Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Proverbes 21.22
Bible en Swahili de l’est


1 Moyo wa mfalme huwa katika mkono wa Bwana; Kama mifereji ya maji huugeuza po pote apendapo.
Proverbes 16.9 Proverbes 20.24 Esdras 6.22 Actes 7.10 Daniel 4.35
2 Kila njia ya mtu ni sawa machoni pake mwenyewe; Bali Bwana huipima mioyo.
Proverbes 16.2 Proverbes 16.25 Luc 16.15 Proverbes 24.12 1 Samuel 16.7
3 Kutenda haki na hukumu Humpendeza Bwana kuliko kutoa sadaka.
1 Samuel 15.22 Proverbes 15.8 Osée 6.6 Michée 6.6-6.8 Psaumes 50.8
4 Macho yenye kiburi, na moyo wa kutakabari, Hata ukulima wa waovu, ni dhambi.
Proverbes 6.17 Luc 18.14 Romains 14.23 Esaïe 2.11 Esaïe 3.16
5 Mawazo ya wenye bidii huuelekea utajiri tu; Bali kila mwenye pupa huuelekea uhitaji.
Proverbes 10.4 Proverbes 13.4 Proverbes 14.29 Proverbes 27.23-27.27 Proverbes 28.22
6 Kupata akiba ya mali kwa ulimi wa uongo Ni moshi upeperushwao; ni kutafuta mauti.
Proverbes 20.21 Proverbes 13.11 Proverbes 10.2 2 Pierre 2.3 Proverbes 8.36
7 Jeuri ya wabaya itawaondolea mbali; Kwa sababu wamekataa kutenda hukumu.
Ezéchiel 18.18 Proverbes 1.18-1.19 Michée 3.9-3.12 Jérémie 7.15 Proverbes 21.21
8 Njia yake aliyelemewa na dhambi imepotoka sana; Bali mtu aliye safi, kazi yake ni sawasawa.
Proverbes 2.15 Tite 2.14 Matthieu 12.33 1 Pierre 1.22-1.23 Actes 15.9
9 Ni afadhali kukaa katika pembe ya darini, Kuliko katika nyumba pana pamoja na mwanamke mgomvi.
Proverbes 19.13 Proverbes 25.24 Proverbes 21.19 Proverbes 12.4 Proverbes 15.17
10 Nafsi ya mtu mbaya hutamani uovu; Jirani yake hapati fadhili machoni pake.
Marc 7.21-7.22 Proverbes 3.29 Michée 3.2-3.3 Jacques 2.13 Psaumes 36.4
11 Mwenye mzaha aadhibiwapo, mjinga hupata hekima; Na mwenye hekima afundishwapo, hupokea maarifa.
Proverbes 19.25 Actes 5.11-5.14 Psaumes 64.7-64.9 Actes 5.5 Hébreux 2.1-2.3
12 Mwenye haki huitafakari nyumba ya mtu mbaya; Jinsi wabaya waangushwavyo wakaangamia.
Psaumes 37.35-37.36 2 Pierre 3.6-3.7 Proverbes 14.32 Job 8.15 1 Corinthiens 10.5
13 Azibaye masikio yake asisikie kilio cha maskini, Yeye naye atalia, lakini hatasikiwa.
Jacques 2.13-2.16 Actes 7.57 Esaïe 58.6-58.9 Matthieu 18.30-18.35 Néhémie 5.1-5.5
14 Kipawa cha siri hutuliza hasira; Na rushwa bindoni humliza ghadhabu kali.
Proverbes 18.16 Proverbes 19.6 Proverbes 17.8 Genèse 43.11 Matthieu 6.3-6.4
15 Ni furaha yao wenye haki kutenda hukumu; Lakini ni uharibifu kwao watendao maovu.
Proverbes 10.29 Matthieu 7.23 Ecclésiaste 3.12 Psaumes 40.8 Psaumes 119.16
16 Mtu aikosaye njia ya busara Atakaa katika mkutano wao waliokufa.
Psaumes 49.14 Hébreux 10.38 Ephésiens 2.1 Proverbes 9.18 Psaumes 125.5
17 Mtu apendaye anasa atakuwa maskini; Apendaye mvinyo na mafuta hatakuwa tajiri.
Proverbes 23.21 Proverbes 21.20 Proverbes 5.10-5.11 Luc 16.24-16.25 1 Timothée 5.6
18 Mtu asiye haki ni fidia ya wenye haki; Naye afanyaye hila ni badala ya watu wa adili.
Proverbes 11.8 Esaïe 53.4-53.5 Esaïe 55.8-55.9 1 Pierre 3.18 Esaïe 43.3-43.4
19 Ni afadhali kukaa katika nchi ya nyika; Kuliko na mwanamke mgomvi, mchokozi.
Proverbes 21.9 Psaumes 55.6-55.7 Psaumes 120.5-120.6 Jérémie 9.2
20 Kuna hazina ya thamani na mafuta katika maskani ya mwenye hekima; Bali mwanadamu aliye mpumbavu huyameza.
Psaumes 112.3 Matthieu 25.3-25.4 Psaumes 23.5 Proverbes 15.6 Proverbes 10.22
21 Aandamaye haki na fadhili, Ataona uhai na haki na heshima.
Matthieu 5.6 Proverbes 15.9 1 Corinthiens 15.58 Romains 14.19 2 Timothée 2.22
22 Mwenye hekima huupandia mji wao wenye nguvu; Na kuziangusha nguvu za tumaini lao.
Ecclésiaste 7.19 Ecclésiaste 9.13-9.18 Proverbes 24.5 2 Samuel 5.6-5.9 2 Samuel 20.16-20.22
23 Mtu azuiaye kinywa chake na ulimi wake, Atajilinda nafsi yake na taabu.
Proverbes 12.13 Proverbes 13.3 Proverbes 18.21 Proverbes 10.19 Jacques 3.2-3.13
24 Mwenye kiburi na kutakabari, jina lake ni mbishi; Hutenda mambo katika majivuno ya kiburi chake.
Psaumes 1.1 Proverbes 1.22 Matthieu 2.16 Esaïe 16.6 Ecclésiaste 7.8-7.9
25 Matakwa yake mtu mvivu humfisha, Kwa maana mikono yake hukataa kufanya kazi.
Proverbes 13.4 Proverbes 12.27 Proverbes 24.30-24.34 Proverbes 19.24 Proverbes 26.16
26 Kuna atamaniye kwa choyo mchana kutwa; Bali mwenye haki hutoa wala hanyimi.
Psaumes 37.26 Psaumes 112.9 Luc 6.30-6.36 2 Corinthiens 8.7-8.9 1 Thessaloniciens 2.5-2.9
27 Sadaka ya wasio haki ni chukizo; Si zaidi sana ailetapo mwenye nia mbaya!
Esaïe 66.3 Proverbes 15.8 Jérémie 6.20 1 Samuel 15.21-15.23 Jérémie 7.11-7.12
28 Shahidi wa uongo atapotea; Bali mtu asikiaye atasema maneno yadumuyo.
Proverbes 19.5 Proverbes 19.9 Proverbes 25.18 Proverbes 6.19 Tite 3.8
29 Asiye haki huufanya uso wake kuwa mgumu; Bali mtu mnyofu huzifikiri njia zake.
Proverbes 11.5 Aggée 2.18-2.19 Psaumes 119.5 1 Thessaloniciens 3.11 Psaumes 119.59
30 Hapana hekima, wala ufahamu, Wala shauri, juu ya Bwana.
Actes 5.39 Jérémie 9.23 Esaïe 8.9-8.10 Proverbes 19.21 Esaïe 14.27
31 Farasi huwekwa tayari kwa siku ya vita; Lakini Bwana ndiye aletaye wokovu.
Esaïe 31.1 Psaumes 20.7 Psaumes 3.8 Psaumes 33.17-33.18 Psaumes 144.10

Cette Bible est dans le domaine public.