Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Ezéchiel 17.14
Bible en Swahili de l’est


Parabole des deux aigles

1 Neno la Bwana likanijia, kusema,
2 Mwanadamu, tega kitendawili, ukawaambie nyumba ya Israeli mithali;
Ezéchiel 20.49 Matthieu 13.35 Ezéchiel 24.3 Osée 12.10 1 Corinthiens 13.12
3 useme, Bwana MUNGU asema hivi; Tai mkubwa, mwenye mabawa makubwa na manyoya marefu katika mabawa, mwenye kujaa manyoya, yaliyo ya rangi mbalimbali, alifika Lebanoni, akakitwaa kilele cha mwerezi;
Jérémie 48.40 Osée 8.1 Ezéchiel 17.7 Daniel 4.22 Ezéchiel 17.12-17.21
4 akakikata kitawi kilicho juu katika vitawi vyake, akakichukua mpaka nchi ya biashara, akakiweka katika mji wa wachuuzi.
Esaïe 43.14 Apocalypse 18.11-18.19 Apocalypse 18.3 Esaïe 47.15 Jérémie 51.13
5 Akatwaa tena mbegu katika mbegu za nchi hiyo, akaipanda katika udongo uzaao sana, akaiweka kando ya maji mengi; aliipandikiza kama mti ukuao karibu na mto.
Esaïe 44.4 Deutéronome 8.7-8.9 Ezéchiel 19.11-19.12 2 Rois 24.17 Ezéchiel 17.13
6 Ikakua, ikawa mzabibu wenye kuenea sana, wa kimo kifupi, ambao matawi yake yalimgeukia, na mizizi yake ilikuwa chini yake; basi ukawa mzabibu, ukatoa matawi, ukachipuza vichipuko.
Ezéchiel 17.14 Proverbes 16.18-16.19
7 Kulikuwa na tai mwingine mkubwa, mwenye mabawa makubwa na manyoya mengi; na tazama, mzabibu huo ukapinda mizizi yake imwelekee yeye, ukachipuza matawi yake yamwelekee yeye, toka matuta yake ulipopandwa; ili yeye apate kuunywesha.
Ezéchiel 17.15 Ezéchiel 31.4 Jérémie 37.5-37.7 2 Rois 24.20 2 Chroniques 26.13
8 Ulikuwa umepandwa katika udongo mwema, kando ya maji mengi, upate kutoa matawi, na kuzaa matunda, uwe mzabibu mzuri.
Ezéchiel 17.5-17.6
9 Basi nena wewe, Bwana MUNGU asema hivi; Je! Huo utafanikiwa? Yeye hataing’oa mizizi yake na kuyakata matunda yake, ili ukauke? Kwamba majani mabichi yake yote yachipukayo yakauke, hata ikiwa hana nguvu nyingi, wala watu wengi wa kuung’oa na mizizi yake?
Jérémie 52.7-52.11 Jérémie 24.8-24.10 Esaïe 8.9-8.10 Jérémie 37.10 Jérémie 29.4-29.7
10 Naam, tazama, ingawa umepandwa, je! Utafanikiwa? Hautakauka kabisa, upepo wa mashariki utakapoupiga? Naam, utakauka katika matuta hapo ulipopandwa.
Osée 13.15 Osée 12.1 Matthieu 21.19 Marc 11.20 Ezéchiel 19.12-19.14
11 Tena neno la Bwana likanijia, kusema,
12 Waambie sasa nyumba hii iliyoasi, Hamjui maana ya mambo haya? Waambie, Tazama, mfalme wa Babeli alifika Yerusalemu, akamtwaa mfalme wake, na wakuu wake, akawachukua pamoja naye mpaka Babeli;
Ezéchiel 24.19 Ezéchiel 1.2 Ezéchiel 17.3 Marc 4.13 2 Chroniques 36.9-36.10
13 akawatwaa baadhi ya wazao wa kifalme; kisha akafanya agano naye, akamwapisha; akawaondoa watu wa nchi wenye nguvu;
2 Chroniques 36.13 Ezéchiel 17.5 2 Rois 24.15-24.17 Jérémie 24.1 Jérémie 37.1
14 ili ufalme huo uwe duni usijiinue, lakini usimame kwa kulishika agano lake.
Ezéchiel 29.14 Lamentations 5.10 Ezéchiel 17.6 Néhémie 9.36-9.37 1 Samuel 2.30
15 Lakini alimwasi kwa kupeleka wajumbe huko Misri, wampe farasi na watu wengi. Je! Atafanikiwa? Afanyaye mambo hayo ataokoka? Atalivunja agano, kisha akaokoka?
Ezéchiel 17.7 Deutéronome 17.16 Jérémie 34.3 2 Rois 24.20 Jérémie 38.18
16 Kama mimi niishivyo, asema Bwana MUNGU, hakika mahali pale akaapo mfalme aliyemmilikisha, ambaye alikidharau kiapo chake, na kulivunja agano lake, ndipo atakapokufa pamoja naye kati ya Babeli.
Ezéchiel 12.13 Jérémie 52.11 Zacharie 5.3-5.4 Nombres 30.2 Jérémie 32.4-32.5
17 Wala Farao na jeshi lake kubwa, na kusanyiko lake kuu la watu, hawatamfaa kitu vitani, watakapofanya maboma, na kujenga ngome, ili kukatilia mbali watu wengi.
Jérémie 37.7 Ezéchiel 29.6-29.7 Esaïe 36.6 Ezéchiel 4.2 Jérémie 37.5
18 Kwa maana amekidharau kiapo kwa kulivunja agano; na tazama, ametia mkono wake, na pamoja na hayo ameyatenda mambo hayo yote; hataokoka.
1 Chroniques 29.24 Lamentations 5.6 2 Chroniques 30.8
19 Basi Bwana MUNGU asema hivi; Kama mimi niishivyo, hakika kiapo changu alichokidharau, na agano langu alilolivunja, nitampatiliza kichwani pake.
Jérémie 5.9 Jérémie 7.9-7.15 Jérémie 5.2 Deutéronome 5.11 Ezéchiel 21.23-21.27
20 Nami nitatandika wavu wangu juu yake, naye atanaswa katika mtego wangu, nami nitamleta hata Babeli; nami nitateta naye huko kwa sababu ya kosa lake alilonikosa.
Ezéchiel 12.13 Ezéchiel 20.35-20.36 Jérémie 2.35 Ezéchiel 32.3 Jérémie 39.5-39.7
21 Na wakimbizi wake wote wa vikosi vyake vyote wataanguka kwa upanga, na hao watakaosalia watatawanyika kwenye kila upepo; nanyi mtajua ya kuwa mimi, Bwana, nimenena neno hili.
2 Rois 25.11 2 Rois 25.5 Ezéchiel 5.12 Ezéchiel 12.14 Jérémie 48.44
22 Bwana MUNGU asema hivi; Mimi nami nitakitwaa kilele kirefu cha mwerezi, na kukipandikiza mahali; na katika vitawi vyake vilivyo juu nitatwaa kitawi kimoja kilicho chororo, nami nitakipanda juu ya mlima mrefu ulioinuka sana;
Ezéchiel 20.40 Psaumes 2.6 Psaumes 72.16 Daniel 2.44-2.45 Jérémie 33.15-33.16
23 juu ya mlima wa mahali palipoinuka pa Israeli nitakipanda; nacho kitatoa matawi, na kuzaa matunda, nao utakuwa mwerezi mzuri; na chini yake watakaa ndege wa kila namna ya mbawa; katika uvuli wa matawi yake watakaa.
Matthieu 13.32 Galates 3.28 Ezéchiel 31.6 Colossiens 3.11 Esaïe 2.2
24 Na miti yote ya mashamba itajua ya kuwa mimi, Bwana, nimeushusha chini mti mrefu, na kuuinua mti mfupi, na kuukausha mti mbichi, na kuusitawisha mti mkavu; mimi, Bwana, nimenena, nami nimelitenda jambo hili.
Ezéchiel 22.14 Amos 9.11 Ezéchiel 24.14 Job 40.12 1 Corinthiens 1.27-1.28

Cette Bible est dans le domaine public.