Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

2 Rois 6.5
Bible en Swahili de l’est


1 Kisha, wana wa manabii wakamwambia Elisha, Angalia basi, mahali tukaapo mbele yako ni padogo kwetu.
2 Rois 2.3 2 Rois 4.38 Josué 19.47 2 Rois 4.1 1 Rois 20.35
2 Basi twende mpaka Yordani, twakuomba, tutwae huko kila mtu mti mmoja, ili tujifanyie huko mahali pa kukaa. Akajibu, Haya! Nendeni.
1 Corinthiens 9.6 Actes 18.3 1 Timothée 6.6 Jean 21.3 Actes 20.34-20.35
3 Mmoja wao akasema, Uwe radhi, basi nakusihi, uende pamoja na watumishi wako. Akajibu, Nitakwenda.
Juges 4.8 Juges 19.6 2 Rois 5.23 Job 6.28
4 Basi, akaenda pamoja nao. Nao walipofika Yordani, wakakata miti.
Deutéronome 29.11 Deutéronome 19.5
5 Lakini mmojawapo alipokuwa katika kukata boriti, chuma cha shoka kikaanguka majini; akalia, akasema, Ole wangu! Bwana wangu, kwani kiliazimiwa kile.
Apocalypse 18.10 Ecclésiaste 10.10 Esaïe 10.34 Apocalypse 18.16 2 Rois 6.15
6 Mtu wa Mungu akasema, Kilianguka wapi? Akamwonyesha mahali. Akakata kijiti, akakitupa pale pale, chuma kikaelea.
2 Rois 2.21 Exode 15.25 2 Rois 4.41 Marc 7.33-7.34 Marc 8.23-8.25
7 Akasema, Kiokote. Basi akanyosha mkono, akakitwaa.
Luc 7.15 Exode 4.4 2 Rois 4.7 2 Rois 4.36 Actes 9.41
8 Basi, mfalme wa Shamu alikuwa akifanya vita na Israeli. Akafanya mashauri na watumishi wake, akasema, Kituo changu kitakuwapo mahali fulani.
Job 5.12-5.13 2 Rois 6.24 Esaïe 8.10 1 Rois 20.1 1 Rois 22.31
9 Yule mtu wa Mungu akapeleka habari kwa mfalme wa Israeli, kusema, Jihadhari, usipite mahali fulani; kwa sababu ndiko wanakoshukia Washami.
2 Rois 6.12 2 Rois 4.27 Apocalypse 1.1 1 Rois 20.13 2 Rois 3.17-3.19
10 Mfalme wa Israeli akapeleka watu mpaka mahali pale alipoambiwa na yule mtu wa Mungu, na kuhadharishwa; akajiokoa nafsi yake, si mara moja, wala si mara mbili.
Matthieu 3.7 2 Chroniques 20.20 2 Rois 13.14 Matthieu 2.12 1 Rois 20.15
11 Basi mfalme wa Shamu moyo wake ukamfadhaika sana kwa ajili ya jambo hili; akawaita watumishi wake, akawaambia, Je! Hamtanionyesha, ni mtu yupi miongoni mwenu aliye upande wa mfalme wa Israeli?
1 Samuel 22.8 Psaumes 48.4-48.5 Matthieu 2.3-2.12 Job 18.7-18.11 Esaïe 57.20-57.21
12 Mmojawapo wa watumishi wake akasema, La, bwana wangu, mfalme; lakini Elisha, yule nabii aliye katika Israeli, humwambia mfalme wa Israeli maneno uyanenayo katika chumba chako cha kulala.
Daniel 2.28-2.30 Ecclésiaste 10.20 Daniel 4.9-4.18 2 Rois 5.8 2 Rois 5.3
13 Akasema, Enendeni, mkamwangalie aliko, nipate kupeleka watu kwenda kumchukua. Akaambiwa ya kwamba, Tazama, yuko Dothani.
Genèse 37.17 Psaumes 10.8-10.10 Jérémie 36.26 Psaumes 37.32-37.33 Actes 23.12-23.27
14 Kwa hiyo akapeleka huko farasi, na magari, na jeshi kubwa; wakafika usiku, wakauzingira mji ule pande zote.
2 Rois 18.17 Matthieu 26.47 2 Rois 1.9-1.13 Jean 18.3-18.6 Matthieu 26.55
15 Hata asubuhi na mapema mtumishi wake yule mtu wa Mungu alipoondoka, na kwenda nje, kumbe! Pana jeshi la watu, na farasi na magari, wameuzingira mji ule. Mtumishi wake akamwambia, Ole wetu! Bwana wangu, tufanyeje?
Matthieu 8.26 Exode 24.13 2 Chroniques 20.12 2 Rois 3.11 2 Rois 5.20
16 Akamjibu, Usiogope; maana walio pamoja nasi ni wengi kuliko wale walio pamoja nao.
Esaïe 41.10-41.14 Romains 8.31 Psaumes 55.18 1 Jean 4.4 2 Chroniques 32.7-32.8
17 Elisha akaomba, akasema, Ee Bwana, nakusihi, mfumbue macho yake, apate kuona. Bwana akamfumbua macho yule mtumishi; naye akaona; na tazama, kile kilima kilikuwa kimejaa farasi na magari ya moto yaliyomzunguka Elisha pande zote.
2 Rois 2.11 Psaumes 68.17 Zacharie 6.1-6.7 Psaumes 34.7 Hébreux 1.14
18 Na walipomtelemkia Elisha akamwomba Bwana, akasema, Uwapige, nakusihi, watu hawa kwa upofu. Akawapiga kwa upofu sawasawa na neno la Elisha.
Actes 13.11 Genèse 19.11 Job 5.14 Jean 12.40 Deutéronome 28.28
19 Elisha akawaambia, Njia hii siyo, na mji huu sio, nifuateni mimi, nami nitawapeleka kwa mtu yule mnayemtafuta. Akawapeleka Samaria.
2 Samuel 16.18-16.19 Marc 8.34 Luc 24.16 Luc 9.23 Matthieu 16.24
20 Hata walipokwisha kuingia Samaria, Elisha akasema, Bwana wafumbue macho watu hawa, wapate kuona. Bwana akawafumbua macho wakaona; kumbe! Walikuwa katikati ya Samaria.
2 Rois 6.17 Luc 16.23 Juges 20.40-20.42 Luc 24.31
21 Naye mfalme wa Israeli alipowaona, akamwambia Elisha, Ee baba yangu, niwapige? Niwapige?
2 Rois 5.13 2 Rois 8.9 2 Rois 2.12 Luc 22.49 Luc 9.54-9.56
22 Akamjibu, Usiwapige; je! Ungetaka kuwapiga watu ambao umewatwaa mateka kwa upanga wako na uta wako? Weka chakula na maji mbele yao, wapate kula na kunywa, na kwenda kwa bwana wao.
Genèse 48.22 Osée 2.18 Romains 12.20-12.21 2 Chroniques 28.8-28.15 Josué 24.12
23 Basi akawaandalia chakula tele; nao walipokwisha kula na kunywa, akawaacha, wakaenda zao kwa bwana wao. Na vikosi vya Shamu havikuja tena katika nchi ya Israeli.
2 Rois 5.2 2 Rois 24.2 2 Rois 6.8-6.9 1 Samuel 24.17-24.18 Matthieu 5.47

Siège et délivrance de Samarie

24 Ikawa baada ya hayo, Ben-hadadi mfalme wa Shamu akakusanya majeshi yake yote, akakwea akauhusuru Samaria.
1 Rois 20.1 Deutéronome 28.52 2 Rois 18.9 1 Rois 22.31 Ecclésiaste 9.14
25 Njaa ikawa kuu huko Samaria; na tazama, wakauhusuru, hata kichwa cha punda kikapata kuuzwa kwa vipande themanini vya fedha, na kibaba cha mavi ya njiwa kwa vipande vitano vya fedha.
2 Rois 6.28-6.29 2 Rois 7.4 Jérémie 14.13-14.15 Lévitique 26.26 2 Rois 25.3
26 Ikawa mfalme wa Israeli alipokuwa akipita ukutani, mwanamke mmoja akamwita akisema, Unisaidie, bwana wangu, mfalme.
2 Samuel 14.4 Esaïe 10.3 Luc 18.3 Actes 21.28
27 Akasema, Bwana asipokusaidia, nikusaidieje mimi? Ya sakafuni, au ya shinikizoni?
Psaumes 127.1 Psaumes 118.8-118.9 Esaïe 2.2 Psaumes 124.1-124.3 Psaumes 146.3
28 Mfalme akamwambia, Una nini? Akajibu, Mwanamke huyu aliniambia, Mtoe mtoto wako, tumle leo, na mtoto wangu tutamla kesho.
Juges 18.23 2 Samuel 14.5 Lamentations 4.10 Esaïe 49.15 1 Samuel 1.8
29 Basi, tukamtokosa mtoto wangu, tukamla; nikamwambia siku ya pili, Mtoe mtoto wako, tumle; naye amemficha mtoto wake.
Lévitique 26.29 Deutéronome 28.53 Deutéronome 28.57 Esaïe 66.13 Esaïe 49.15
30 Ikawa, mfalme alipoyasikia maneno ya huyo mwanamke, aliyararua mavazi yake; (naye alikuwa akipita juu ya ukuta;) na watu wakaona, na tazama, alikuwa amevaa magunia ndani mwilini mwake.
1 Rois 21.27 Esaïe 58.5-58.7 2 Rois 5.7 2 Rois 19.1
31 Ndipo akasema, Mungu anifanyie hivyo, na kuzidi, kikimbakia kichwa Elisha mwana wa Shafati juu yake leo.
1 Rois 19.2 Ruth 1.17 1 Rois 18.17 2 Samuel 19.13 Actes 23.12-23.13
32 Lakini Elisha alikuwa akikaa nyumbani mwake, na wazee wakikaa pamoja naye; na mfalme akamtuma mtu wa mbele yake; lakini hata kabla ya kufika kwake yule aliyetumwa, akawaambia wazee, Je! Mwaona jinsi huyu mwana wa mwuaji alivyotuma aniondolee kichwa changu? Angalieni, huyo aliyetumwa akifika, fungeni mlango, mkamzuie mlangoni; je! Sauti ya miguu ya bwana wake haiko nyuma yake?
Ezéchiel 20.1 1 Rois 18.4 Ezéchiel 8.1 Ezéchiel 14.1 1 Rois 21.10
33 Hata alipokuwa katika kusema nao, tazama, yule aliyetumwa akamshukia; naye akasema, Angalia, mabaya haya yatoka kwa Bwana; kwani mimi kumngojea Bwana tena?
Job 2.9 Esaïe 8.21 Esaïe 26.3 Psaumes 27.14 Luc 18.1

Cette Bible est dans le domaine public.