Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Ecclésiaste 7.19
Bible en Swahili de l’est


Conseils de sagesse

Les épreuves et la sagesse

1 Heri sifa njema kuliko marhamu nzuri; Na siku ya kufa kuliko siku ya kuzaliwa.
Proverbes 22.1 Ecclésiaste 4.2 Apocalypse 14.13 2 Corinthiens 5.8 Philippiens 1.21-1.23
2 Heri kuiendea nyumba ya matanga, Kuliko kuiendea nyumba ya karamu. Kwa maana huo ndio mwisho wa wanadamu wote, naye aliye hai atautia moyoni mwake.
Psaumes 90.12 Nombres 23.10 Job 1.4-1.5 1 Pierre 4.3-4.4 Aggée 1.5
3 Huzuni ni afadhali kuliko kicheko, Maana simanzi ya uso ni faida ya moyo.
2 Corinthiens 7.9-7.11 Hébreux 12.10-12.11 Jacques 4.8-4.10 Romains 5.3-5.4 Zacharie 12.10-12.14
4 Moyo wake mwenye hekima umo nyumbani mwa matanga, bali moyo wake mpumbavu umo nyumbani mwa furaha.
2 Samuel 13.28 Jean 11.31-11.35 Jérémie 51.39 Daniel 5.30 Esaïe 53.3-53.4
5 Heri kusikia laumu ya wenye hekima, Kuliko mtu kusikia wimbo wa wapumbavu;
Proverbes 15.31-15.32 Psaumes 141.5 Proverbes 13.18 Proverbes 9.8 Proverbes 13.13
6 Maana kama mlio wa miiba chini ya sufuria, Ndivyo kilivyo kicheko cha mpumbavu. Hayo nayo ni ubatili.
Psaumes 58.9 Psaumes 118.12 Ecclésiaste 2.2 2 Pierre 2.13-2.17 Luc 6.25
7 Kweli jeuri humpumbaza mwenye hekima, Na rushwa huuharibu ufahamu.
Deutéronome 16.19 Exode 23.8 Proverbes 17.23 Deutéronome 28.65 Deutéronome 28.33-28.34
8 Heri mwisho wa neno kuliko mwanzo wake, Na mvumilivu rohoni kuliko mwenye roho ya kiburi.
Proverbes 14.29 Hébreux 10.36 1 Pierre 1.13 Proverbes 28.25 Luc 21.19
9 Usifanye haraka kukasirika rohoni mwako, Maana hasira hukaa kifuani mwa wapumbavu.
Jacques 1.19 Proverbes 14.17 Proverbes 16.32 Proverbes 26.23-26.26 Genèse 34.30-34.31
10 Usiseme, Kwani siku za kale kupita siku hizi? Maana si kwa hekima uulizavyo neno hilo.
Juges 6.13 Romains 3.9-3.19 Romains 1.22-1.32 Esaïe 50.1 Psaumes 14.2-14.3
11 Hekima ni njema, mfano wa urithi; Naam, nayo ni bora kwao walionao jua.
Ecclésiaste 11.7 1 Timothée 6.17-6.19 1 Rois 3.6-3.9 Proverbes 8.10-8.11 Ecclésiaste 2.13
12 Kwa maana hekima ni ulinzi, kama vile fedha ilivyo ulinzi; na ubora wa maarifa ni ya kwamba hekima humhifadhi yeye aliye nayo.
Proverbes 3.18 Proverbes 8.35 Proverbes 2.11 Esaïe 30.2 Esaïe 32.2
13 Tafakari vema kazi yake Mungu; kwa sababu ni nani awezaye kukinyosha kitu kile alichokipotosha yeye?
Ecclésiaste 1.15 Esaïe 14.27 Job 12.14 Romains 9.19 Esaïe 46.10-46.11
14 Siku ya kufanikiwa ufurahi, Na siku ya mabaya ufikiri. Mungu ameifanya hiyo moja kwenda sambamba na hiyo ya pili, ili mwanadamu asipate kulijua neno lo lote litakalofuata baada yake.
Ecclésiaste 3.22 Ecclésiaste 3.4 Deutéronome 28.47 Luc 15.17-15.18 Job 10.1-10.2
15 Mambo hayo yote nimeyaona mimi katika siku za ubatili wangu, yuko mwenye haki apoteaye katika haki yake, yuko na mtu mwovu azidishaye maisha yake katika udhalimu wake.
Ecclésiaste 8.12-8.14 Ecclésiaste 6.12 Ecclésiaste 2.23 1 Samuel 22.18-22.19 1 Rois 21.13
16 Usiwe na haki kupita kiasi; Wala usijiongezee hekima mno; Kwani kujiangamiza mwenyewe?
Romains 12.3 Philippiens 3.6 Luc 18.12 Proverbes 25.16 Genèse 3.6
17 Usiwe mwovu kupita kiasi; Wala usiwe mpumbavu; Kwani ufe kabla ya wakati wako?
Proverbes 10.27 Psaumes 55.23 Actes 5.10 Actes 12.23 Job 15.32-15.33
18 Ni vizuri kwamba ulishike neno hilo; naam, hata kwa neno hilo tena usiuondoe mkono wako; kwa kuwa mtu yule amchaye Mungu atatoka katika hayo yote.
Ecclésiaste 12.13 Luc 11.42 Ecclésiaste 8.12 Ecclésiaste 11.6 Proverbes 8.20
19 Hekima ni nguvu zake mwenye hekima, Zaidi ya wakuu kumi waliomo mjini.
Proverbes 24.5 Proverbes 21.22 Colossiens 1.9-1.11 Ecclésiaste 9.13-9.18 2 Samuel 20.16-20.22
20 Bila shaka hakuna mwanadamu mwenye haki hapa duniani, ambaye afanya mema, asifanye dhambi.
1 Rois 8.46 Romains 3.23 2 Chroniques 6.36 Esaïe 53.6 Jacques 3.2
21 Tena, usitie moyoni mwako maneno yote yaliyosemwa; usije ukamsikia mtumwa wako mwenyewe ali anakutukana.
Proverbes 30.10 1 Corinthiens 13.5-13.7 Esaïe 29.21 2 Samuel 16.10 2 Samuel 19.19
22 Kwa kuwa mara nyingi moyo wako pia unajua ya kwamba wewe mwenyewe umewatukana watu wengine.
Matthieu 15.19 1 Rois 2.44 Jacques 3.9 Matthieu 18.32-18.35 Jean 8.7-8.9

La sagesse et les hommes

23 Mambo hayo yote mimi nimeyahakikisha katika hekima. Nilisema, Mimi nitakuwa na hekima, lakini imefarakana nami.
Romains 1.22 1 Corinthiens 1.20 Genèse 3.5 1 Rois 11.1-11.8 1 Rois 3.11-3.12
24 Mambo yale yaliyo mbali, na yale yaendayo chini sana, ni mtu yupi awezaye kuyatafuta?
Romains 11.33 1 Timothée 6.16 Job 28.28 Psaumes 139.6 Job 11.7-11.8
25 Nikageuka, na moyo wangu ulikazwa katika kujua na kupeleleza, na kuitafuta hekima, na maana ya mambo yaliyoko; ili nifahamu ya kuwa uovu ni upumbavu, na upumbavu ni wazimu.
Ecclésiaste 10.13 Ecclésiaste 1.13-1.17 Proverbes 26.11 Ecclésiaste 9.1-9.3 Jérémie 12.1-12.2
26 Nami nimeona lililo na uchungu kupita mauti; yaani, mwanamke ambaye moyo wake ni mitego na tanzi, na mikono yake ni kama vifungo; yeye ampendezaye Mungu atamponyoka, bali mwenye dhambi atanaswa na yeye.
Proverbes 22.14 Proverbes 5.3-5.5 Proverbes 2.18-2.19 Ecclésiaste 2.26 Proverbes 2.16
27 Tazama, asema Mhubiri, mimi nimeyaona hayo kwa kulinganisha hili na hili, ili kuitafuta jumla;
Ecclésiaste 12.8-12.10 Ecclésiaste 1.1-1.2
28 ambayo bado nafsi yangu nikali nikiitafuta, nisiione; mwanamume mmoja katika elfu nimemwona; bali mwanamke mmoja miongoni mwa wote mimi sikumwona.
Job 33.23 Psaumes 12.1 Esaïe 26.9 1 Rois 11.1-11.3 Ecclésiaste 7.23-7.24
29 Tazama, hili tu nimeliona; Mungu amemfanya mwanadamu mnyofu, lakini wamebuni mavumbuzi mengi.
Genèse 3.6-3.7 Genèse 1.26-1.27 Jérémie 4.22 Romains 1.21-1.32 Jérémie 2.12-2.13

Cette Bible est dans le domaine public.