Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Ezéchiel 21.12
Bible en Swahili de l’est


Jugement d’Israël et des Ammonites

1 Neno la Bwana likanijia, kusema,
2 Mwanadamu, uelekeze uso wako kuelekea Yerusalemu, ukadondoze neno lako upande wa mahali patakatifu, ukatabiri juu ya nchi ya Israeli;
Ezéchiel 20.46 Ezéchiel 4.7 Ezéchiel 28.21 Ezéchiel 25.2 Jérémie 26.11-26.12
3 uiambie nchi ya Israeli, Bwana asema hivi; Tazama, mimi ni juu yako, nami nitautoa upanga wangu alani, nami nitamkatilia mbali nawe mtu mwenye haki na mtu mbaya.
Job 9.22 Jérémie 21.13 Ezéchiel 21.19 Nahum 2.13 Ezéchiel 5.8
4 Basi, kwa kuwa nitamkatilia mbali nawe mtu mwenye haki na mtu mbaya, upanga wangu utatoka alani mwake, uwe juu ya watu wote wenye mwili toka kusini hata kaskazini,
Ezéchiel 20.47 Ezéchiel 7.2 Ezéchiel 6.11-6.14
5 na watu wote wenye mwili watajua ya kuwa mimi, Bwana, nimeufuta upanga wangu alani mwake; hautarudi tena.
Ezéchiel 21.30 Nahum 1.9 1 Samuel 3.12 Ezéchiel 20.48 Jérémie 23.20
6 Ugua, basi, Ee mwanadamu; kwa kuvunjika kwake viuno vyako, na kwa uchungu, utaugua mbele ya macho yao.
Esaïe 22.4 Ezéchiel 6.11 Esaïe 16.11 Ezéchiel 12.3-12.5 Jérémie 19.10
7 Na itakuwa, wakuambiapo, Mbona unaugua? Ndipo utakaposema, Kwa sababu ya habari hizo, maana linakuja; na kila moyo utayeyuka, na mikono yote itakuwa dhaifu, na kila roho itazimia, na magoti yote yatalegea kama maji; tazama, linakuja, nalo litatendeka, asema Bwana MUNGU.
Ezéchiel 7.17 Nahum 2.10 Esaïe 13.7 Ezéchiel 7.26 Jérémie 50.43
8 Neno la Bwana likanijia, kusema,
9 Mwanadamu, tabiri, useme, Bwana asema hivi; Nena, Upanga, upanga, umenolewa na kusuguliwa,
Ezéchiel 21.3 Deutéronome 32.41-32.42 Amos 9.4 Esaïe 27.1 Esaïe 66.16
10 umenolewa ili kufanya machinjo; umesuguliwa ili uwe kama umeme; basi je! Tufanye furaha? Upanga unadharau fimbo ya mwanangu, kama unavyodharau kila mti.
Ezéchiel 20.47 Psaumes 110.5-110.6 Esaïe 5.12-5.14 Esaïe 22.12-22.14 Ezéchiel 19.11-19.14
11 Nao umenolewa usuguliwe, upate kushikwa mkononi; upanga umenolewa, naam, umesuguliwa, ili kutiwa katika mkono wake auaye.
Ezéchiel 21.19 Jérémie 25.33 Jérémie 51.20-51.23 Jérémie 25.9
12 Piga kelele, utoe sauti ya uchungu, Ee mwanadamu, kwa maana upanga u juu ya watu wangu, u juu ya wakuu wote wa Israeli; wametolewa wauawe na upanga pamoja na watu wangu, basi, jipige pajani.
Ezéchiel 21.6 Joël 1.13 Ezéchiel 9.8 Ezéchiel 30.2 Michée 1.8
13 Kwa maana kuna kujaribiwa; itakuwaje, basi, ikiwa upanga unaidharau hiyo fimbo? Haitakuwapo tena; asema Bwana MUNGU.
Ezéchiel 21.10 2 Corinthiens 8.2 Job 9.23 Ezéchiel 21.25
14 Basi, wewe mwanadamu, tabiri, ukapige makofi; upanga huo na uongezwe mara mbili, hata mara tatu; upanga wao waliotiwa jeraha kiasi cha kuwaua; ni upanga wa mkuu aliyetiwa jeraha kiasi cha kumwua; uwazungukao pande zote.
Nombres 24.10 2 Rois 24.1 Ezéchiel 6.11 Lévitique 26.24 2 Rois 24.10-24.16
15 Nimeweka ncha ya upanga huo juu ya malango yao yote, ili mioyo yao iyeyuke, yakaongezeke makwazo yao; aha! Umefanywa kuwa kama umeme, umenolewa, ili uchinje.
Ezéchiel 21.7 Jérémie 17.27 Ezéchiel 21.10 Ezéchiel 15.7 Ezéchiel 21.28
16 Jiweke tayari, enenda upande wa kuume; jipange, enenda upande wa kushoto; mahali po pote utakapouelekeza uso wako.
Ezéchiel 21.20 Ezéchiel 14.17 Ezéchiel 21.4 Ezéchiel 16.46 Genèse 13.9
17 Mimi nami nitapiga makofi, mimi nami nitashibisha ghadhabu yangu; mimi, Bwana, nimenena neno hili.
Ezéchiel 5.13 Ezéchiel 21.14 Ezéchiel 22.13 Esaïe 1.24 Deutéronome 28.63
18 Neno la Bwana likanijia tena, kusema,
19 Tena, mwanadamu, ujiwekee njia mbili, upanga wa mfalme wa Babeli upate kuja; hizo mbili zitatoka katika nchi moja; ukaandike mahali, upaandike penye kichwa cha njia iendayo mjini.
Jérémie 1.10 Ezéchiel 4.1-4.3 Ezéchiel 5.1-5.17
20 Utaagiza njia, upanga upate kufikilia Raba wa wana wa Amoni, na kufikilia Yuda katika Yerusalemu, wenye maboma.
Amos 1.14 Jérémie 49.2 Deutéronome 3.11 Ezéchiel 25.5 Psaumes 48.12-48.13
21 Maana mfalme wa Babeli alisimama penye njia panda, penye kichwa cha njia hizo mbili, ili atumie uganga; aliitikisa mishale huko na huko, akaziuliza terafi, akayatazama maini.
Genèse 31.19 Proverbes 16.33 Genèse 31.30 Juges 18.20 Juges 17.5
22 Katika mkono wake wa kuume alikuwa na kura ya Yerusalemu, kuviweka vyombo vya kubomolea, kufumbua kinywa katika machinjo, kuiinua sauti kwa kupiga kelele sana, kuweka vyombo vya kubomolea juu ya malango, kufanya maboma, na kujenga ngome.
Ezéchiel 4.2 Ezéchiel 26.9 Jérémie 52.4 Josué 6.20 Job 39.25
23 Jambo hili litakuwa kwao kama uganga wa ubatili, mbele ya macho yao waliowaapia viapo lakini ataufanya uovu ukumbukwe, ili kwamba wakamatwe.
Nombres 5.15 Ezéchiel 21.24 Ezéchiel 29.16 Jérémie 52.3-52.11 1 Rois 17.18
24 Basi Bwana MUNGU asema hivi; Kwa kuwa mmeufanya uovu wenu ukumbukwe, kwa maana makosa yenu yamefunuliwa, hata dhambi zenu zikaonekana kwa matendo yenu; kwa sababu mmekumbukwa, mtakamatwa kwa mkono.
Amos 9.1-9.3 Ezéchiel 24.7 Jérémie 5.27-5.28 Ezéchiel 23.5-23.21 Michée 3.10-3.12
25 Na wewe, Ewe mtu mwovu, uliyetiwa jeraha kiasi cha kukuua, mkuu wa Israeli, ambaye siku yako imekuja, katika wakati wa uovu wa mwisho;
Ezéchiel 35.5 Ezéchiel 21.29 Ezéchiel 17.19 Jérémie 52.2 2 Chroniques 36.13
26 Bwana MUNGU asema hivi; Kiondoe kilemba, ivue taji; haya hayatakuwa tena kama yalivyo; kikweze kilicho chini, kakishushe kilichoinuka.
Ezéchiel 17.24 Psaumes 75.7 Jérémie 13.18 Jérémie 52.31-52.34 Ezéchiel 16.12
27 Nitakipindua, nitakipindua, nitakipindua; hiki nacho hakitakuwa tena, hata atakapokuja yeye ambaye ni haki yake; nami nitampa.
Psaumes 2.6 Michée 5.2 Aggée 2.21-2.22 Jérémie 23.5-23.6 Genèse 49.10
28 Nawe, mwanadamu, tabiri useme, Bwana MUNGU asema hivi, katika habari za wana wa Amoni, na katika habari za aibu yao; Nena, Upanga; upanga umefutwa; umesuguliwa, ili kuua, ili kuufanya uue sana, upate kuwa kama umeme;
Ezéchiel 21.9-21.10 Ezéchiel 21.20 Sophonie 2.8-2.10 Ezéchiel 25.2-25.7 Jérémie 12.12
29 wakati wakuoneapo ubatili, wakati wakufanyiao uganga wa uongo, ili kukuweka juu ya shingo zao waliotiwa jeraha kiasi cha kuwaua, ambao siku yao imekuja, katika wakati wa uovu wa mwisho.
Ezéchiel 21.25 Ezéchiel 22.28 Jérémie 27.9 Ezéchiel 35.5 Psaumes 37.13
30 Uurudishe alani mwake. Mahali pale ulipoumbwa, katika nchi uliyozaliwa; nitakuhukumu wewe.
Jérémie 47.6-47.7 Ezéchiel 16.38 Ezéchiel 28.15 Ezéchiel 16.3-16.4 Genèse 15.14
31 Nami nitamwaga ghadhabu yangu juu yako; nitakupulizia moto wa hasira yangu; nami nitakutia katika mikono ya watu walio kama hayawani, wajuao sana kuangamiza.
Ezéchiel 7.8 Jérémie 6.22-6.23 Esaïe 30.33 Ezéchiel 14.19 Psaumes 18.15
32 Utakuwa kuni za kutiwa motoni; damu yako itakuwa katikati ya nchi; hutakumbukwa tena; maana mimi, Bwana, nimenena neno hili.
Ezéchiel 25.10 Malachie 4.1 Ezéchiel 20.47-20.48 Matthieu 3.10 Sophonie 2.9

Cette Bible est dans le domaine public.