalemu akanijia, akisema, Mji umepigwa.
Ezéchiel 1.2 2 Rois 25.10 Jérémie 39.1-39.8 Ezéchiel 24.26-24.27 Ezéchiel 40.1
22 Basi mkono wa Bwana umekuwa juu yangu wakati wa jioni, kabla hajafika yeye aliyetoroka; naye alikuwa amenifumbua kinywa changu, hata aliponijia wakati wa asubuhi; na kinywa changu kilikuwa wazi, wala sikuwa bubu tena.
Ezéchiel 1.3 Ezéchiel 3.26-3.27 Ezéchiel 24.26-24.27 Ezéchiel 37.1 Ezéchiel 40.1
23 Neno la Bwana likanijia, kusema,
24 Mwanadamu, watu wale wakaao mahali palipoharibika katika nchi ya Israeli husema ya kwamba, Ibrahimu alikuwa mmoja, akairithi nchi hii; lakini sisi tu watu wengi; tumepewa nchi hii iwe urithi wetu.
Esaïe 51.2 Ezéchiel 33.27 Actes 7.5 Ezéchiel 36.4 Jérémie 40.7
25 Basi, waambie, Bwana MUNGU asema hivi; Mnakula nyama pamoja na damu yake, na kuviinulia vinyago vyenu macho yenu, na kumwaga damu; je, mtaimiliki nchi hii?
Deutéronome 12.16 Genèse 9.4 Jérémie 7.9-7.10 Ezéchiel 18.6 Ezéchiel 22.27
26 Mnategemea upanga wenu, mnatenda machukizo, mnanajisi kila mtu mke wa jirani yake; je! Mtaimiliki nchi hii?
Michée 2.1-2.2 Sophonie 3.3 Genèse 27.40 Psaumes 94.20-94.21 Psaumes 50.16-50.20
27 Hivi ndivyo utakavyowaambia, Bwana MUNGU asema hivi; Kama mimi niishivyo, hakika watu wale wakaao mahali palipoharibika wataanguka kwa upanga, naye mtu aliye katika uwanda, nitamtoa na kuwapa wanyama wakali, ili aliwe; na hao walio ndani ya ngome na mapango watakufa kwa tauni.
Jérémie 42.22 1 Samuel 13.6 Ezéchiel 39.4 Ezéchiel 6.11-6.14 1 Samuel 23.14
28 Nami nitaifanya nchi kuwa ukiwa na ajabu, na kiburi cha uwezo wake kitakoma; nayo milima ya Israeli itakuwa ukiwa, asipite mtu.
Ezéchiel 7.24 Jérémie 44.22 Jérémie 44.6 Ezéchiel 6.14 Jérémie 44.2
29 Ndipo watakapojua ya kuwa mimi ndimi Bwana, nitakapoifanya nchi kuwa ukiwa na ajabu, kwa sababu ya machukizo yao yote waliyoyatenda.
Ezéchiel 6.7 Exode 14.18 2 Rois 17.9-17.18 Jérémie 5.1-5.9 2 Chroniques 36.14-36.17
30 Nawe, mwanadamu, wana wa watu wako husimulia habari zako karibu na kuta, na ndani ya milango ya nyumba zao, na kuambiana, kila mtu na ndugu yake, wakisema, Haya! Twende tukasikie ni neno gani hilo litokalo kwa Bwana.
Esaïe 58.2 Esaïe 29.13 Jérémie 18.18 Jérémie 23.35 Jérémie 42.20
31 Nao huja kwako kama watu wajavyo, nao hukaa mbele yako kama watu wangu, nao husikia maneno yako, wasiyatende; maana kwa vinywa vyao hujifanya kuwa wenye upendo mwingi, lakini mioyo yao inatafuta faida yao.
Matthieu 13.22 Esaïe 29.13 Psaumes 78.36-78.37 Luc 11.28 Jacques 1.22-1.24
32 Na tazama, wewe umekuwa kwao kama wimbo mzuri sana, wa mtu mwenye sauti ipendezayo, awezaye kupiga kinanda vizuri; maana, wasikia maneno yako, lakini hawayatendi.
Marc 6.20 Jean 5.35 Marc 4.16-4.17
33 Na hayo yatakapokuwapo (tazama, yanakuja), ndipo watakapojua ya kuwa nabii amekuwapo kati yao.
Jérémie 28.9 Ezéchiel 2.5 Ezéchiel 33.29 2 Rois 5.8 Luc 10.11

Cette Bible est dans le domaine public.