Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

2 Rois 5.15
Bible en Swahili de l’est


1 Basi Naamani, jemadari wa jeshi la mfalme wa Shamu, alikuwa mtu mkubwa mbele ya bwana wake, na mwenye kuheshimiwa, kwa sababu kwa mkono wake Bwana alikuwa amewapa Washami kushinda; tena alikuwa mtu hodari wa vita; lakini alikuwa mwenye ukoma.
Luc 4.27 Nombres 12.10-12.12 Proverbes 21.31 Esther 9.4 Jérémie 27.5-27.6
2 Na Washami walikuwa wametoka vikosi, wakachukua mfungwa mmoja kijana mwanamke kutoka nchi ya Israeli; naye akamhudumia mkewe Naamani.
2 Rois 6.23 2 Rois 13.20 Juges 9.34 Psaumes 123.2 1 Samuel 13.17-13.18
3 Akamwambia bibi yake, Laiti bwana wangu angekuwa pamoja na yule nabii aliyeko Samaria! Maana angemponya ukoma wake.
Matthieu 11.5 Luc 17.12-17.14 Actes 26.29 Nombres 11.29 1 Corinthiens 4.8
4 Mtu mmoja akaingia, akamwambia bwana wake, akasema, Yule kijana mwanamke aliyetoka nchi ya Israeli asema hivi na hivi.
Marc 16.9-16.10 Marc 5.19 2 Rois 7.9-7.11 1 Corinthiens 1.26-1.27 Jean 1.42-1.46
5 Mfalme wa Shamu akasema, Haya! Basi, mimi nitampelekea mfalme wa Israeli waraka. Basi akaenda zake, akachukua mikononi mwake talanta kumi za fedha, na vipande vya dhahabu elfu sita, na mavazi kumi.
Juges 14.12 2 Rois 8.8-8.9 Jacques 4.13 Jacques 5.1-5.3 Genèse 11.3
6 Akampelekea mfalme wa Israeli waraka ule, kusema, Waraka huu utakapokuwasilia, tazama, nimemtuma mtumishi wangu Naamani kwako, ili upate kumponya ukoma wake.
7 Ikawa, mfalme wa Israeli alipousoma waraka, alirarua mavazi yake, akasema, Je! Mimi ni Mungu, niue na kuhuisha, hata mtu huyu akanipelekea mtu nimponye ukoma wake? Fahamuni, basi, nakusihini, mwone ya kuwa mtu huyu anataka kugombana nami.
1 Samuel 2.6 Genèse 30.2 1 Rois 20.7 Luc 11.54 Deutéronome 32.39
8 Ikawa, Elisha, yule mtu wa Mungu, aliposikia kwamba mfalme wa Israeli ameyararua mavazi yake, ndipo akatuma mtu kwa mfalme, akisema, Mbona umeyararua mavazi yako? Na aje sasa kwangu mimi, naye atajua ya kuwa yuko nabii katika Israeli.
2 Rois 5.7 1 Rois 17.24 2 Samuel 3.31 Exode 11.8 Romains 11.13
9 Basi Naamani akaja na farasi wake na magari yake, akasimama mlangoni pa nyumba ya Elisha.
Esaïe 60.14 2 Rois 6.32 Actes 16.37-16.39 2 Rois 3.12 Actes 16.29-16.30
10 Naye Elisha akampelekea mjumbe, akisema, Enenda ukaoge katika Yordani mara saba, na nyama ya mwili wako itakurudia, nawe utakuwa safi.
Jean 9.7 Lévitique 14.7 Nombres 19.19 Lévitique 16.19 Lévitique 16.14
11 Lakini Naamani akakasirika, akaondoka, akasema, Tazama, nalidhania, Bila shaka atatoka kwangu, na kusimama, na kuomba kwa jina la Bwana, Mungu wake, na kupitisha mkono wake mahali penye ugonjwa, na kuniponya mimi mwenye ukoma.
Proverbes 13.10 Proverbes 1.32 Matthieu 15.27 1 Corinthiens 3.18-3.20 1 Corinthiens 2.14-2.16
12 Je! Abana na Farpari, mito ya Dameski, si bora kuliko maji yote ya Israeli? Je! Siwezi kujiosha ndani yake, na kuwa safi? Akageuka, akaondoka kwa hasira.
Proverbes 14.17 Zacharie 14.8 Proverbes 19.11 Zacharie 13.1 Marc 1.9
13 Watumishi wake wakamkaribia, wakamwambia, wakasema, Baba yangu, kama yule nabii angalikuambia kutenda jambo kubwa, usingalilitenda? Je! Si zaidi basi, akikuambia, Jioshe, uwe safi?
2 Rois 6.21 2 Rois 2.12 2 Rois 13.14 Apocalypse 7.14 Psaumes 51.7
14 Ndipo akashuka, akajichovya mara saba katika Yordani, sawasawa na neno lake yule mtu wa Mungu; nayo nyama ya mwili wake ikarudi ikawa kama nyama ya mwili wa mtoto mchanga, akawa safi.
Job 33.25 Luc 4.27 2 Rois 5.10 Luc 5.13 Zacharie 14.8
15 Akamrudia yule mtu wa Mungu, yeye na mafuatano yake yote. Akaja, akasimama mbele yake; akasema, Sasa tazama, najua ya kwamba hakuna Mungu duniani mwote, ila katika Israeli; basi nakuomba upokee mbaraka kwa mtumwa wako.
Daniel 2.47 1 Samuel 25.27 2 Rois 5.8 Daniel 6.26-6.27 Daniel 3.29
16 Lakini akasema, Kama Bwana aishivyo, ambaye nimesimama mbele yake, sipokei kitu. Akamshurutisha apokee; lakini akakataa.
2 Rois 5.20 2 Rois 3.14 2 Rois 5.26 Daniel 5.17 1 Rois 17.1
17 Naamani akasema; Kama sivyo, lakini mtumwa wako na apewe mzigo wa udongo wa baghala wawili; kwa maana mtumwa wako hatatoa tena sadaka ya kuteketezwa wala dhabihu kwa miungu mingine, ila kwa Bwana.
Exode 20.24 1 Pierre 4.3 1 Thessaloniciens 1.9 Romains 14.1 2 Rois 5.12
18 Jambo hili Bwana amwachilie mtumwa wako; bwana wangu akiingia nyumbani mwa Rimoni ili aabudu humo, naye akitegemea mkononi mwangu, nami nikijiinama nyumbani mwa Rimoni, hapo ninapojiinama nyumbani mwa Rimoni, Bwana amwachilie mtumwa wako jambo hili.
2 Rois 7.2 2 Rois 7.17 2 Rois 17.35 1 Rois 19.18 Exode 20.5
19 Akamwambia, Enenda kwa amani Basi akamwondokea mbali kidogo.
1 Samuel 1.17 Exode 4.18 Marc 5.34 Matthieu 9.16-9.17 Genèse 35.16
20 Lakini Gehazi, mtumishi wa Elisha mtu wa Mungu, akasema, Tazama, bwana wangu amemwachilia huyo Naamani Mshami, asivipokee mikononi mwake vile vitu alivyovileta; kama Bwana aishivyo, mimi nitamfuata mbio, nipokee kitu kwake.
2 Rois 4.12 Exode 20.7 2 Rois 4.31 2 Rois 4.36 2 Rois 6.31
21 Basi Gehazi akamfuata Naamani. Naye Naamani, alipoona mtu apigaye mbio anakuja nyuma yake, alishuka garini amlaki, akasema, Je! Ni amani?
2 Rois 4.26 Actes 8.31 Actes 10.25-10.26 2 Rois 9.17-9.22 Luc 7.6-7.7
22 Akasema, Amani. Bwana wangu amenituma, kusema, Tazama, sasa hivi wamenijia kutoka milimani mwa Efraimu vijana wawili wa wana na manabii; uwape, nakuomba, talanta ya fedha, na mavazi mawili.
2 Rois 5.5 Josué 24.33 Actes 5.3-5.4 Jean 8.44 1 Rois 13.18
23 Naamani akasema, Uwe radhi, ukatwae talanta mbili. Akamshurutisha, akafunga talanta mbili za fedha ndani ya mifuko miwili, na mavazi mawili, akawatwika watumishi wake wawili; nao wakayachukua mbele yake.
1 Rois 20.7 2 Rois 12.10 2 Rois 2.17 2 Rois 6.3 Esaïe 30.6
24 Naye alipofika kilimani, alivitwaa mikononi mwao, akaviweka nyumbani; akawaacha wale watu kuondoka, nao wakaenda zao.
Josué 7.1 1 Rois 21.16 Josué 7.11-7.12 Josué 7.21 Zacharie 5.3-5.4
25 Lakini yeye akaingia, akasimama mbele ya bwana wake. Elisha akamwambia, Watoka wapi, Gehazi? Akanena, Mtumwa wako hakuenda mahali.
2 Rois 5.22 Genèse 4.9 Genèse 3.8-3.9 Matthieu 26.21 Ezéchiel 33.31
26 Akamwambia, Je! Moyo wangu haukuenda na wewe, hapo alipogeuka yule mtu katika gari ili akulaki? Je! Huu ndio wakati wa kupokea fedha, na kupokea mavazi, na mashamba ya mizeituni, na mizabibu, na kondoo, na ng’ombe, na watumwa, na wajakazi?
2 Rois 5.16 Psaumes 63.11 Ecclésiaste 3.1-3.8 Colossiens 2.5 Actes 20.35
27 Basi ukoma wa Naamani utakushika wewe, na wazao wako hata milele. Naye akatoka usoni pake mwenye ukoma kama theluji.
Exode 4.6 Nombres 12.10 2 Rois 15.5 Matthieu 27.3-27.5 1 Timothée 6.10

Cette Bible est dans le domaine public.