Bénédictions après l’épreuve
 1 Mpigie Mungu kelele za shangwe, nchi yote,
Psaumes 100.1  Psaumes 81.1  Psaumes 98.4  1 Chroniques 15.28  1 Chroniques 16.23-16.24  
 2 Imbeni utukufu wa jina lake, Tukuzeni sifa zake.
Psaumes 96.3-96.10  Psaumes 105.2-105.3  Esaïe 49.13  Psaumes 72.18  Psaumes 106.2  
 3 Mwambieni Mungu, Matendo yako yatisha kama nini! Kwa ajili ya wingi wa nguvu zako, Adui zako watakuja kunyenyekea mbele zako.
Psaumes 65.5  Psaumes 18.44  Juges 5.2-5.4  Psaumes 81.15  Psaumes 47.2  
 4 Nchi yote itakusujudia na kukuimbia, Naam, italiimbia jina lako.
Psaumes 22.27  Psaumes 117.1  Apocalypse 15.4  Psaumes 96.1-96.2  Esaïe 11.9  
 5 Njoni yatazameni matendo ya Mungu; Hutisha kwa mambo awatendayo wanadamu;
Psaumes 46.8  Ezéchiel 1.18  Psaumes 111.2  Psaumes 66.3  Psaumes 106.22  
 6 Aligeuza bahari ikawa nchi kavu; Katika mto walivuka kwa miguu; Huko ndiko mlikomfurahia.
Josué 3.16  Josué 3.14  Exode 14.21-14.22  Esaïe 63.13-63.14  Psaumes 104.5-104.7  
 7 Atawala kwa uweza wake milele; Macho yake yanaangalia mataifa; Waasio wasijitukuze nafsi zao.
Psaumes 11.4  Psaumes 73.3-73.12  Esaïe 10.7-10.16  Matthieu 28.18  Esaïe 37.28-37.29  
 8 Enyi mataifa, mtukuzeni Mungu wetu, Itangazeni sauti ya sifa zake;
Psaumes 66.2  Psaumes 47.1  Apocalypse 5.11-5.14  Deutéronome 32.43  Romains 15.10-15.11  
 9 Aliyeiweka nafsi yetu katika uhai, Wala hakuuacha mguu wetu usogezwe.
Psaumes 121.3  Psaumes 112.6  Psaumes 22.29  1 Samuel 25.29  Psaumes 94.18  
 10 Kwa maana umetupima, Ee Mungu, Umetujaribu inavyojaribiwa fedha.
Esaïe 48.10  Psaumes 17.3  Zacharie 13.9  1 Pierre 1.6-1.7  Proverbes 17.3  
 11 Ulituingiza ndani ya wavu, Na kuweka viunoni mwetu mzigo uliotulemea.
Lamentations 1.13  Osée 7.12  Deutéronome 33.11  Lamentations 3.2-3.66  Job 19.6  
 12 Uliwapandisha watu Juu ya vichwa vyetu. Tulipita motoni na majini; Ukatutoa na kutuleta kunako wingi.
Esaïe 51.23  1 Thessaloniciens 3.3-3.4  Psaumes 107.35-107.37  Psaumes 40.2-40.3  Jacques 5.11  
 13 Nitaingia nyumbani mwako na kafara; Nitaondoa kwako nadhiri zangu;Ecclésiaste 5.4  Psaumes 116.17-116.19  Psaumes 56.12  Jonas 2.9  Psaumes 100.4  
 14 Ambazo midomo yangu ilizinena; Kinywa changu kikazisema nilipokuwa taabuni.
Nombres 30.2  2 Samuel 22.7  1 Samuel 1.11  Genèse 28.20-28.22  Juges 11.35-11.36  
 15 Kafara za vinono nitakutolea, Pamoja na fukizo la kondoo waume, Nitatoa ng’ombe pamoja na mbuzi.
2 Samuel 6.17-6.19  Nombres 6.14  Jérémie 41.5  1 Chroniques 16.1-16.3  Psaumes 51.19  
 16 Njoni, sikieni, ninyi nyote mnaomcha Mungu, Nami nitayatangaza aliyonitendea roho yangu.
Psaumes 34.11  Psaumes 22.23-22.24  Malachie 3.16  Psaumes 71.20  Psaumes 32.5-32.6  
 17 Nalimwita kwa kinywa changu, Na sifa kuu zilikuwa chini ya ulimi wangu.
Psaumes 30.1  Psaumes 34.6  Psaumes 116.12  Psaumes 145.1  Psaumes 116.1-116.2  
 18 Kama ningaliwaza maovu moyoni mwangu, Bwana asingesikia.
Jean 9.31  Proverbes 28.9  Esaïe 1.15  Jacques 4.3  Job 27.8-27.9  
 19 Hakika Mungu amesikia; Ameisikiliza sauti ya maombi yangu.
Psaumes 116.1-116.2  Lamentations 3.55-3.56  Hébreux 5.7  Psaumes 34.6  1 Jean 3.20-3.22  
 20 Na ahimidiwe Mungu asiyeyakataa maombi yangu, Wala kuniondolea fadhili zake.
Psaumes 22.24  Psaumes 86.12-86.13  Psaumes 51.11  Psaumes 68.35  2 Samuel 7.14-7.15