Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

1 Samuel 12.5
Bible en Swahili de l’est


Avertissements de Samuel

1 Kisha Samweli akawaambia Israeli wote, Angalieni, nimeisikiliza sauti yenu katika hayo yote mliyoniambia, nami nimemtawaza mfalme juu yenu.
1 Samuel 10.24 1 Samuel 11.14-11.15 1 Samuel 8.5-8.8 1 Samuel 8.19-8.22 1 Samuel 10.1
2 Basi sasa, angalieni, mfalme anakwenda mbele yenu; na mimi ni mzee, mwenye mvi; tena, tazameni, wana wangu wapo pamoja nanyi; nami nimekwenda mbele yenu toka ujana wangu hata leo.
1 Samuel 8.5 1 Samuel 8.1 1 Samuel 8.20 1 Samuel 8.3 Nombres 27.17
3 Nami nipo hapa; basi, mnishuhudie mbele za Bwana, na mbele ya masihi wake,nalitwaa ng`ombe wa nani? au nalitwaa punda wa nani? au ni nani niliye mdhulumu? Ni nani niliyemwonea? Au kwa mkono wa nani nimepokea rushwa inipofushe macho? Nami nitawarudishia ninyi.
1 Samuel 10.1 1 Samuel 24.6 Nombres 16.15 Actes 20.33 Deutéronome 16.19
4 Nao wakasema, hukutudhulumu, wala hukutuonea, wala hukupokea kitu kwa mkono wa mtu awaye yote.
Psaumes 37.5-37.6 3 Jean 1.12 Daniel 6.4
5 Akawaambia, Bwana ni shahidi juu yenu, na masihi
Exode 22.4 Actes 23.9 Actes 24.20 Psaumes 17.3 Actes 24.16
6 Samweli akawaambia watu, Ni yeye Bwana aliyewaweka Musa na Haruni, ndiye yeye aliyewatoa baba zenu kutoka nchi ya Misri.
Michée 6.4 Exode 6.26 Esaïe 63.7-63.14 Psaumes 77.19-77.20 Psaumes 78.12-78.72
7 Basi sasa simameni, ili niwahutubie mbele za Bwana, kwa kutaja matendo yote ya haki ya Bwana, aliyowatendea ninyi na baba zenu.
Esaïe 1.18 Ezéchiel 18.25-18.30 Esaïe 5.3-5.4 Actes 17.3 Juges 5.11
8 Yakobo alipokuwa ameingia Misri, na baba zenu walipomlilia Bwana, ndipo Bwana akawapeleka Musa na Haruni, nao wakawatoa baba zenu kutoka Misri, wakawakalisha mahali hapa.
Exode 4.14-4.16 Exode 2.23-2.24 Exode 3.9-3.10 Exode 6.26 Josué 1.6
9 Lakini wakamsahau Bwana, Mungu wao, naye akawauza na kuwatia katika mikono ya Sisera, jemadari wa jeshi la Hazori, na katika mikono ya Wafilisti, na katika mikono ya mfalme wa Moabu, nao wakapigana nao.
Juges 13.1 Juges 10.7 Juges 4.2 Juges 3.12 Deutéronome 32.18
10 Nao wakamlilia Bwana, wakasema, Tumefanya dhambi, kwa kuwa tumemwacha Bwana, na kuwatumikia Mabaali na Maashtorethi; lakini sasa utuokoe na mikono ya adui zetu, nasi tutakutumikia wewe.
Juges 2.13 Juges 10.10 Juges 10.15-10.16 Juges 3.7 Juges 3.9
11 Bwana akawatuma Yerubaali, na Baraka, na Yeftha, na Samweli, akawaokoa ninyi na mikono ya adui zenu pande zote, nanyi mkakaa salama.
Juges 6.32 Juges 4.6 Juges 8.35 Juges 11.1-11.33 Juges 8.29
12 Hata mlipomwona Nahashi, mfalme wa wana wa Amoni, amekuja kupigana nanyi, mliniambia, Sivyo, lakini mfalme atatutawala; ingawa Bwana, Mungu wenu, ni mfalme wenu.
Juges 8.23 1 Samuel 8.5-8.7 1 Samuel 11.1-11.2 1 Samuel 10.19 Genèse 17.7
13 Basi sasa, mtazameni mfalme mliyemchagua na kumtaka; tazameni, Bwana ameweka mfalme juu yenu.
1 Samuel 10.24 Osée 13.11 1 Samuel 8.5 1 Samuel 11.15 1 Samuel 9.20
14 Kama mkimcha Bwana, na kumtumikia, na kuisikia sauti yake, msiiasi amri ya Bwana, tena kama ninyi, na mfalme anayewatawala, mkimfuata Bwana, Mungu wenu, vema!
Josué 24.14 Lévitique 20.1-20.13 Romains 2.7 Esaïe 3.10 Josué 24.20
15 Bali msipoisikia sauti ya Bwana, mkiiasi amri ya Bwana, ndipo mkono wa Bwana utakuwa juu yenu, kama ulivyokuwa juu ya baba zenu.
Josué 24.20 Esaïe 1.20 1 Samuel 12.9 Deutéronome 28.15-28.68 Esaïe 3.11
16 Na sasa simameni, mkalione jambo hili kubwa, Bwana atakalolitenda mbele ya macho yenu.
Exode 14.13 Exode 14.31 1 Samuel 15.16 1 Samuel 12.7
17 Leo je! Si mavuno ya ngano? Nitamwomba Bwana, kwamba apeleke ngurumo na mvua; nanyi mtajua na kuona ya kuwa uovu wenu ni mwingi sana, mlioufanya machoni pa Bwana, kwa kujitakia mfalme.
Proverbes 26.1 1 Samuel 8.7 1 Samuel 7.9-7.10 Jacques 5.16-5.18 Jérémie 15.1
18 Basi Samweli akamwomba Bwana, naye Bwana akapeleka ngurumo na mvua siku ile; nao watu wote wakamwogopa Bwana sana, na Samweli pia.
Exode 14.31 Esdras 10.9 Apocalypse 11.5-11.6 Exode 9.23-9.25 Psaumes 106.12-106.13
19 Watu wote wakamwambia Samweli, Utuombee sisi watumwa wako kwa Bwana, Mungu wako, tusije tukafa; maana tumeongeza dhambi zetu zote kwa uovu huu, wa kujitakia mfalme.
Exode 9.28 1 Jean 5.16 Exode 10.17 1 Samuel 12.23 Genèse 20.7
20 Samweli akawaambia, Msiogope; ni kweli mmeutenda uovu huu wote; lakini msigeuke na kuacha kumfuata Bwana, bali mtumikieni Bwana kwa mioyo yenu yote.
Deutéronome 11.16 Jérémie 3.1 1 Pierre 3.16 Deutéronome 31.29 Josué 23.6
21 Wala msigeuke upande, maana, kufuata vitu vya ubatili,
Habakuk 2.18 Jérémie 16.19 Jérémie 10.15 1 Corinthiens 8.4 Esaïe 45.20
22 visivyoweza kusaidia wala kuokoa, kwa kuwa havifai kitu. Maana Bwana hatawaacha watu wake kwa ajili ya jina lake kuu; kwa kuwa imempendeza Bwana kuwafanya ninyi kuwa watu wake mwenyewe.
Psaumes 106.8 1 Rois 6.13 Josué 7.9 Deutéronome 7.7-7.8 Jérémie 14.21
23 Walakini mimi, hasha! Nisimtende Bwana dhambi kwa kuacha kuwaombea ninyi; lakini nitawaelimisha katika njia iliyo njema, na kunyoka
Romains 1.9 Colossiens 1.9 2 Timothée 1.3 1 Rois 8.36 Proverbes 4.11
24 Mcheni Bwana tu, mkamtumikie kwa kweli kwa mioyo yenu yote; maana, kumbukeni jinsi alivyowatendea mambo makuu.
Deutéronome 10.21 Esaïe 5.12 Psaumes 126.2-126.3 Job 28.28 Ecclésiaste 12.13
25 Lakini kama mkiendelea kutenda mabaya, mtaangamia, ninyi na mfalme wenu pia.
Josué 24.20 1 Samuel 31.1-31.5 Deutéronome 28.36 Osée 10.3 Esaïe 3.11

Cette Bible est dans le domaine public.