Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Genèse 45.13
Bible en Swahili de l’est


Joseph reconnu par ses frères

1 Hapo Yusufu hakuweza kujizuia mbele yao wote waliosimama karibu naye. Akapiga kelele, na kusema, Mwondoeni kila mtu mbele yangu. Wala hakusimama mtu pamoja naye, Yusufu alipojitambulisha kwa nduguze.
Esaïe 42.14 Jérémie 20.9 Actes 10.41 1 Corinthiens 13.5 Matthieu 18.15
2 Akapaza sauti yake akalia, nao Wamisri wakasikia. Watu wa nyumba ya Farao nao wakasikia.
Nombres 14.1 2 Rois 20.3 Actes 20.37 Ruth 1.9 Genèse 46.29
3 Yusufu akawaambia ndugu zake, Mimi ndimi Yusufu; baba yangu angali hai bado? Wala ndugu zake hawakuweza kumjibu, maana waliingiwa na hofu mbele yake.
Actes 7.13 Actes 9.5 Matthieu 14.26-14.27 Job 4.5 Luc 24.37-24.38
4 Yusufu akawaambia ndugu zake, Karibuni kwangu; basi, wakakaribia. Akasema, Mimi ni Yusufu, ndugu yenu, ambaye mliniuza kwenda Misri.
Genèse 37.28 Genèse 50.18 Actes 9.5 Matthieu 14.27
5 Basi sasa, msihuzunike, wala msiudhike nafsi zenu, kwa kuniuza huku; maana Mungu alinipeleka mbele yenu kuhifadhi maisha ya watu.
Genèse 50.20 Job 1.21 Genèse 45.7-45.8 Psaumes 105.16-105.17 Luc 23.34
6 Maana miaka hii miwili njaa imekuwa katika nchi, na iko tena miaka mitano isiyo na kulima wala kuvuna.
Esaïe 30.24 Exode 34.21 Deutéronome 21.4 1 Samuel 8.12 Genèse 47.23
7 Mungu alinipeleka mbele yenu kuwahifadhia masazo katika nchi, na kuwaokoa ninyi kwa wokovu mkuu.
Psaumes 18.50 Actes 7.35 1 Chroniques 11.14 Psaumes 44.4 Juges 15.18
8 Basi si ninyi mlionipeleka huku, ila Mungu; naye ameniweka kama baba kwa Farao, na bwana katika nyumba yake yote, na mtawala katika nchi yote ya Misri.
Juges 17.10 Genèse 45.5 Genèse 41.39-41.48 Jean 19.11 Psaumes 105.21-105.22
9 Fanyeni haraka, mmwendee baba yangu, mkamwambie, Hivi ndivyo asemavyo mwanao Yusufu, Mungu ameniweka kuwa bwana katika Misri yote, basi unishukie, usikawie.
Genèse 45.13 Genèse 45.19-45.20
10 Nawe utakaa katika nchi ya Gosheni, utakuwa karibu nami, wewe, na wanao, na wana wa wanao, na wanyama wako, ng’ombe zako, na yote uliyo nayo. Nami nitakulisha huko;
Exode 8.22 Jean 17.24 Genèse 46.34-47.6 Genèse 46.28-46.29 Jean 14.2-14.3
11 maana bado imesalia miaka mitano ya njaa; usije ukaingia katika uhitaji, wewe, na nyumba yako, na yote uliyo nayo.
Genèse 47.12 Marc 7.9-7.12 Genèse 47.6 1 Timothée 5.4 Matthieu 15.5-15.6
12 Na tazama, macho yenu yanaona, na macho ya ndugu yangu Benyamini, ya kwamba ni kinywa changu mimi kinachosema nanyi.
Genèse 42.23 Luc 24.39 Jean 20.27
13 Nanyi mtamwarifu baba yangu habari za fahari yangu yote katika Misri, na za vyote mlivyoviona; mkafanye haraka kumleta huku baba yangu.
Actes 7.14 1 Pierre 1.10-1.12 Jean 17.24 Apocalypse 21.23
14 Akaanguka shingoni mwa ndugu yake Benyamini, akalia; Benyamini naye akalia shingoni mwake.
Genèse 46.29 Genèse 29.11 Genèse 33.4 Romains 1.31
15 Akawabusu ndugu zake wote, akalia nao, baada ya hayo, nduguze wakazungumza naye
Luc 15.20 Exode 4.27 1 Samuel 20.41 Actes 20.37 Genèse 45.2
16 Habari ikasikika nyumbani mwa Farao kusema, Ndugu zake Yusufu wamekuja. Ikawa vema machoni pa Farao, na machoni pa watumwa wake.
Genèse 34.18 Deutéronome 1.33 Genèse 20.15 Genèse 41.33 Genèse 16.6
17 Farao akamwambia Yusufu, Uwaambie ndugu zako, Fanyeni hivi; wachukuzeni mizigo wanyama wenu, mwondoke mwende nchi ya Kanaani;
Genèse 44.1-44.2 Genèse 42.25-42.26
18 kisha mkamtwae baba yenu, na watu wa nyumbani mwenu, mkanijie; nami nitawapa mema ya nchi ya Misri, nanyi mtakula unono wa nchi.
Genèse 27.28 Genèse 47.6 Nombres 18.29 Nombres 18.12 Psaumes 147.14
19 Nawe umeamriwa; fanyeni hivi, mjitwalie magari katika nchi ya Misri kwa watoto wenu wadogo na wake zenu, mkamchukue baba yenu mje.
Genèse 46.5 Genèse 45.27 Esaïe 49.23 Genèse 31.17-31.18 Esaïe 49.1
20 Wala msivisumbukie vyombo vyenu, maana mema ya nchi yote ya Misri ni yenu.
1 Samuel 30.24 Ezéchiel 12.3-12.4 1 Samuel 10.22 Josué 7.11 1 Samuel 25.13
21 Ndivyo walivyofanya wana wa Israeli. Yusufu akawapa magari kama Farao alivyoamuru, akawapa na chakula cha njiani.
Genèse 45.19 Exode 17.1 Genèse 46.5 Ecclésiaste 8.2 Ezéchiel 23.24
22 Akawapa kila mtu nguo za kubadili; lakini Benyamini, alimpa fedha mia tatu na mavazi matano ya kubadili.
Genèse 43.34 2 Rois 5.5 2 Rois 5.22-5.23 Juges 14.12 Juges 14.19
23 Na babaye akampelekea kama hivi, punda kumi waliochukua mema ya Misri, na punda wake kumi waliochukua nafaka, na mikate, na chakula kwa babaye njiani.
Genèse 43.11 Exode 16.3 Genèse 24.10
24 Akaagana na ndugu zake, wakaenda zao; naye akawaambia, Msigombane njiani.
1 Thessaloniciens 5.13 Genèse 42.21-42.22 Colossiens 3.12-3.13 Psaumes 133.1-133.3 Jean 13.34-13.35
25 Wakatoka Misri, wakafika nchi ya Kanaani kwa Yakobo, baba yao.
26 Wakampasha habari, wakisema, Yusufu angali hai; naye ndiye mtawala katika nchi yote ya Misri. Moyo wake ukazimia, kwa sababu hakuwasadiki.
Genèse 44.28 Genèse 37.35 Job 9.16 Luc 24.41 Psaumes 126.1
27 Wakamwambia maneno yote ya Yusufu, aliyowaambia; na alipoona magari aliyoyapeleka Yusufu, ili kumchukua, roho ya Yakobo baba yao ikafufuka.
Genèse 45.19 Osée 6.2 Juges 15.19 1 Samuel 30.12 Esaïe 57.15
28 Israeli akasema, Yatosha! Yusufu mwanangu angali hai; nitakwenda, nionane naye kabla sijafa.
Genèse 46.30 Luc 2.28-2.30 Jean 16.21-16.22

Cette Bible est dans le domaine public.