Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

1 Rois 15.3
Bible en Swahili de l’est


Règne d’Abijam sur Juda

1 Mwaka wa kumi na nane wa mfalme Yeroboamu mwana wa Nebati, Abiya alianza kutawala juu ya Yuda.
1 Rois 14.31 2 Chroniques 13.1-13.22
2 Miaka mitatu akatawala huko Yerusalemu; na jina la mamaye aliitwa Maaka, binti Absalomu.
2 Chroniques 13.2 2 Chroniques 11.20-11.22 1 Rois 15.13
3 Akaziendea dhambi zote za babaye, alizozifanya kabla yake; wala moyo wake haukuwa mkamilifu na Bwana, Mungu wake, kama moyo wa Daudi babaye.
1 Rois 11.4 Psaumes 119.80 1 Rois 3.14 2 Rois 20.3 2 Chroniques 31.20-31.21
4 Walakini kwa ajili ya Daudi, Bwana, Mungu wake, akampa taa humo Yerusalemu, amwinue mwanawe baada yake, na kuufanya imara Yerusalemu;
1 Rois 11.36 2 Chroniques 21.7 Esaïe 62.7 2 Samuel 21.17 Genèse 19.29
5 kwa sababu Daudi alifanya yaliyo mema machoni pa Bwana, wala hakukosa katika yote aliyomwamuru, siku zote za maisha yake, isipokuwa katika habari ya Uria, Mhiti.
1 Rois 14.8 2 Samuel 11.15-11.17 Luc 1.6 2 Samuel 12.9-12.10 1 Rois 9.4
6 Basi kulikuwa na vita kati ya Rehoboamu na Yeroboamu siku zote za maisha yake.
1 Rois 14.30
7 Na mambo yote ya Abiya yaliyosalia, na yote aliyoyafanya, je! Hayakuandikwa katika kitabu-cha-tarehe cha wafalme wa Yuda? Kulikuwa na vita kati ya Abiya na Yeroboamu.
2 Chroniques 13.2-13.22 1 Rois 14.29
8 Abiya akalala na baba zake, wakamzika mjini mwa Daudi. Akatawala Asa mwanawe mahali pake.
2 Chroniques 14.1 1 Rois 14.31 1 Rois 14.1 1 Chroniques 3.9 Matthieu 1.7-1.8

Règne d’Asa sur Juda

9 Mwaka wa ishirini wa Yeroboamu mfalme wa Israeli, Asa alianza kutawala juu ya Yuda.
10 Akatawala miaka arobaini na mmoja huko Yerusalemu; na jina la mamaye aliitwa Maaka, binti Absalomu.
1 Rois 15.2 2 Chroniques 13.2 1 Rois 15.13 2 Chroniques 11.20-11.21
11 Basi, Asa akafanya yaliyo mema machoni pa Mungu, kama alivyofanya babaye Daudi.
2 Chroniques 14.2 2 Chroniques 14.11 2 Chroniques 15.17 1 Rois 15.3 2 Chroniques 16.7-16.10
12 Akawafukuza mahanithi katika nchi, akaziondoa sanamu zote walizozifanya baba zake.
1 Rois 22.46 2 Chroniques 14.2-14.5 1 Rois 11.7-11.8 1 Rois 14.23-14.24 Zacharie 1.2-1.6
13 Hata na Maaka, mamaye, akamwondolea daraja yake asiwe malkia, kwa kuwa amefanya sanamu ya kuchukiza kwa Ashera; basi Asa akaikata sanamu yake akaiteketeza penye kijito cha Kidroni.
Exode 32.20 Jean 18.1 Deutéronome 9.21 Deutéronome 13.6-13.11 Deutéronome 33.9
14 Lakini mahali pa juu hapakuondoshwa; ila moyo wake Asa ulikuwa mkamilifu kwa Bwana siku zake zote.
1 Rois 15.3 1 Rois 22.43 1 Rois 8.61 2 Rois 12.3 2 Rois 14.4
15 Akavileta vile vitu alivyovitakasa baba yake, na vile alivyovitakasa yeye mwenyewe, katika nyumba ya Bwana, fedha; na dhahabu, na vyombo.
1 Rois 7.51 2 Chroniques 14.13 2 Chroniques 15.18 1 Chroniques 26.26-26.28
16 Kulikuwa na vita kati ya Asa na Baasha mfalme wa Israeli siku zao zote.
1 Rois 15.32 1 Rois 15.6-15.7 2 Chroniques 16.1-16.6 1 Rois 14.30
17 Kisha, Baasha mfalme wa Israeli akaondoka juu ya Yuda, akaujenga Rama, ili asimwache mtu ye yote kutoka wala kuingia kwa Asa mfalme wa Yuda.
1 Rois 12.27 2 Chroniques 16.1-16.6 Josué 18.25 1 Rois 15.21-15.22 Jérémie 31.15
18 Ndipo Asa akazitwaa fedha zote na dhahabu zilizosalia katika hazina za nyumba ya Bwana, na hazina za nyumba ya mfalme, akazitia mikononi mwa watumishi wake; mfalme Asa akawatuma kwa Ben-hadadi, mwana wa Tabrimoni, mwana wa Hezioni, mfalme wa Shamu, aliyekaa Dameski, akasema,
1 Rois 14.26 2 Rois 12.18 1 Rois 15.15 1 Rois 11.23-11.24 Genèse 14.15
19 Tumepatana mimi nawe, na baba yangu na baba yako; angalia, nimekuletea zawadi, fedha na dhahabu; basi nenda, uyavunje mapatano yako na Baasha mfalme wa Israeli, ili aniondokee mimi.
2 Chroniques 19.2 2 Samuel 21.2 Romains 1.31 Romains 3.8 2 Chroniques 16.7
20 Naye Ben-hadadi akamsikiliza mfalme Asa, akawatuma wakuu wa majeshi yake juu ya miji ya Israeli, akapiga Iyoni, na Dani, na Abel-beth-maaka na Kinerothi yote, na nchi yote ya Naftali.
2 Rois 15.29 Juges 18.29 Josué 11.2 2 Samuel 20.14-20.15 1 Rois 12.29
21 Ikawa Baasha aliposikia habari hiyo akaacha kuujenga Rama, akaenda akakaa Tirza.
1 Rois 14.17 1 Rois 16.15-16.18 2 Chroniques 16.5 1 Rois 15.17 Cantique 6.4
22 Ndipo mfalme Asa akatangaza kwa Yuda pia; asiachiliwe mtu; nao wakayachukua mawe ya Rama na miti yake, aliyoijengea Baasha; naye mfalme Asa akajenga kwa vitu hivyo Geba wa Benyamini na Mispa.
Josué 21.17 Josué 18.24 Josué 18.26 1 Samuel 7.5 Jérémie 40.10
23 Na mambo yote ya Asa yaliyosalia, na nguvu zake zote, na yote aliyoyafanya, na miji aliyoijenga, je! Hayakuandikwa katika kitabu-cha-tarehe cha wafalme wa Yuda? Lakini alipokuwa mzee alikuwa na ugonjwa wa miguu.
Psaumes 90.10 2 Chroniques 16.11-16.14 1 Rois 15.7-15.8 1 Rois 14.29-14.31
24 Asa akalala na babaze, akazikwa pamoja na babaze mjini mwa Daudi baba yake. Na Yehoshafati mwanawe akatawala mahali pake.
Matthieu 1.8 1 Rois 22.41-22.43 2 Chroniques 17.1-17.9

Règne de Nadab sur Israël

25 Nadabu mwana wa Yeroboamu alianza kutawala juu ya Israeli, mwaka wa pili wa Asa mfalme wa Yuda, akatawala juu ya Israeli miaka miwili.
1 Rois 14.20 1 Rois 14.12
26 Akafanya yaliyo mabaya machoni pa Bwana, akaiendea njia ya baba yake, na kosa lake alilowakosesha Israeli.
1 Rois 14.16 1 Rois 15.30 1 Rois 15.34 1 Rois 12.28-12.33 1 Rois 13.33-13.34
27 Basi Baasha wa Ahiya, wa mbari ya Isakari, akamfanyia fitina; Baasha akampiga huko Gibethoni ulio wa Wafilisti; kwani Nadabu na Israeli wote walikuwa wakiuhusuru Gibethoni.
Josué 19.44 Josué 21.23 1 Rois 14.14 1 Rois 16.15 2 Rois 12.20
28 Mwaka wa tatu wa Asa mfalme wa Yuda Baasha akamwua, akatawala mahali pake.
Deutéronome 32.35
29 Ikawa mara alipotawala, akawapiga nyumba yote ya Yeroboamu. Hakumwachia Yeroboamu mwenye pumzi ye yote, hata alipomharibu sawasawa na neno la Bwana alilolinena kwa mtumishi wake Ahiya, Mshiloni;
1 Rois 14.9-14.16 2 Rois 10.10-10.11 2 Rois 9.7-9.10 2 Rois 9.36-9.37 2 Rois 19.25
30 kwa sababu ya makosa yake Yeroboamu aliyoyakosa, ambayo kwa hayo aliwakosesha Israeli; kwa sababu ya chukizo lake alilomchukiza Bwana, Mungu wa Israeli, hata kumghadhibisha.
1 Rois 15.26 1 Rois 14.9-14.16 1 Rois 14.22
31 Basi mambo yote ya Nadabu yaliyosalia, na yote aliyoyafanya, je! Hayakuandikwa katika kitabu-cha-tarehe cha wafalme wa Israeli?
1 Rois 14.19 1 Rois 16.5 1 Rois 16.20 1 Rois 16.14 1 Rois 16.27

Règne de Baesha sur Israël

32 Kulikuwa na vita kati ya Asa na Baasha mfalme wa Israeli siku zao zote.
1 Rois 15.16
33 Katika mwaka wa tatu wa Asa mfalme wa Yuda, Baasha mwana wa Ahiya alianza kutawala juu ya Israeli wote huko Tirza, akatawala miaka ishirini na minne.
1 Rois 16.8
34 Akafanya yaliyo mabaya machoni pa Bwana akaiendea njia ya Yeroboamu, na kosa lake ambalo kwa hilo aliwakosesha Israeli.
1 Rois 15.26 1 Rois 14.16 1 Rois 12.28-12.29 1 Rois 13.33-13.34 Esaïe 1.4

Cette Bible est dans le domaine public.