Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

2 Chroniques 34.18
Bible en Swahili de l’est


Règne de Josias

1 Yosia alikuwa na umri wa miaka minane alipoanza kutawala; akatawala miaka thelathini na mmoja huko Yerusalemu.
Jérémie 1.2 Sophonie 1.1 1 Samuel 2.18 2 Chroniques 33.1 1 Rois 3.7-3.9
2 Akafanya yaliyo mema machoni pa Bwana, akaziendea njia za Daudi babaye, asigeuke kwa kuume wala kwa kushoto.
2 Chroniques 29.2 Deutéronome 17.11 Deutéronome 28.14 Deutéronome 5.32 2 Chroniques 17.3
3 Kwa kuwa katika mwaka wa nane wa kutawala kwake, naye akali mchanga, alianza kumtafuta Mungu wa Daudi babaye; hata katika mwaka wa kumi na mbili akaanza kusafisha Yuda na Yerusalemu kwa kuondoa mahali pa juu, na kwa kuondoa maashera, na sanamu za kuchora, nazo za kusubu.
2 Chroniques 15.2 2 Chroniques 33.22 2 Chroniques 33.17 Proverbes 8.17 Psaumes 119.9
4 Wakazibomoa madhabahu za mabaali machoni pake; na sanamu za jua, zilizoinuliwa juu yake, akazikata-kata; na maashera, na sanamu za kuchonga, nazo za kusubu, akazivunja-vunja, akaziponda kuwa mavumbi, akayamimina juu ya makaburi ya hao waliozichinjia dhabihu.
Exode 32.20 Lévitique 26.30 2 Rois 23.4-23.6 2 Chroniques 14.5 Deutéronome 7.25
5 Akaiteketeza mifupa ya makuhani madhabahuni mwao, akasafisha Yuda na Yerusalemu.
1 Rois 13.2 Ezéchiel 22.24 2 Rois 23.16 Jérémie 4.14 Jérémie 8.1-8.2
6 Na katika miji ya Manase, na Efraimu, na Simeoni, mpaka Naftali, akafanya vile vile; na katika maganjo yake pande zote.
Esaïe 7.25 2 Chroniques 30.1 2 Chroniques 31.1 2 Rois 23.15-23.20 2 Chroniques 30.10-30.11
7 Akazibomoa madhabahu, akaponda-ponda maashera na sanamu kuwa mavumbi, akazikata-kata sanamu zote za jua katika nchi yote ya Israeli, kisha akarejea Yerusalemu.
2 Chroniques 31.1 Deutéronome 9.21 2 Chroniques 34.1
8 Hata katika mwaka wa kumi na nane wa kutawala kwake, alipokwisha kuisafisha nchi, na nyumba, akamtuma Shafani, mwana wa Azalia, na Maaseya, akida wa mji, na Yoa, mwana wa Yoahazi, mwandishi wa tarehe, waitengeneze nyumba ya Bwana, Mungu wake.
2 Samuel 8.16 2 Chroniques 18.25 Jérémie 29.25 Jérémie 36.10 2 Rois 22.3-22.20
9 Wakamjia Hilkia kuhani mkuu, wakampa fedha, iliyoletwa nyumbani mwa Mungu, waliyoikusanya Walawi, wangoje mlango, mikononi mwa Manase na Efraimu, na mabaki yote ya Israeli, na Yuda yote na Benyamini, na wenyeji wa Yerusalemu.
2 Chroniques 35.8 2 Chroniques 30.18 2 Chroniques 30.10 2 Chroniques 34.18 2 Chroniques 24.11-24.14
10 Wakaitia mikononi mwa watenda kazi walioisimamia nyumba ya Bwana; na hao mafundi waliotenda kazi nyumbani mwa Bwana wakaitoa kwa kuitengeneza na kuifanya upya nyumba;
2 Rois 12.14 Esdras 3.7 2 Rois 12.11-12.12 2 Rois 22.5-22.6
11 wakawapa maseremala na waashi, ili wanunue mawe ya kuchonga, na miti ya kuungia, na kuifanyiza boriti kwa nyumba zile walizoziharibu wafalme wa Yuda.
2 Chroniques 33.4-33.7 2 Chroniques 33.22
12 Nao watu wakatenda kazi kwa uaminifu; na wasimamizi wao walikuwa Yahathi na Obadia, Walawi, wa wana wa Merari; na Zekaria na Meshulamu, wa wana wa Wakohathi, ili kuihimiza kazi; na wengine katika Walawi, wote waliokuwa wastadi wa kupiga vinanda.
2 Rois 12.15 1 Chroniques 23.5 Proverbes 28.20 1 Chroniques 16.41 1 Corinthiens 4.2
13 Tena walikuwa juu ya wachukuzi wa mizigo, wakawahimiza wote waliotenda kazi ya huduma yo yote; na miongoni mwa Walawi kulikuwa na waandishi, na wasimamizi, na mabawabu.
Néhémie 4.10 2 Chroniques 2.18 1 Chroniques 26.29-26.30 1 Chroniques 16.42 1 Chroniques 23.4-23.5
14 Nao walipotoa ile fedha iliyoletwa nyumbani mwa Bwana, Hilkia kuhani akakiona kitabu cha torati ya Bwana iliyotolewa kwa mkono wa Musa.
Jérémie 8.8 Josué 1.8 Lévitique 10.11 Esdras 7.10 2 Chroniques 31.4
15 Akajibu Hilkia akamwambia Shafani mwandishi, Kitabu cha torati nimekiona nyumbani mwa Bwana. Hilkia akampa Shafani kile kitabu.
16 Shafani akampelekea mfalme hicho kitabu, tena akampasha mfalme habari, akisema, Yote waliyokabidhiwa watumishi wako, wayafanya.
2 Rois 22.9-22.10 Jérémie 36.20-36.21
17 Nao wameimimina fedha iliyoonekana nyumbani mwa Bwana, nayo wameitia mikononi mwa wasimamizi, na mikononi mwa watenda kazi.
18 Shafani mwandishi akamweleza mfalme, akisema, Hilkia kuhani amenipa kitabu. Shafani akasoma ndani yake mbele ya mfalme.
Psaumes 119.97-119.99 Psaumes 119.46 Deutéronome 17.19 Josué 1.8 Jérémie 36.20-36.21
19 Ikawa, mfalme alipoyasikia maneno ya torati, aliyararua mavazi yake.
Josué 7.6 Jérémie 36.22-36.24 2 Rois 22.19 2 Rois 22.11 Galates 3.10-3.13
20 Mfalme akawaamuru Hilkia, na Ahikamu, mwana wa Shafani, na Abdoni, mwana wa Mika, na Shafani mwandishi, na Asaya, mtumishi wa mfalme, kusema,
2 Rois 22.12 Jérémie 26.22 2 Rois 25.22 Jérémie 40.6 Jérémie 26.24
21 Nendeni, mkamwulize Bwana kwa ajili yangu, na kwa hao waliosalia wa Israeli na wa Yuda, katika habari za maneno ya kitabu kilichoonekana; maana ghadhabu ya Bwana ni nyingi iliyomwagika juu yetu, kwa sababu baba zetu hawakulishika neno la Bwana, kutenda sawasawa na yote yaliyoandikwa kitabuni humo.
Jérémie 21.2 Ezéchiel 14.1-14.11 2 Chroniques 28.6 Lévitique 26.14-26.46 Deutéronome 31.16-31.22
22 Basi Hilkia, na hao waliotumwa na mfalme, wakamwendea Hulda nabii mke, mkewe Shalumu, mwana wa Tohathi, mwana wa Hasra, mtunza mavazi; (naye alikuwa akikaa Yerusalemu katika mtaa wa pili); wakasema naye kama hayo.
Exode 15.20 Luc 1.41-1.45 Juges 4.4 2 Rois 22.14 Actes 21.9
23 Akawaambia, Bwana, Mungu wa Israeli, asema hivi; Mwambieni mtu huyo aliyewatuma kwangu,
Jérémie 37.7-37.10 2 Rois 22.15-22.20 Jérémie 21.3-21.7
24 Bwana asema hivi, Angalia, nitaleta mabaya juu ya mahali hapa, na juu ya wakaao, laana zote zilizoandikwa katika kitabu hicho walichokisoma mbele ya mfalme wa Yuda;
2 Chroniques 36.14-36.20 Josué 23.16 Deutéronome 28.15-28.68 Esaïe 5.4-5.6 Jérémie 19.15
25 kwa sababu wameniacha mimi, na kuifukizia uvumba miungu mingine, ili wanikasirishe mimi kwa matendo yote ya mikono yao; kwa hiyo ghadhabu yangu imemwagika juu ya mahali hapa, wala isizimike.
Jérémie 7.20 Nahum 1.6 2 Chroniques 33.3-33.9 Ezéchiel 20.48 2 Chroniques 12.2
26 Lakini mfalme wa Yuda, aliyewatuma kumwuliza Bwana, mtamwambia hivi, Bwana, Mungu wa Israeli, asema hivi; Kwa habari ya maneno uliyoyasikia,
2 Chroniques 34.21 2 Chroniques 34.23
27 kwa kuwa moyo wako ulikuwa mwororo, nawe umejinyenyekeza mbele ya Mungu, uliposikia maneno yake juu ya mahali hapa, na juu ya wakaao, ukajinyenyekeza mbele zangu, na kuyararua mavazi yako, na kulia mbele zangu; mimi nami nimekusikia, asema Bwana.
2 Chroniques 32.26 Psaumes 10.17 Psaumes 51.17 Esaïe 65.24 Ezéchiel 9.4
28 Tazama, nitakukusanya kwa baba zako, nawe utawekwa kaburini mwako kwa amani, wala macho yako hayataona mabaya yote nitakayoyaleta juu ya mahali hapa, na juu ya wakaao. Basi wakamrudishia mfalme habari.
2 Chroniques 35.24 Ezéchiel 14.14-14.21 Jérémie 15.1 2 Rois 22.20 Psaumes 37.37
29 Ndipo mfalme akapeleka wajumbe, akawakusanya wazee wote wa Yuda na Yerusalemu.
2 Rois 23.1-23.3 2 Chroniques 30.2 1 Chroniques 29.2-29.9 Marc 14.8 1 Samuel 12.23
30 Akapanda mfalme nyumbani kwa Bwana, na watu wote wa Yuda, na wenyeji wa Yerusalemu, na makuhani na Walawi, na watu wote, wakubwa kwa wadogo; naye akasoma masikioni mwao maneno yote ya kitabu cha agano kilichoonekana nyumbani mwa Bwana.
2 Rois 23.2 Job 3.19 2 Chroniques 34.24 Néhémie 8.1-8.5 Deutéronome 1.17
31 Akasimama mfalme mahali pake, akafanya agano mbele za Bwana, kumfuata Bwana, na kuzishika amri zake, na shuhuda zake, na sheria zake, kwa moyo wake wote, na kwa roho yake yote, kuyatenda maneno ya agano yaliyoandikwa kitabuni humo.
2 Chroniques 23.16 2 Rois 23.3 2 Chroniques 15.12 2 Chroniques 6.13 2 Rois 11.14
32 Akawafanya wote walioonekana katika Yerusalemu na Benyamini walikubali. Na wenyeji wa Yerusalemu wakafanya sawasawa na agano la Mungu, Mungu wa baba zao.
2 Chroniques 14.4 Jérémie 3.10 2 Chroniques 30.12 Genèse 18.19 2 Chroniques 29.29
33 Naye Yosia akayaondolea mbali machukizo yote katika nchi zote zilizokuwa milki ya wana wa Israeli, akawafanya wote walioonekana katika Israeli kutumika, naam, wamtumikie Bwana, Mungu wao. Siku zake zote hawakuacha kumfuata Bwana, Mungu wa baba zao.
2 Chroniques 34.3-34.7 Osée 6.4 2 Rois 23.4-23.20 Josué 24.31 1 Rois 11.5-11.7

Cette Bible est dans le domaine public.