Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Psaumes 66.1
Bible en Swahili de l’est


Bénédictions après l’épreuve

1 Mpigie Mungu kelele za shangwe, nchi yote,
Psaumes 100.1 Psaumes 81.1 Psaumes 98.4 1 Chroniques 15.28 1 Chroniques 16.23-16.24
2 Imbeni utukufu wa jina lake, Tukuzeni sifa zake.
1 Chroniques 29.10-29.13 Esaïe 6.3 Psaumes 107.15 Esaïe 12.4-12.6 Apocalypse 4.8-4.11
3 Mwambieni Mungu, Matendo yako yatisha kama nini! Kwa ajili ya wingi wa nguvu zako, Adui zako watakuja kunyenyekea mbele zako.
Psaumes 18.44 Psaumes 65.5 Psaumes 81.15 Psaumes 47.2 Juges 5.2-5.4
4 Nchi yote itakusujudia na kukuimbia, Naam, italiimbia jina lako.
Psaumes 22.27 Psaumes 117.1 Psaumes 67.2-67.3 Psaumes 65.5 Esaïe 2.2-2.4
5 Njoni yatazameni matendo ya Mungu; Hutisha kwa mambo awatendayo wanadamu;
Psaumes 46.8 Ezéchiel 1.18 Psaumes 111.2 Psaumes 66.3 Psaumes 106.22
6 Aligeuza bahari ikawa nchi kavu; Katika mto walivuka kwa miguu; Huko ndiko mlikomfurahia.
Josué 3.16 Josué 3.14 Exode 14.21-14.22 Psaumes 78.13 Esaïe 63.13-63.14
7 Atawala kwa uweza wake milele; Macho yake yanaangalia mataifa; Waasio wasijitukuze nafsi zao.
Psaumes 11.4 Matthieu 6.13 Psaumes 52.1-52.5 Psaumes 62.11 Daniel 6.26-6.27
8 Enyi mataifa, mtukuzeni Mungu wetu, Itangazeni sauti ya sifa zake;
Psaumes 98.4 Psaumes 66.2 Psaumes 47.1 Apocalypse 5.11-5.14 Deutéronome 32.43
9 Aliyeiweka nafsi yetu katika uhai, Wala hakuuacha mguu wetu usogezwe.
Psaumes 121.3 1 Samuel 2.9 Psaumes 125.3 Psaumes 62.6 Psaumes 112.6
10 Kwa maana umetupima, Ee Mungu, Umetujaribu inavyojaribiwa fedha.
Esaïe 48.10 Psaumes 17.3 Zacharie 13.9 1 Pierre 1.6-1.7 Proverbes 17.3
11 Ulituingiza ndani ya wavu, Na kuweka viunoni mwetu mzigo uliotulemea.
Lamentations 1.13 Matthieu 6.13 Osée 7.12 Deutéronome 33.11 Lamentations 3.2-3.66
12 Uliwapandisha watu Juu ya vichwa vyetu. Tulipita motoni na majini; Ukatutoa na kutuleta kunako wingi.
Esaïe 51.23 1 Thessaloniciens 3.3-3.4 Esaïe 43.1-43.2 Job 36.16 Esaïe 35.6-35.7
13 Nitaingia nyumbani mwako na kafara; Nitaondoa kwako nadhiri zangu;
Ecclésiaste 5.4 Psaumes 118.27 Psaumes 51.18-51.19 Psaumes 22.25 Deutéronome 12.11-12.12
14 Ambazo midomo yangu ilizinena; Kinywa changu kikazisema nilipokuwa taabuni.
Nombres 30.12 Nombres 30.2 2 Samuel 22.7 1 Samuel 1.11 Genèse 28.20-28.22
15 Kafara za vinono nitakutolea, Pamoja na fukizo la kondoo waume, Nitatoa ng’ombe pamoja na mbuzi.
2 Samuel 6.13 2 Samuel 6.17-6.19 Nombres 6.14 Jérémie 41.5 1 Chroniques 16.1-16.3
16 Njoni, sikieni, ninyi nyote mnaomcha Mungu, Nami nitayatangaza aliyonitendea roho yangu.
Psaumes 34.11 Psaumes 71.18 Psaumes 71.24 1 Corinthiens 15.8-15.10 Psaumes 71.15
17 Nalimwita kwa kinywa changu, Na sifa kuu zilikuwa chini ya ulimi wangu.
Psaumes 30.1 Psaumes 34.3-34.4 Psaumes 34.6 Psaumes 116.12 Psaumes 145.1
18 Kama ningaliwaza maovu moyoni mwangu, Bwana asingesikia.
Jean 9.31 Proverbes 28.9 Esaïe 1.15 Jacques 4.3 Job 27.8-27.9
19 Hakika Mungu amesikia; Ameisikiliza sauti ya maombi yangu.
Psaumes 116.1-116.2 Lamentations 3.55-3.56 Psaumes 6.9 Hébreux 5.7 Psaumes 34.6
20 Na ahimidiwe Mungu asiyeyakataa maombi yangu, Wala kuniondolea fadhili zake.
2 Samuel 7.14-7.15 Psaumes 22.24 Psaumes 86.12-86.13 Psaumes 51.11 Psaumes 68.35

Cette Bible est dans le domaine public.