Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Exode 33.17
Bible en Swahili de l’est


1 Bwana akanena na Musa, Haya, ondokeni, katokeni hapo, wewe na hao watu uliowaleta wakwee kutoka nchi ya Misri, waende nchi hiyo niliyomwapia Ibrahimu, na Isaka, na Yakobo, niliposema, Nitakipa kizazi chako nchi hii;
Genèse 12.7 Exode 32.13 Exode 32.7 Genèse 26.3 Genèse 22.16-22.18
2 nami nitamtuma malaika aende mbele yako; nami nitawafukuza Mkanaani, na Mwamori, na Mhiti, na Mperizi, na Mhivi, na Myebusi;
Josué 24.11 Exode 32.34 Exode 23.20 Exode 23.27-23.31 Exode 34.11
3 waifikilie nchi imiminikayo maziwa na asali; kwa maana mimi sitakwenda kati yenu; kwa sababu ninyi ni watu wenye shingo ngumu; nisiwaangamize ninyi katika njia.
Exode 32.9-32.10 Exode 3.8 Nombres 16.21 Exode 33.15-33.17 Nombres 16.45
4 Watu waliposikia habari hizo mbaya wakaomboleza wala hapana mtu aliyevaa vyombo vyake vya uzuri.
Nombres 14.39 Ezéchiel 26.16 Ezéchiel 24.17 Ezéchiel 24.23 Nombres 14.1
5 Bwana akamwambia Musa, Waambie wana wa Israeli, Ninyi ni watu wenye shingo ngumu; kama mimi nikiingia kati yenu dakika moja, nitawaangamiza; basi sasa vueni vyombo vyenu vya uzuri ili nipate kujua nitakalowatenda.
Exode 33.3-33.4 Deutéronome 8.2 Genèse 22.12 Psaumes 139.23 Nombres 16.21
6 Basi wana wa Israeli wakavua vyombo vyao vyote vya uzuri, tangu mlima wa Horebu na mbele.
Exode 33.4 Exode 32.3 Jérémie 2.19

Les rencontres de Moïse avec l’Éternel

7 Basi desturi ya Musa, ilikuwa kuitwaa ile hema, na kuikita nje ya marago mbali na hayo marago; akaiita, hema ya kukutania. Hata kila mtu aliyekuwa akitaka neno kwa Bwana, akatoka, akaenda hata hema ya kukutania, iliyokuwa nje ya marago.
Exode 29.42-29.43 2 Samuel 21.1 Deutéronome 4.29 Matthieu 7.7-7.8 Esaïe 55.6-55.7
8 Hata Musa alipotoka kuiendea ile hema, watu wote waliondoka wakasimama, kila mtu mlangoni pa hema yake, akamtazama Musa, hata alipokwisha kuingia hemani.
Nombres 16.27
9 Ikawa Musa alipoingia humo hemani, ile nguzo ya wingu ikashuka, ikasimama mlangoni pa ile hema; naye Bwana akasema na Musa.
Psaumes 99.7 Exode 31.18 Exode 13.21-13.22 Nombres 11.17 Ezéchiel 3.22
10 Watu wote wakaiona nguzo ya wingu ikisimama penye mlango wa hema; watu wote wakaondoka wakasujudu, kila mtu mlangoni pa hema yake.
Luc 18.13 Exode 4.31 1 Rois 8.22 1 Rois 8.14
11 Naye Bwana akasema na Musa uso kwa uso, kama vile mtu asemavyo na rafiki yake. Kisha akageuka akarejea hata maragoni; bali mtumishi wake Yoshua, mwana wa Nuni, naye ni kijana, hakutoka mle hemani.
Nombres 12.8 Deutéronome 34.10 Genèse 32.30 Exode 24.13 Exode 17.9
12 Musa akamwambia Bwana, Angalia, wewe waniambia, Wachukue watu hawa; nawe hukunijulisha ni nani utakayemtuma pamoja nami. Walakini umesema, Nakujua jina lako, nawe umepata neema mbele zangu.
Exode 33.17 Exode 32.34 Jean 10.14-10.15 2 Timothée 2.19 Genèse 18.19
13 Basi, sasa nakuomba, ikiwa nimepata neema mbele zako, unionyeshe njia zako, nipate kukujua, ili nipate neema mbele zako; ukakumbuke ya kuwa taifa hilo ndilo watu wako.
Psaumes 25.4 Psaumes 119.33 Psaumes 86.11 Deutéronome 9.29 Psaumes 27.11
14 Akasema, Uso wangu utakwenda pamoja nawe, nami nitakupa raha.
Esaïe 63.9 Josué 21.44 Josué 22.4 Josué 23.1 Deutéronome 3.20
15 Naye akamwambia, Uso wako usipokwenda pamoja nami, usituchukue kutoka hapa.
Exode 33.3 Exode 34.9 Psaumes 4.6
16 Kwa maana itajulikanaje kuwa nimepata neema mbele zako, mimi na watu wako? Siyo kwa sababu unakwenda pamoja nasi, hata mimi na watu wako tutengwe na watu wote walio juu ya uso wa nchi?
Nombres 14.14 1 Rois 8.53 Exode 34.10 Exode 19.5-19.6 Deutéronome 4.7
17 Bwana akamwambia Musa, Nitafanya na neno hili ulilolinena, kwa maana umepata neema mbele zangu, nami nakujua jina lako.
Exode 33.12 Genèse 19.21 Esaïe 65.24 Jacques 5.16 1 Jean 5.14-5.15
18 Akasema, Nakusihi unionyeshe utukufu wako.
Exode 33.20 1 Timothée 6.16 Apocalypse 21.23 Jean 1.18 2 Corinthiens 3.18
19 Akasema, Nitapitisha wema wangu wote mbele yako, nami nitalitangaza jina la Bwana mbele yako; nami nitamfadhili yeye nitakayemfadhili; nitamrehemu yeye nitakayemrehemu.
Exode 34.5-34.7 Jérémie 31.14 Romains 9.15-9.18 Psaumes 25.13 Romains 9.23
20 Kisha akasema, Huwezi kuniona uso wangu, maana mwanadamu hataniona akaishi.
Esaïe 6.5 Genèse 32.30 Exode 24.10 1 Timothée 6.16 Jean 1.18
21 Bwana akasema, Tazama, hapa pana mahali karibu nami, nawe utasimama juu ya mwamba;
Deutéronome 5.31 Esaïe 56.5 Luc 15.1 Zacharie 3.7 Josué 20.4
22 kisha itakuwa wakati unapopita utukufu wangu, nitakutia katika ufa wa ule mwamba, na kukufunika kwa mkono wangu hata nitakapokuwa nimekwisha kupita;
Psaumes 91.4 Psaumes 91.1 Esaïe 2.21 1 Corinthiens 10.4 Esaïe 32.2
23 nami nitaondoa mkono wangu, nawe utaniona nyuma yangu, bali uso wangu hautaonekana.
Jean 1.18 Exode 33.20 1 Timothée 6.16 1 Corinthiens 13.12 Job 11.7

Cette Bible est dans le domaine public.