Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Ezéchiel 26.6
Bible en Swahili de l’est


Sur Tyr

1 Ikawa katika mwaka wa kumi na mmoja, siku ya kwanza ya mwezi, neno la Bwana likanijia, kusema,
Ezéchiel 20.1 Jérémie 39.2 Ezéchiel 1.2 Ezéchiel 8.1
2 Mwanadamu, Kwa sababu Tiro amesema juu ya Yerusalemu, Aha! Yeye amevunjika aliyekuwa lango la kabila za watu; amenigeukia; nitajazwa kwa kuwa sasa ameharibika;
Esaïe 23.1-23.18 Jérémie 25.22 Ezéchiel 36.2 Joël 3.4 Psaumes 83.2-83.4
3 basi Bwana MUNGU asema hivi; Tazama, mimi ni juu yako, Ee Tiro, nami nitaleta mataifa mengi kupigana nawe, kama bahari iinuavyo mawimbi yake.
Jérémie 51.42 Esaïe 5.30 Michée 4.11 Jérémie 50.42 Ezéchiel 27.32-27.34
4 Nao wataziharibu kuta za Tiro, na kuibomoa minara yake; tena nitakwangua hata mavumbi yake yamtoke, na kumfanya kuwa jabali tupu.
Esaïe 23.11 Amos 1.10 Ezéchiel 26.9 Zacharie 9.3 Jérémie 5.10
5 Naye atakuwa mahali pa kutandazia nyavu za wavuvi kati ya bahari; maana mimi nimenena neno hili, asema Bwana MUNGU; naye atakuwa mateka ya mataifa.
Ezéchiel 29.19 Ezéchiel 25.7 Ezéchiel 27.32 Ezéchiel 47.10 Ezéchiel 26.14
6 Na binti zake walio katika mashamba watauawa kwa upanga; nao watajua ya kuwa mimi ndimi Bwana.
Ezéchiel 16.46 Ezéchiel 26.8 Ezéchiel 16.48 Ezéchiel 25.17 Ezéchiel 25.11
7 Maana Bwana MUNGU asema hivi; Tazama, nitamleta Nebukadreza, mfalme wa Babeli, mfalme wa wafalme, juu ya Tiro toka kaskazini, pamoja na farasi, na magari ya vita, na wapanda farasi, na jeshi, na watu wengi.
Daniel 2.37 Esdras 7.12 Nahum 2.3-2.4 Ezéchiel 23.24 Daniel 2.47
8 Atawaua binti zako kwa upanga katika mashamba; naye atafanya ngome juu yako, na kufanya maboma juu yako, na kuiinua ngao juu yako.
Ezéchiel 21.22 Jérémie 52.4 Jérémie 32.24 Jérémie 6.6 2 Samuel 20.15
9 Naye ataweka vyombo vyake vya kubomolea mbele za kuta zako, na kwa mashoka yake ataiangusha chini minara yako.
2 Chroniques 26.15
10 Kwa sababu wingi wa farasi zake, mavumbi yao yatakufunika; kuta zako zitatetemeka kwa sababu ya mshindo wa wapanda farasi, na wa magurudumu, na wa magari ya vita, atakapoingia katika malango yako, kama watu waingiavyo katika mji uliobomolewa mahali.
Ezéchiel 26.15 Jérémie 47.3 Ezéchiel 27.28 Ezéchiel 26.7 Josué 6.5
11 Kwa kwato za farasi zake atazikanyaga njia zako zote; atawaua watu wako kwa upanga, na minara ya nguvu zako itashuka hata nchi.
Esaïe 5.28 Esaïe 26.5 Habakuk 1.8 Jérémie 43.13 Jérémie 51.27
12 Nao wataufanya utajiri wako kuwa mateka, na bidhaa yako kuwa mawindo; nao watazibomoa kuta zako, na kuziharibu nyumba zako zipendezazo; nao wataweka mawe yako, na miti yako, na mavumbi yako, kati ya maji.
Esaïe 23.8 2 Chroniques 32.27 Amos 5.11 Nahum 2.9 Zacharie 9.3-9.4
13 Nami nitaikomesha sauti ya nyimbo zako, wala sauti ya vinubi vyako haitasikiwa tena.
Jérémie 7.34 Esaïe 23.16 Esaïe 24.8-24.9 Esaïe 14.11 Jérémie 25.10
14 Nami nitakufanya kuwa jabali tupu; utakuwa mahali pa kutandazia nyavu za wavuvi; hutajengwa tena; maana mimi, Bwana, nimenena neno hili, asema Bwana MUNGU.
Job 12.14 Malachie 1.4 Nombres 23.19 Deutéronome 13.16 Ezéchiel 26.4-26.5
15 Bwana MUNGU amwambia Tiro neno hili; Je! Visiwa havitatikisika kwa mshindo wa kuanguka kwako, watakapougua waliojeruhiwa, yatakapofanyika machinjo kati yako.
Ezéchiel 27.35 Jérémie 49.21 Ezéchiel 26.18 Ezéchiel 31.16 Ezéchiel 32.10
16 Ndipo wakuu wote wa bahari watashuka kutoka viti vyao vya enzi, na kuweka upande mavazi yao, na kuvua nguo zao zilizotiwa taraza; watajivika matetemeko; wataketi na kutetemeka kila dakika, na kukustaajabia,
Ezéchiel 32.10 Osée 11.10 Jonas 3.6 Job 8.22 Esaïe 3.26
17 Nao watakufanyia maombolezo, na kukuambia, Imekuwaje wewe kuharibika, wewe uliyekaliwa na wana-maji, mji wenye sifa, uliyekuwa na nguvu katika bahari, mji huo, na hao waliokaa ndani yake, waliowatia hofu wote waliokaa ndani yake!
Esaïe 14.12 Ezéchiel 19.1 2 Samuel 1.25-1.27 Apocalypse 18.16-18.19 Apocalypse 18.9-18.10
18 Sasa visiwa vitatetemeka katika siku ya kuanguka kwako; naam, visiwa vilivyo katika bahari vitafadhaika, kwa sababu ya kuondoka kwako.
Ezéchiel 26.15 Esaïe 23.5-23.7 Ezéchiel 27.35 Esaïe 41.5 Ezéchiel 27.28-27.30
19 Maana Bwana MUNGU asema hivi; Nitakapokufanya kuwa mji wa ukiwa, kama miji isiyokaliwa na watu; nitakapoleta vilindi vya bahari juu yako, na maji makuu yatakapokufunika;
Esaïe 8.7-8.8 Ezéchiel 26.3 Apocalypse 17.15 Daniel 11.40 Daniel 9.26
20 ndipo nitakapokushusha pamoja nao washukao shimoni, uende kwa watu wa kale; nami nitakukalisha pande za chini za nchi; mahali palipokuwa ukiwa tangu zamani, pamoja nao washukao shimoni; ili usikaliwe na watu, wala usiweke utukufu wako katika nchi yao walio hai.
Psaumes 27.13 Zacharie 2.8 Ezéchiel 34.1-34.31 Amos 9.2 Ezéchiel 39.7
21 Nitakufanya kuwa kitu cha kutisha, wala hutakuwako tena; ujapotafutwa, lakini hutaonekana tena kabisa, asema Bwana MUNGU.
Ezéchiel 27.36 Apocalypse 18.21 Ezéchiel 28.19 Psaumes 37.36 Ezéchiel 26.14-26.16

Cette Bible est dans le domaine public.