Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Jérémie 35.15
Bible en Swahili de l’est


L’exemple des Récabites

1 Neno hili ndilo lililomjia Yeremia, kutoka kwa Bwana, katika siku za Yehoyakimu, mwana wa Yosia, mfalme wa Yuda, kusema,
2 Rois 23.35 Jérémie 1.3 Jérémie 25.1 Jérémie 36.29 Jérémie 26.1
2 Enenda nyumbani kwa Warekabi, ukanene nao, ukawalete nyumbani kwa Bwana, katika chumba kimoja, ukawape divai wanywe.
1 Chroniques 2.55 1 Chroniques 9.26 1 Rois 6.5-6.6 Jérémie 35.8 Ezéchiel 41.5-41.11
3 Basi nikamtwaa Yaazania, mwana wa Yeremia, mwana wa Habasinia, na ndugu zake, na wanawe wote, na nyumba yote ya Warekabi;
4 nikawaleta ndani ya nyumba ya Bwana, ndani ya chumba cha wana wa Hanani, mwana wa Igdalia, mtu wa Mungu, kilichokuwa karibu na chumba cha wakuu, nacho kilikuwa juu ya chumba cha Maaseya, mwana wa Shalumu, bawabu;
Deutéronome 33.1 2 Rois 12.9 2 Chroniques 8.14 2 Rois 1.11-1.13 1 Chroniques 9.18-9.19
5 nikaweka mabakuli yaliyojaa divai, na vikombe, mbele ya wana wa nyumba ya Warekabi, nikawaambia, Nyweni divai.
Amos 2.12 Ecclésiaste 9.7 Jérémie 35.2 2 Corinthiens 2.9
6 Lakini wakasema, Hatutakunywa divai; kwa maana Yonadabu, mwana wa Rekabu, baba yetu, alituamuru, akisema, Msinywe divai, ninyi wala wana wenu, hata milele;
2 Rois 10.15 Lévitique 10.9 Luc 1.15 1 Chroniques 2.55 Juges 13.7
7 wala msijenge nyumba, wala msipande mbegu, wala msipande mizabibu, wala msiwe nayo; bali siku zenu zote mtakaa katika hema; mpate kuishi siku nyingi katika nchi ambayo mtakaa ndani yake hali ya wageni.
Ephésiens 6.2-6.3 Genèse 25.27 Exode 20.12 Lévitique 23.42-23.43 Hébreux 11.9-11.13
8 Nasi tumeitii sauti ya Yonadabu, mwana wa Rekabu, baba yetu, katika yote aliyotuamuru, kwamba tusinywe divai siku zetu zote, sisi, na wake zetu, na wana wetu, na binti zetu;
Colossiens 3.20 Proverbes 4.10 Proverbes 4.1-4.2 Proverbes 6.20 Proverbes 1.8-1.9
9 wala tusijijengee nyumba za kukaa; wala hatuna shamba la mizabibu, wala konde, wala mbegu;
1 Timothée 6.6 Psaumes 37.16 Jérémie 35.7 2 Rois 5.26 Nombres 16.14
10 bali tumekaa katika hema, nasi tumetii; tukafanya sawasawa na yote aliyotuamuru Yonadabu, baba yetu.
11 Lakini ikawa, Nebukadreza, mfalme wa Babeli, alipopanda akaingia nchi hii, ndipo tukasema, Haya! Twende Yerusalemu, tukiliogopa jeshi la Wakaldayo, na tukiliogopa jeshi la Washami; basi hivyo tunakaa Yerusalemu.
Jérémie 8.14 2 Rois 24.1-24.2 Daniel 1.1-1.2 Jérémie 4.5-4.7 Marc 13.14
12 Ndipo neno la Bwana likamjia Yeremia, kusema,
13 Bwana wa majeshi, Mungu wa Israeli, asema hivi, Enenda ukawaambie wana wa Yuda, na wenyeji wa Yerusalemu, Je! Hamtaki kupokea mafundisho, myasikilize maneno yangu? Asema Bwana.
Jérémie 32.33 Jérémie 5.3 Jérémie 6.8-6.10 Esaïe 28.9-28.12 Esaïe 42.23
14 Maneno ya Yonadabu, mwana wa Rekabu, aliyowaamuru wanawe, kwamba wasinywe divai, yametimizwa, na hata leo hawanywi; maana waitii hiyo amri ya baba yao; lakini mimi nimesema nanyi, nikiamka mapema na kunena, bali ninyi hamkunisikiliza mimi.
Esaïe 30.9 Jérémie 7.13 Jérémie 11.7 Esaïe 50.2 Jérémie 25.3-25.4
15 Pia naliwapeleka watumishi wangu wote, manabii, kwenu ninyi, nikiamka mapema na kuwapeleka, nikisema, Rudini sasa, kila mtu na aiache njia yake mbaya, mkatengeneze matendo yenu, wala msiwafuate miungu mingine, ili kuwatumikia, nanyi mtakaa katika nchi hii, niliyowapa ninyi na baba zenu; lakini hamkutega masikio yenu, wala hamkunisikiliza.
Jérémie 18.11 Jérémie 25.5-25.6 Jérémie 17.20-17.25 Ezéchiel 18.30-18.32 Actes 26.20
16 Basi, kwa kuwa wana wa Yonadabu, mwana wa Rekabu, wameitimiza amri ya baba yao aliyowaamuru, lakini watu hawa hawakunisikiliza mimi;
Malachie 1.6 Jérémie 35.14 Luc 15.11-15.13 Esaïe 1.3 Luc 15.28-15.30
17 kwa sababu hiyo, asema Bwana, Mungu wa majeshi, Mungu wa Israeli; Tazama nitaleta juu ya Yuda, na juu ya wenyeji wote wa Yerusalemu, mabaya yote niliyoyatamka juu yao; kwa sababu nimesema nao, wasinisikilize; nimewaita, wala hawakuniitikia.
Jérémie 7.13 Romains 10.21 Esaïe 66.4 Esaïe 65.12 Jérémie 7.26-7.27
18 Naye Yeremia akawaambia watu wa nyumba ya Warekabi, Bwana wa majeshi, Mungu wa Israeli, asema hivi, Kwa sababu mmeitii amri ya Yonadabu, baba yenu, na kuyashika maagizo yake yote, na kutenda sawasawa na yote aliyowaamuru;
Exode 20.12 Ephésiens 6.1-6.3 Deutéronome 5.16
19 basi, kwa sababu hiyo, Bwana wa majeshi, Mungu wa Israeli, asema hivi, Yonadabu, mwana wa Rekabu, hatakosa kuwa na mtu wa kusimama mbele zangu hata milele.
Jérémie 15.19 1 Chroniques 2.55 Luc 21.36 Jude 1.24 Jérémie 33.17-33.18

Cette Bible est dans le domaine public.