Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Psaumes 66.8
Bible en Swahili de l’est


Bénédictions après l’épreuve

1 Mpigie Mungu kelele za shangwe, nchi yote,
Psaumes 100.1 Psaumes 98.4 Psaumes 81.1 1 Chroniques 16.23-16.24 Psaumes 96.1
2 Imbeni utukufu wa jina lake, Tukuzeni sifa zake.
Esaïe 49.13 Psaumes 72.18 Psaumes 106.2 Néhémie 9.5 Esaïe 42.12
3 Mwambieni Mungu, Matendo yako yatisha kama nini! Kwa ajili ya wingi wa nguvu zako, Adui zako watakuja kunyenyekea mbele zako.
Psaumes 65.5 Psaumes 18.44 Juges 5.2-5.4 Psaumes 81.15 Psaumes 47.2
4 Nchi yote itakusujudia na kukuimbia, Naam, italiimbia jina lako.
Psaumes 22.27 Psaumes 117.1 Psaumes 96.1-96.2 Esaïe 11.9 Daniel 7.14
5 Njoni yatazameni matendo ya Mungu; Hutisha kwa mambo awatendayo wanadamu;
Psaumes 46.8 Psaumes 66.3 Psaumes 106.22 Nombres 23.23 Psaumes 66.16
6 Aligeuza bahari ikawa nchi kavu; Katika mto walivuka kwa miguu; Huko ndiko mlikomfurahia.
Josué 3.16 Josué 3.14 Exode 14.21-14.22 Exode 15.1-15.21 Psaumes 136.13-136.14
7 Atawala kwa uweza wake milele; Macho yake yanaangalia mataifa; Waasio wasijitukuze nafsi zao.
Psaumes 11.4 2 Chroniques 16.9 Psaumes 145.13 Psaumes 140.8 Psaumes 75.4-75.5
8 Enyi mataifa, mtukuzeni Mungu wetu, Itangazeni sauti ya sifa zake;
Apocalypse 5.11-5.14 Deutéronome 32.43 Romains 15.10-15.11 Jérémie 33.11 Apocalypse 19.5-19.6
9 Aliyeiweka nafsi yetu katika uhai, Wala hakuuacha mguu wetu usogezwe.
Psaumes 121.3 Psaumes 22.29 1 Samuel 25.29 Psaumes 94.18 Psaumes 62.2
10 Kwa maana umetupima, Ee Mungu, Umetujaribu inavyojaribiwa fedha.
Esaïe 48.10 Psaumes 17.3 Zacharie 13.9 Proverbes 17.3 1 Pierre 1.6-1.7
11 Ulituingiza ndani ya wavu, Na kuweka viunoni mwetu mzigo uliotulemea.
Lamentations 1.13 Lamentations 3.2-3.66 Job 19.6 Ezéchiel 12.13 Matthieu 6.13
12 Uliwapandisha watu Juu ya vichwa vyetu. Tulipita motoni na majini; Ukatutoa na kutuleta kunako wingi.
Esaïe 51.23 1 Thessaloniciens 3.3-3.4 Jacques 5.11 Psaumes 33.19 Actes 14.22
13 Nitaingia nyumbani mwako na kafara; Nitaondoa kwako nadhiri zangu;
Ecclésiaste 5.4 Jonas 2.9 Psaumes 100.4 Hébreux 13.15 Psaumes 116.14
14 Ambazo midomo yangu ilizinena; Kinywa changu kikazisema nilipokuwa taabuni.
1 Samuel 1.11 Genèse 28.20-28.22 Juges 11.35-11.36 Nombres 30.8 Genèse 35.3
15 Kafara za vinono nitakutolea, Pamoja na fukizo la kondoo waume, Nitatoa ng’ombe pamoja na mbuzi.
Jérémie 41.5 1 Chroniques 16.1-16.3 Psaumes 51.19 2 Samuel 6.13 2 Samuel 6.17-6.19
16 Njoni, sikieni, ninyi nyote mnaomcha Mungu, Nami nitayatangaza aliyonitendea roho yangu.
Psaumes 34.11 Psaumes 71.20 Psaumes 32.5-32.6 Psaumes 34.2 1 Jean 1.3
17 Nalimwita kwa kinywa changu, Na sifa kuu zilikuwa chini ya ulimi wangu.
Psaumes 30.1 Psaumes 116.12 Psaumes 145.1 Psaumes 116.1-116.2 Psaumes 30.8
18 Kama ningaliwaza maovu moyoni mwangu, Bwana asingesikia.
Jean 9.31 Proverbes 28.9 Esaïe 1.15 Jacques 4.3 Job 27.8-27.9
19 Hakika Mungu amesikia; Ameisikiliza sauti ya maombi yangu.
Psaumes 116.1-116.2 Lamentations 3.55-3.56 Psaumes 34.6 1 Jean 3.20-3.22 Psaumes 6.9
20 Na ahimidiwe Mungu asiyeyakataa maombi yangu, Wala kuniondolea fadhili zake.
Psaumes 51.11 Psaumes 68.35 2 Samuel 7.14-7.15 Psaumes 22.24 Psaumes 86.12-86.13

Cette Bible est dans le domaine public.