Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Job 39.26
Bible en Swahili de l’est


1 Je! Wajua majira ya kuzaa kwao mbuzi-mwitu walio majabalini? Au waweza kusema majira ya kuzaa kulungu?
Psaumes 29.9 1 Samuel 24.2 Psaumes 104.18 Jérémie 14.5 Deutéronome 14.5
2 Je! Waweza kuhesabu miezi yao watakayoitimiza? Au je! Wajua majira ya kuzaa kwao?
Jérémie 2.24
3 Wao hujiinamisha, kuzaa watoto wao, Watupa taabu zao.
4 Watoto wao wa katika hali nzuri, hukua katika bara wazi; Huenda zao, wala hawarudi tena.
5 Ni nani aliyempeleka punda-milia aende huru? Au je! Ni nani aliyemfungulia vifungo punda-mwitu?
Job 24.5 Job 6.5 Job 11.12 Psaumes 104.11 Daniel 5.21
6 Ambaye nimeifanya nyika kuwa nyumba yake, Na nchi ya chumvi kuwa makao yake.
Psaumes 107.34 Jérémie 17.6 Job 24.5 Jérémie 2.24 Deutéronome 29.23
7 Yeye hudharau mshindo wa mji, Wala hasikii kelele zake msimamizi.
Job 3.18 Esaïe 58.3 Job 39.18 Exode 5.18 Esaïe 31.4
8 Upana wa milima ni malisho yake, Hutafuta-tafuta kila kitu kilicho kibichi.
Job 40.20-40.22 Job 40.15 Psaumes 104.27-104.28 Genèse 1.29-1.30 Psaumes 145.15-145.16
9 Je! Nyati atakubali kukutumikia? Au atakaa katika zizi lako?
Nombres 23.22 Deutéronome 33.17 Psaumes 92.10 Esaïe 1.3 Psaumes 22.21
10 Je! Waweza kumfunga nyati kwa kamba matutani? Au, yeye atayalima mabonde nyuma yako?
Osée 10.10-10.11 Job 39.5 Michée 1.13 Psaumes 129.3 Job 1.14
11 Je! Utamtumaini kwa sababu ana nguvu nyingi? Au, utamwachia yeye kazi yako?
Proverbes 14.4 Genèse 9.2 Psaumes 144.14 Genèse 1.28 Esaïe 46.1
12 Je! Utamtumaini kwamba ataileta mbegu yako nyumbani. Na kukusanya nafaka ya kiwanja chako cha kupuria?
Proverbes 3.16 Matthieu 13.30 Néhémie 13.15 Aggée 2.19 Amos 2.13
13 Bawa la mbuni hufurahi; Lakini mabawa yake na manyoya yake, je! Yana huruma?
Zacharie 5.9 Jérémie 8.7 Job 30.29 2 Chroniques 9.21 Psaumes 104.17
14 Kwani yeye huyaacha mayai yake juu ya nchi, Na kuyatia moto mchangani,
15 Na kusahau kwamba yumkini mguu kuyavunja, Au mnyama wa mwitu kuyakanyaga.
16 yeye huyafanyia ukali makinda yake, kana kwamba si yake; Ijapokuwa taabu yake ni ya bure, hana hofu;
Lamentations 4.3 1 Rois 3.26-3.27 Romains 1.31 2 Rois 6.28-6.29 Habakuk 2.13
17 Kwa sababu Mungu amemnyima akili, Wala hakumpa fahamu.
Job 35.11 Esaïe 19.11-19.14 2 Chroniques 32.31 Deutéronome 2.30 Esaïe 57.17
18 Wakati anapojiinua juu aende, Humdharau farasi na mwenye kumpanda.
Job 39.22 2 Rois 19.21 Job 41.29 Job 39.7 Job 5.22
19 Je! Wewe ulimpa farasi uwezo wake? Au, ni wewe uliyemvika shingo yake manyoya yatetemayo?
Psaumes 147.10 Psaumes 93.1 Psaumes 104.1 Exode 15.1 Job 39.25
20 Ndiwe uliyemfanya aruke kama nzige? Fahari ya mlio wake hutisha.
Jérémie 8.16 Job 41.20-41.21 Joël 2.5
21 Hupara-para bondeni, na kuzifurahia nguvu zake; Hutoka kwenda kukutana na wenye silaha.
Jérémie 8.6 Psaumes 19.5 1 Samuel 17.42 Proverbes 21.31 1 Samuel 17.4-17.10
22 Yeye hufanyia kicho dhihaka, wala hashangai; Wala hageuki kurudi nyuma mbele ya upanga.
Job 39.16 Job 39.18 Job 41.33
23 Podo humpigia makelele, Mkuki ung’aao na fumo.
Job 41.26-41.29
24 Huimeza nchi kwa ukali wake na ghadhabu; Wala hasimami kwa sauti ya baragumu.
Job 9.16 Job 37.20 Jérémie 4.19 Amos 3.6 Job 29.24
25 Kila ipigwapo baragumu yeye husema, Aha! Naye husikia harufu ya vita toka mbali, Mshindo wa maakida, na makelele.
Ezéchiel 36.2 Ezéchiel 26.2 Psaumes 70.3
26 Je! Mwewe huruka juu kwa akili zako, Na kuyanyosha mabawa yake kwenda kusini?
Cantique 2.12 Deutéronome 14.15 Lévitique 16.11 Jérémie 8.7
27 Je! Tai hupaa juu kwa amri yako, Na kufanya kioto chake mahali pa juu?
Abdias 1.4 Jérémie 49.16 Lévitique 11.13 Osée 8.1 Proverbes 23.5
28 Hukaa jabalini, ndiko kwenye malazi yake, Juu ya genge la jabali, na ngomeni.
1 Samuel 14.4
29 Toka huko yeye huchungulia mawindo; Macho yake huyaangalia toka mbali.
Job 9.26
30 Makinda yake nayo hufyonza damu; Na kwenye maiti ndiko aliko.
Matthieu 24.28 Luc 17.37 Ezéchiel 39.17-39.19

Cette Bible est dans le domaine public.