Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Job 28.23
Bible en Swahili de l’est


1 Hakika kuna shimo wachimbako fedha, Na mahali wapatapo dhahabu waisafishayo.
1 Rois 7.48-7.50 Genèse 2.11-2.12 1 Pierre 1.7 1 Rois 10.21 Proverbes 27.21
2 Chuma hufukuliwa katika ardhi, Na shaba huyeyushwa katika mawe.
Deutéronome 8.9 Genèse 4.22 Nombres 31.22 1 Chroniques 22.14
3 Binadamu hukomesha giza; Huyatafuta-tafuta hata mpaka ulio mbali, Mawe ya giza kuu, giza tupu.
Ecclésiaste 1.13 Luc 16.8 Job 38.16-38.17 Proverbes 2.4 Job 10.21-10.22
4 Hufukua shimo mbali na makao ya watu; Husahauliwa na nyayo zipitazo; Huning’inia mbali na watu, huyumba-yumba huko na huko.
5 Katika ardhi ndimo kitokeamo chakula; Na chini yake hupinduliwa kama kwa moto.
Psaumes 104.14-104.15 Genèse 1.11-1.12 Ezéchiel 28.13-28.14 Genèse 1.29 Esaïe 28.25-28.29
6 Mawe yake ni mahali zipatikanapo yakuti; Nayo ina mchanga wa dhahabu.
Exode 24.10 Job 28.16 Esaïe 54.11 Apocalypse 21.19 Cantique 5.14
7 Njia ile hapana ndege mkali aijuaye, Wala jicho la tai halijaiona;
Job 11.6 Job 38.19 Job 28.21-28.23 Romains 11.33 Job 38.24
8 Wanyama wakali wajivunao hawajaikanyaga, Wala simba mkali hajaipita.
9 Huunyoshea mwamba wa gumegume mkono wake; Huipindua milima hata misingi yake.
Nahum 1.4-1.6
10 Hukata mifereji kati ya majabali; Na jicho lake huona kila kito cha thamani
Proverbes 14.23 Habakuk 3.9 Proverbes 24.4
11 Hufunga vijito visichuruzike; Na kitu kilichostirika hukifunua.
Esaïe 37.25 Esaïe 45.2-45.3 1 Corinthiens 4.5 Esaïe 44.27 Job 26.8
12 Bali hekima itapatikana wapi? Na mahali pa ufahamu ni wapi?
Job 28.20 Jacques 1.17 Jacques 1.5 1 Corinthiens 1.19-1.20 Ecclésiaste 7.23-7.25
13 Mwanadamu hajui thamani yake, Wala haionekani katika nchi ya walio hai.
Proverbes 3.14-3.15 Job 28.15-28.19 Esaïe 53.8 Esaïe 38.11 Proverbes 8.11
14 Vilindi vyasema, Haimo ndani yangu; Na bahari yasema, Haiko kwangu.
Romains 11.33-11.34
15 Haipatikani kwa dhahabu, Wala fedha haitapimwa iwe thamani yake.
Proverbes 16.16 Proverbes 8.19 Proverbes 3.13-3.15 Proverbes 8.10-8.11 Job 28.18
16 Haiwezi kutiwa thamani kwa dhahabu ya Ofiri, Wala kwa shohamu ya thamani nyingi, wala kwa yakuti ya samawi.
Psaumes 45.9 Esaïe 13.12 Ezéchiel 28.13 Exode 28.20 1 Chroniques 29.4
17 Dhahabu na vioo haviwezi kulinganishwa nayo; Wala kubadili kwake hakutakuwa kwa vyombo vya dhahabu safi.
Apocalypse 22.1 Ezéchiel 1.22 Proverbes 16.16 Apocalypse 21.11 Apocalypse 4.6
18 Havitatajwa fedhaluka wala bilauri; Naam, kima cha hekima chapita marijani.
Proverbes 3.15 Proverbes 31.10 Ezéchiel 27.16 Lamentations 4.7 Apocalypse 18.12
19 Yakuti ya rangi ya manjano ya Kushi haitasawazishwa nayo, Wala haitatiwa kima kwa dhahabu safi.
Exode 28.17 Exode 39.10 Ezéchiel 28.13 Apocalypse 21.20 Proverbes 8.19
20 Basi hekima yatoka wapi? Na mahali pa ufahamu ni wapi?
Jacques 1.5 Jacques 1.17 Job 28.12 Ecclésiaste 7.23-7.24 Proverbes 2.6
21 Kwa kuwa imefichwa mbali na macho ya wote walio hai, Na kusitirika na ndege wa angani.
Colossiens 2.3 Psaumes 49.3-49.4 Matthieu 13.35 1 Corinthiens 2.7-2.10 Matthieu 11.25
22 Uharibifu na Mauti husema, Tumesikia habari zake kwa masikio yetu.
Job 26.6 Job 28.14 Psaumes 83.10-83.12
23 Mungu ndiye aijuaye njia yake, Naye anajua mahali pake.
Proverbes 8.22-8.31 Proverbes 2.6 Romains 11.33 Matthieu 11.27 Luc 10.21-10.22
24 Maana anatazama hata miisho ya nchi, Na kuona chini ya mbingu nzima.
Proverbes 15.3 Zacharie 4.10 2 Chroniques 16.9 Apocalypse 5.6 Psaumes 33.13-33.14
25 Apate kuufanyia upepo uzito wake; Naam, anayapima maji kwa kipimo.
Psaumes 135.7 Esaïe 40.12 Job 12.15
26 Hapo alipoiwekea mvua amri, Na njia kwa umeme wa radi.
Job 38.25 Job 37.3 Jérémie 14.22 Zacharie 10.1 Job 36.26
27 Ndipo alipoiona na kuitangaza; Aliithibitisha, naam, na kuichunguza.
Proverbes 8.22-8.29 Psaumes 19.1
28 Kisha akamwambia mwanadamu, Tazama, kumcha Bwana ndiyo hekima, Na kujitenga na uovu ndio ufahamu.
Proverbes 1.7 Psaumes 111.10 Proverbes 9.10 Ecclésiaste 12.13 Deutéronome 4.6

Cette Bible est dans le domaine public.