Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

1 Rois 16.18
Bible en Swahili de l’est


1 Ndipo neno la Bwana likamjia Yehu mwana wa Hanani juu ya Baasha, kusema,
2 Chroniques 20.34 2 Chroniques 19.2 1 Rois 16.7 2 Chroniques 16.7-16.10 1 Rois 15.33
2 Kwa kuwa mimi nilikuinua kutoka katika mavumbi, na kukufanya uwe mkuu juu ya watu wangu Israeli; nawe umeiendea njia ya Yeroboamu, na kuwakosesha watu wangu Israeli, hata wanighadhibishe kwa makosa yao;
1 Rois 15.34 1 Rois 14.7 1 Samuel 2.8 Psaumes 113.7-113.8 1 Samuel 26.19
3 angalia, kuondoa nitawaondoa Baasha na jamaa yake; tena nitaifanya nyumba yako iwe kama nyumba ya Yeroboamu mwana wa Nebati.
1 Rois 14.10 Esaïe 66.24 1 Rois 15.29-15.30 Jérémie 22.19 1 Rois 21.21-21.24
4 Mtu amfiaye Baasha mjini mbwa watamla; naye amfiaye mashambani ndege wa angani watamla.
1 Rois 14.11 1 Rois 21.24
5 Basi, mambo yote ya Baasha yaliyosalia, na aliyoyafanya, na nguvu zake, je! Hayakuandikwa katika kitabu-cha-tarehe cha wafalme wa Israeli?
1 Rois 14.19 1 Rois 15.31 2 Chroniques 16.1-16.6
6 Baasha akalala na babaze, akazikwa katika Tirza; naye Ela mwanawe akatawala mahali pake.
1 Rois 14.17 1 Rois 15.21 1 Rois 16.13-16.14 1 Rois 14.20 1 Rois 15.25
7 Tena neno la Bwana likaja kwa mkono wa nabii Yehu mwana wa Hanani juu ya Baasha, na juu ya nyumba yake, kwa sababu ya mabaya yote aliyoyatenda machoni pa Bwana, akimghadhibisha kwa kazi ya mikono yake, kwa kufanana na nyumba ya Yeroboamu, na kwa sababu aliiharibu.
1 Rois 14.14 Psaumes 115.4 Osée 1.4 Esaïe 2.8 Actes 4.27-4.28

Règne d’Éla sur Israël

8 Katika mwaka wa ishirini na sita wa Asa mfalme wa Yuda, Ela mwana wa Baasha alianza kutawala juu ya Israeli huko Tirza, akatawala miaka miwili.
9 Na mtumwa wake Zimri, jemadari wa nusu ya magari yake, akamfanyia fitina; alipokuwako Tirza akinywa hata kulewa nyumbani mwa Arsa, aliyekuwa juu ya nyumba huko Tirza;
Genèse 24.2 Genèse 39.4 1 Rois 18.3 Jérémie 51.57 1 Rois 15.27
10 Zimri akaingia akampiga, akamwua, katika mwaka wa ishirini na saba wa Asa mfalme wa Yuda, akatawala mahali pake.
2 Rois 9.31
11 Ikawa, alipoanza kutawala, mara alipoketi juu ya kiti chake cha enzi, akawaua nyumba yote ya Baasha; hakumwachia mwanamume ye yote, wa jamaa zake, wala wa rafiki zake.
1 Rois 15.29 1 Samuel 25.22 1 Rois 16.3 1 Samuel 25.34 1 Rois 14.10
12 Hivyo Zimri akaiharibu nyumba yote ya Baasha, sawasawa na neno la Bwana, alilolinena juu ya Baasha kwa Yehu nabii,
1 Rois 16.1 1 Rois 16.3 Proverbes 26.6 2 Chroniques 10.15 2 Rois 14.25
13 kwa sababu ya makosa yake Baasha, na makosa yote ya Ela mwanawe, waliyoyakosa, na kuwakosesha Israeli, wakimghadhibisha Bwana, Mungu wa Israeli, kwa matendo yao ya ubatili.
Deutéronome 32.21 Esaïe 41.29 1 Samuel 12.21 1 Rois 15.30 1 Corinthiens 8.4
14 Na mambo yote ya Ela yaliyosalia, na yote aliyoyafanya, je! Hayakuandikwa katika kitabu-cha-tarehe cha wafalme wa Israeli?

Règne de Zimri sur Israël

15 Katika mwaka wa ishirini na saba wa Asa mfalme wa Yuda, Zimri akatawala muda wa siku saba huko Tirza. Basi, watu walikuwa wametua maragoni kupigana na Gibethoni, ulio wa Wafilisti.
1 Rois 15.27 Josué 19.44 Josué 21.23 Psaumes 37.35 Job 20.5
16 Na hao watu waliokuwako maragoni wakasikia habari ya kwamba Zimri amefanya fitina, tena amempiga mfalme; kwa hiyo Israeli wote wakamfanya Omri, jemadari wa jeshi, awe mfalme juu ya Israeli siku ile maragoni.
2 Rois 8.26 Michée 6.16 2 Chroniques 22.2 1 Rois 16.30
17 Omri akapanda kutoka Gibethoni, na Israeli wote pamoja naye, wakauhusuru Tirza.
2 Rois 6.24-6.25 2 Rois 25.1-25.4 Juges 9.56-9.57 Juges 9.45 Luc 19.43-19.44
18 Ikawa Zimri alipoona ya kuwa mji umetwaliwa, akaingia ngomeni mwa nyumba ya mfalme, akaiteketeza nyumba ya mfalme juu yake kwa moto, akafa;
2 Samuel 17.23 1 Samuel 31.4-31.5 Juges 9.54 Job 2.9-2.10 Matthieu 27.5
19 kwa sababu ya makosa aliyoyakosa, akifanya mabaya machoni pa Bwana, kwa kuiendea njia ya Yeroboamu na makosa yake aliyoyafanya akiwakosesha Israeli.
1 Rois 15.26 1 Rois 12.28 1 Rois 15.34 1 Rois 14.16 Psaumes 58.9-58.11
20 Na mambo yote ya Zimri yaliyosalia na fitina yake aliyoifanya, je! Hayakuandikwa katika kitabu-cha-tarehe cha wafalme wa Israeli?
1 Rois 16.5 1 Rois 16.27 1 Rois 16.14 1 Rois 14.19 1 Rois 22.39
21 Ndipo watu wa Israeli wakatengwa sehemu mbili; nusu ya watu wakamfuata Tibni mwana wa Ginathi, ili wamfanye mfalme; nusu wakamfuata Omri.
Esaïe 19.2 1 Rois 16.29 1 Rois 15.28 Matthieu 12.25 Esaïe 9.18-9.21
22 Lakini hao watu waliomfuata Omri wakawashinda watu waliomfuata Tibni mwana wa Ginathi; basi akafa Tibni, akatawala Omri.

Règne d’Omri sur Israël

23 Katika mwaka wa thelathini na moja wa Asa, mfalme wa Yuda, Omri alianza kutawala juu ya Israeli, akatawala miaka kumi na miwili. Akatawala huko Tirza miaka sita.
1 Rois 15.21 2 Chroniques 22.2 1 Rois 16.29 1 Rois 16.8
24 Kisha akanunua kilima cha Samaria kwa Shemeri kwa talanta mbili za fedha; akajenga juu ya kilima kile, akauita mji alioujenga Samaria, kwa kuliandama jina lake Shemeri, aliyekuwa mwenye kilima.
1 Rois 13.32 2 Rois 17.6 1 Rois 20.1 1 Rois 16.28-16.29 2 Rois 17.1
25 Omri akafanya yaliyo mabaya machoni pa Bwana, akatenda maovu kuliko wote waliomtangulia;
Michée 6.16 1 Rois 16.33 1 Rois 16.30-16.31 1 Rois 14.9
26 kwa kuwa aliiendea njia yote ya Yeroboamu mwana wa Nebati, na makosa yake, aliyowakosesha Israeli, ili kumghadhibisha Bwana, Mungu wa Israeli, kwa matendo yao ya ubatili.
1 Rois 16.19 1 Rois 16.13 1 Rois 12.26-12.33 Jérémie 10.8 Psaumes 31.6
27 Nayo mambo yote ya Omri yaliyosalia aliyoyatenda, na uthabiti alioufanya, je! Hayakuandikwa katika kitabu-cha-tarehe cha wafalme wa Israeli?
1 Rois 16.14 1 Rois 15.31 1 Rois 16.5 1 Rois 16.20
28 Omri akalala na babaze, akazikwa huko Samaria; na Ahabu mwanawe akatawala mahali pake.

Règne d’Achab et Jézabel sur Israël

29 Ahabu mwana wa Omri alianza kutawala juu ya Israeli katika mwaka wa thelathini na nane wa Asa mfalme wa Yuda; akatawala Ahabu mwana wa Omri juu ya Israeli katika Samaria miaka ishirini na miwili.
30 Ahabu mwana wa Omri akafanya yaliyo mabaya machoni pa Bwana kuliko wote waliomtangulia.
1 Rois 16.25 1 Rois 14.9 1 Rois 21.25 2 Rois 3.2 1 Rois 16.31
31 Ikawa, kama ingalikuwa neno dogo tu kuyaendea makosa ya Yeroboamu mwana wa Nebati, akamwoa Yezebeli binti Ethbaali, mfalme wa Wasidoni, akaenda akamtumikia Baali, akamsujudia.
2 Rois 17.16 2 Rois 10.18 Juges 18.7 Juges 2.11 Deutéronome 7.3-7.4
32 Akamjengea Baali madhabahu katika nyumba ya Baali, aliyoijenga huko Samaria.
2 Rois 10.21 2 Rois 10.26-10.27
33 Ahabu akaifanya Ashera; Ahabu akazidi kumghadhibisha Bwana, Mungu wa Israeli, kuliko wafalme wote wa Israeli waliomtangulia.
2 Rois 13.6 1 Rois 21.25 2 Rois 21.3 Exode 34.13 Jérémie 17.1-17.2
34 Katika siku zake, Hieli Mbetheli akajenga Yeriko; akatia misingi yake kwa kufiwa na Abiramu mzaliwa wake wa kwanza, na kuyaweka malango yake kwa kufiwa na mwana wake mdogo Segubu; sawasawa na neno la Bwana alilolinena kwa Yoshua mwana wa Nuni.
Josué 6.26 Matthieu 24.35 Zacharie 1.5 Josué 23.14-23.15

Cette Bible est dans le domaine public.