Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Proverbes 21.1
Bible en Swahili de l’est


1 Moyo wa mfalme huwa katika mkono wa Bwana; Kama mifereji ya maji huugeuza po pote apendapo.
Proverbes 16.9 Proverbes 20.24 Esdras 6.22 Actes 7.10 Daniel 4.35
2 Kila njia ya mtu ni sawa machoni pake mwenyewe; Bali Bwana huipima mioyo.
Proverbes 16.2 Proverbes 16.25 Luc 16.15 1 Samuel 16.7 Proverbes 24.12
3 Kutenda haki na hukumu Humpendeza Bwana kuliko kutoa sadaka.
1 Samuel 15.22 Proverbes 15.8 Osée 6.6 Michée 6.6-6.8 Jérémie 7.21-7.23
4 Macho yenye kiburi, na moyo wa kutakabari, Hata ukulima wa waovu, ni dhambi.
Proverbes 6.17 Proverbes 8.13 Proverbes 21.27 Proverbes 30.13 Esaïe 2.17
5 Mawazo ya wenye bidii huuelekea utajiri tu; Bali kila mwenye pupa huuelekea uhitaji.
Proverbes 10.4 Proverbes 13.4 Proverbes 14.29 Proverbes 27.23-27.27 Proverbes 28.22
6 Kupata akiba ya mali kwa ulimi wa uongo Ni moshi upeperushwao; ni kutafuta mauti.
Proverbes 13.11 Proverbes 20.21 Proverbes 8.36 Proverbes 10.2 2 Pierre 2.3
7 Jeuri ya wabaya itawaondolea mbali; Kwa sababu wamekataa kutenda hukumu.
Psaumes 9.16 Ephésiens 5.6 Zacharie 5.3-5.4 Psaumes 7.16 Proverbes 22.22-22.23
8 Njia yake aliyelemewa na dhambi imepotoka sana; Bali mtu aliye safi, kazi yake ni sawasawa.
Proverbes 2.15 1 Jean 2.29 Genèse 6.12 Ephésiens 2.2-2.3 Ecclésiaste 9.3
9 Ni afadhali kukaa katika pembe ya darini, Kuliko katika nyumba pana pamoja na mwanamke mgomvi.
Proverbes 19.13 Proverbes 25.24 Proverbes 21.19 Proverbes 12.4 Proverbes 15.17
10 Nafsi ya mtu mbaya hutamani uovu; Jirani yake hapati fadhili machoni pake.
Michée 3.2-3.3 Marc 7.21-7.22 Proverbes 3.29 Esaïe 32.6-32.8 Proverbes 12.12
11 Mwenye mzaha aadhibiwapo, mjinga hupata hekima; Na mwenye hekima afundishwapo, hupokea maarifa.
Proverbes 19.25 Nombres 16.34 Deutéronome 13.11 Hébreux 10.28-10.29 Proverbes 18.15
12 Mwenye haki huitafakari nyumba ya mtu mbaya; Jinsi wabaya waangushwavyo wakaangamia.
Psaumes 37.35-37.36 Proverbes 11.3-11.5 Habakuk 2.9-2.12 Job 5.3 Psaumes 52.5
13 Azibaye masikio yake asisikie kilio cha maskini, Yeye naye atalia, lakini hatasikiwa.
Jacques 2.13-2.16 Matthieu 6.14 Néhémie 5.13 Psaumes 18.41 Jérémie 34.16-34.17
14 Kipawa cha siri hutuliza hasira; Na rushwa bindoni humliza ghadhabu kali.
Proverbes 18.16 Proverbes 19.6 Proverbes 17.8 Genèse 32.20 Genèse 43.11
15 Ni furaha yao wenye haki kutenda hukumu; Lakini ni uharibifu kwao watendao maovu.
Proverbes 10.29 Psaumes 119.92 Esaïe 64.5 Jean 4.34 Luc 13.27-13.28
16 Mtu aikosaye njia ya busara Atakaa katika mkutano wao waliokufa.
Psaumes 49.14 2 Pierre 2.21-2.22 Jean 3.19-3.20 1 Jean 2.19 Hébreux 10.26-10.27
17 Mtu apendaye anasa atakuwa maskini; Apendaye mvinyo na mafuta hatakuwa tajiri.
Proverbes 23.21 Proverbes 21.20 Luc 15.13-15.16 2 Timothée 3.4 Proverbes 5.10-5.11
18 Mtu asiye haki ni fidia ya wenye haki; Naye afanyaye hila ni badala ya watu wa adili.
Proverbes 11.8 Esaïe 55.8-55.9 1 Pierre 3.18 Esaïe 43.3-43.4 Esaïe 53.4-53.5
19 Ni afadhali kukaa katika nchi ya nyika; Kuliko na mwanamke mgomvi, mchokozi.
Proverbes 21.9 Psaumes 120.5-120.6 Jérémie 9.2 Psaumes 55.6-55.7
20 Kuna hazina ya thamani na mafuta katika maskani ya mwenye hekima; Bali mwanadamu aliye mpumbavu huyameza.
Psaumes 112.3 Matthieu 25.3-25.4 Ecclésiaste 7.11 Psaumes 23.5 Proverbes 15.6
21 Aandamaye haki na fadhili, Ataona uhai na haki na heshima.
Matthieu 5.6 Proverbes 15.9 1 Corinthiens 15.58 2 Timothée 4.7-4.8 Osée 6.3
22 Mwenye hekima huupandia mji wao wenye nguvu; Na kuziangusha nguvu za tumaini lao.
Ecclésiaste 7.19 Proverbes 24.5 2 Samuel 5.6-5.9 2 Samuel 20.16-20.22 Ecclésiaste 9.13-9.18
23 Mtu azuiaye kinywa chake na ulimi wake, Atajilinda nafsi yake na taabu.
Proverbes 12.13 Proverbes 13.3 Proverbes 18.21 Proverbes 17.27-17.28 Proverbes 10.19
24 Mwenye kiburi na kutakabari, jina lake ni mbishi; Hutenda mambo katika majivuno ya kiburi chake.
Psaumes 1.1 Proverbes 1.22 Proverbes 16.18 Proverbes 6.17 Jérémie 48.29
25 Matakwa yake mtu mvivu humfisha, Kwa maana mikono yake hukataa kufanya kazi.
Proverbes 13.4 Proverbes 20.4 Proverbes 15.19 Matthieu 25.26 Proverbes 12.24
26 Kuna atamaniye kwa choyo mchana kutwa; Bali mwenye haki hutoa wala hanyimi.
Psaumes 37.26 Psaumes 112.9 Actes 20.33-20.35 Matthieu 5.42 Luc 6.30-6.36
27 Sadaka ya wasio haki ni chukizo; Si zaidi sana ailetapo mwenye nia mbaya!
Esaïe 66.3 Proverbes 15.8 Jérémie 6.20 Matthieu 23.13 1 Samuel 15.21-15.23
28 Shahidi wa uongo atapotea; Bali mtu asikiaye atasema maneno yadumuyo.
Proverbes 19.5 Proverbes 19.9 Deutéronome 19.16-19.19 2 Corinthiens 4.13 Proverbes 25.18
29 Asiye haki huufanya uso wake kuwa mgumu; Bali mtu mnyofu huzifikiri njia zake.
Proverbes 11.5 Proverbes 29.1 Jérémie 5.3 Jérémie 3.2-3.3 Proverbes 28.14
30 Hapana hekima, wala ufahamu, Wala shauri, juu ya Bwana.
Actes 5.39 Esaïe 14.27 Jérémie 9.23 Esaïe 8.9-8.10 Proverbes 19.21
31 Farasi huwekwa tayari kwa siku ya vita; Lakini Bwana ndiye aletaye wokovu.
Esaïe 31.1 Psaumes 20.7 Psaumes 3.8 Psaumes 33.17-33.18 Jérémie 3.23

Cette Bible est dans le domaine public.