Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

2 Rois 6.25
Bible en Swahili de l’est


1 Kisha, wana wa manabii wakamwambia Elisha, Angalia basi, mahali tukaapo mbele yako ni padogo kwetu.
2 Rois 2.3 2 Rois 4.38 Esaïe 54.2-54.3 Josué 17.14 1 Samuel 19.20
2 Basi twende mpaka Yordani, twakuomba, tutwae huko kila mtu mti mmoja, ili tujifanyie huko mahali pa kukaa. Akajibu, Haya! Nendeni.
Jean 21.3 Actes 20.34-20.35 1 Thessaloniciens 2.9 2 Thessaloniciens 3.8 1 Corinthiens 9.6
3 Mmoja wao akasema, Uwe radhi, basi nakusihi, uende pamoja na watumishi wako. Akajibu, Nitakwenda.
Juges 4.8 Juges 19.6 2 Rois 5.23 Job 6.28
4 Basi, akaenda pamoja nao. Nao walipofika Yordani, wakakata miti.
Deutéronome 29.11 Deutéronome 19.5
5 Lakini mmojawapo alipokuwa katika kukata boriti, chuma cha shoka kikaanguka majini; akalia, akasema, Ole wangu! Bwana wangu, kwani kiliazimiwa kile.
Apocalypse 18.10 Exode 22.14-22.15 2 Rois 4.7 2 Rois 3.10 Ecclésiaste 10.10
6 Mtu wa Mungu akasema, Kilianguka wapi? Akamwonyesha mahali. Akakata kijiti, akakitupa pale pale, chuma kikaelea.
2 Rois 2.21 Exode 15.25 2 Rois 4.41 Jean 9.6-9.7 Marc 7.33-7.34
7 Akasema, Kiokote. Basi akanyosha mkono, akakitwaa.
Exode 4.4 2 Rois 4.7 2 Rois 4.36 Actes 9.41 Luc 7.15
8 Basi, mfalme wa Shamu alikuwa akifanya vita na Israeli. Akafanya mashauri na watumishi wake, akasema, Kituo changu kitakuwapo mahali fulani.
1 Rois 20.34 Proverbes 20.18 1 Rois 20.23 Proverbes 21.30 Job 5.12-5.13
9 Yule mtu wa Mungu akapeleka habari kwa mfalme wa Israeli, kusema, Jihadhari, usipite mahali fulani; kwa sababu ndiko wanakoshukia Washami.
1 Rois 20.13 2 Rois 3.17-3.19 1 Rois 20.28 Amos 3.7 2 Rois 6.12
10 Mfalme wa Israeli akapeleka watu mpaka mahali pale alipoambiwa na yule mtu wa Mungu, na kuhadharishwa; akajiokoa nafsi yake, si mara moja, wala si mara mbili.
Actes 27.24 2 Rois 2.12 Ezéchiel 3.18-3.21 2 Rois 5.14 Amos 7.1-7.6
11 Basi mfalme wa Shamu moyo wake ukamfadhaika sana kwa ajili ya jambo hili; akawaita watumishi wake, akawaambia, Je! Hamtanionyesha, ni mtu yupi miongoni mwenu aliye upande wa mfalme wa Israeli?
Matthieu 2.3-2.12 Job 18.7-18.11 Esaïe 57.20-57.21 1 Samuel 28.21 1 Samuel 22.8
12 Mmojawapo wa watumishi wake akasema, La, bwana wangu, mfalme; lakini Elisha, yule nabii aliye katika Israeli, humwambia mfalme wa Israeli maneno uyanenayo katika chumba chako cha kulala.
Daniel 2.28-2.30 Daniel 2.47 Daniel 2.22-2.23 2 Rois 6.9-6.10 Jérémie 23.23-23.24
13 Akasema, Enendeni, mkamwangalie aliko, nipate kupeleka watu kwenda kumchukua. Akaambiwa ya kwamba, Tazama, yuko Dothani.
Genèse 37.17 1 Samuel 23.22-23.23 Psaumes 37.12-37.14 Matthieu 2.4-2.8 Psaumes 10.8-10.10
14 Kwa hiyo akapeleka huko farasi, na magari, na jeshi kubwa; wakafika usiku, wakauzingira mji ule pande zote.
Jean 18.3-18.6 Matthieu 26.55 1 Samuel 24.2 1 Samuel 23.26 2 Rois 18.17
15 Hata asubuhi na mapema mtumishi wake yule mtu wa Mungu alipoondoka, na kwenda nje, kumbe! Pana jeshi la watu, na farasi na magari, wameuzingira mji ule. Mtumishi wake akamwambia, Ole wetu! Bwana wangu, tufanyeje?
Matthieu 8.26 Matthieu 20.26-20.28 Actes 13.5 1 Rois 19.21 2 Rois 5.27
16 Akamjibu, Usiogope; maana walio pamoja nasi ni wengi kuliko wale walio pamoja nao.
Esaïe 41.10-41.14 Romains 8.31 Psaumes 55.18 1 Jean 4.4 2 Chroniques 32.7-32.8
17 Elisha akaomba, akasema, Ee Bwana, nakusihi, mfumbue macho yake, apate kuona. Bwana akamfumbua macho yule mtumishi; naye akaona; na tazama, kile kilima kilikuwa kimejaa farasi na magari ya moto yaliyomzunguka Elisha pande zote.
2 Rois 2.11 Zacharie 6.1-6.7 Psaumes 68.17 Hébreux 1.14 Psaumes 34.7
18 Na walipomtelemkia Elisha akamwomba Bwana, akasema, Uwapige, nakusihi, watu hawa kwa upofu. Akawapiga kwa upofu sawasawa na neno la Elisha.
Actes 13.11 Genèse 19.11 Romains 11.7 Jean 9.39 Zacharie 12.4
19 Elisha akawaambia, Njia hii siyo, na mji huu sio, nifuateni mimi, nami nitawapeleka kwa mtu yule mnayemtafuta. Akawapeleka Samaria.
Marc 8.34 Luc 24.16 Luc 9.23 Matthieu 16.24 2 Samuel 16.18-16.19
20 Hata walipokwisha kuingia Samaria, Elisha akasema, Bwana wafumbue macho watu hawa, wapate kuona. Bwana akawafumbua macho wakaona; kumbe! Walikuwa katikati ya Samaria.
2 Rois 6.17 Luc 16.23 Juges 20.40-20.42 Luc 24.31
21 Naye mfalme wa Israeli alipowaona, akamwambia Elisha, Ee baba yangu, niwapige? Niwapige?
2 Rois 5.13 2 Rois 8.9 2 Rois 2.12 2 Rois 13.14 1 Samuel 24.19
22 Akamjibu, Usiwapige; je! Ungetaka kuwapiga watu ambao umewatwaa mateka kwa upanga wako na uta wako? Weka chakula na maji mbele yao, wapate kula na kunywa, na kwenda kwa bwana wao.
Genèse 48.22 Osée 1.7 Matthieu 5.44 Proverbes 25.21-25.22 Psaumes 44.6
23 Basi akawaandalia chakula tele; nao walipokwisha kula na kunywa, akawaacha, wakaenda zao kwa bwana wao. Na vikosi vya Shamu havikuja tena katika nchi ya Israeli.
2 Rois 5.2 2 Rois 24.2 2 Rois 6.8-6.9 Luc 6.35 Proverbes 25.21-25.22

Siège et délivrance de Samarie

24 Ikawa baada ya hayo, Ben-hadadi mfalme wa Shamu akakusanya majeshi yake yote, akakwea akauhusuru Samaria.
1 Rois 20.1 Deutéronome 28.52 2 Rois 17.5 2 Rois 25.1 2 Rois 18.9
25 Njaa ikawa kuu huko Samaria; na tazama, wakauhusuru, hata kichwa cha punda kikapata kuuzwa kwa vipande themanini vya fedha, na kibaba cha mavi ya njiwa kwa vipande vitano vya fedha.
Jérémie 14.18 Jérémie 32.24 Ezéchiel 4.13-4.16 Jérémie 52.6 2 Rois 6.28-6.29
26 Ikawa mfalme wa Israeli alipokuwa akipita ukutani, mwanamke mmoja akamwita akisema, Unisaidie, bwana wangu, mfalme.
2 Samuel 14.4 Esaïe 10.3 Luc 18.3 Actes 21.28
27 Akasema, Bwana asipokusaidia, nikusaidieje mimi? Ya sakafuni, au ya shinikizoni?
Psaumes 146.3 Psaumes 62.8 Jérémie 17.5 Psaumes 60.11 Psaumes 127.1
28 Mfalme akamwambia, Una nini? Akajibu, Mwanamke huyu aliniambia, Mtoe mtoto wako, tumle leo, na mtoto wangu tutamla kesho.
2 Samuel 14.5 Lamentations 4.10 Juges 18.23 Luc 23.29 Matthieu 24.18-24.21
29 Basi, tukamtokosa mtoto wangu, tukamla; nikamwambia siku ya pili, Mtoe mtoto wako, tumle; naye amemficha mtoto wake.
Lévitique 26.29 Deutéronome 28.53 Deutéronome 28.57 Esaïe 49.15 1 Rois 3.26
30 Ikawa, mfalme alipoyasikia maneno ya huyo mwanamke, aliyararua mavazi yake; (naye alikuwa akipita juu ya ukuta;) na watu wakaona, na tazama, alikuwa amevaa magunia ndani mwilini mwake.
1 Rois 21.27 Esaïe 58.5-58.7 2 Rois 5.7 2 Rois 19.1
31 Ndipo akasema, Mungu anifanyie hivyo, na kuzidi, kikimbakia kichwa Elisha mwana wa Shafati juu yake leo.
1 Rois 19.2 Ruth 1.17 1 Samuel 3.17 2 Samuel 3.35 Jean 11.50
32 Lakini Elisha alikuwa akikaa nyumbani mwake, na wazee wakikaa pamoja naye; na mfalme akamtuma mtu wa mbele yake; lakini hata kabla ya kufika kwake yule aliyetumwa, akawaambia wazee, Je! Mwaona jinsi huyu mwana wa mwuaji alivyotuma aniondolee kichwa changu? Angalieni, huyo aliyetumwa akifika, fungeni mlango, mkamzuie mlangoni; je! Sauti ya miguu ya bwana wake haiko nyuma yake?
1 Rois 18.4 Ezéchiel 8.1 Ezéchiel 14.1 Ezéchiel 20.1 1 Rois 18.13-18.14
33 Hata alipokuwa katika kusema nao, tazama, yule aliyetumwa akamshukia; naye akasema, Angalia, mabaya haya yatoka kwa Bwana; kwani mimi kumngojea Bwana tena?
Job 2.9 Esaïe 8.21 Esaïe 50.10 Proverbes 19.3 Lamentations 3.25-3.26

Cette Bible est dans le domaine public.