Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Ruth 2.3
Bible en Swahili de l’est


Rencontre de Ruth et Boaz

1 Basi huyo Naomi alikuwa na ndugu ya mumewe, mtu mkuu mwenye mali, wa jamaa yake Elimeleki, na jina lake aliitwa Boazi.
Ruth 4.21 Ruth 3.2 Ruth 3.12 Matthieu 1.5 1 Chroniques 2.10-2.12
2 Naye Ruthuu Mmoabi akamwambia Naomi, Sasa niende kondeni, niokote masazo ya masuke nyuma yake yule ambaye nitaona kibali machoni pake. Akamwambia, Haya, mwanangu, nenda.
Lévitique 23.22 Lévitique 19.9 Deutéronome 24.19-24.21 Ruth 2.7 Lévitique 19.16
3 Basi akaenda, akaja akaokota masazo kondeni nyuma ya wavunaji; na bahati yake ikamtukia kwamba akaifika sehemu ya shamba iliyokuwa mali yake huyo Boazi, ambaye alikuwa wa jamaa yake Elimeleki.
2 Thessaloniciens 3.12 1 Thessaloniciens 4.11-4.12 Luc 10.31 Esther 6.1-6.2 2 Rois 8.5
4 Na tazama, Boazi akaja kutoka Bethlehemu kawaamkia wavunaji, akasema, Bwana akae nanyi. Nao wakamwitikia, Bwana na akubariki.
2 Thessaloniciens 3.16 Psaumes 129.7-129.8 Luc 1.28 Juges 6.12 2 Timothée 4.22
5 Kisha Boazi akamwuliza mtumishi aliyewasimamia wavunaji, Na huyu je! Ni msichana wa nani?
Ruth 4.21 1 Chroniques 2.11-2.12
6 Yule msimamizi aliyewasimamia wavunaji akajibu, akasema, Ni yule msichana Mmoabi aliyerudi pamoja na Naomi, kutoka nchi ya Moabu;
Ruth 1.22 Matthieu 20.8 Ruth 1.19 Matthieu 24.45 Genèse 15.2
7 naye akasema, Tafadhali niruhusu kuokota masazo, na kukusanya nyuma ya wavunaji kati ya miganda; basi akaja, naye ameshinda tangu asubuhi hata sasa, isipokuwa alikaa nyumbani kitambo kidogo.
Proverbes 18.23 Proverbes 15.33 Proverbes 13.4 Ephésiens 5.21 Proverbes 22.29
8 Basi Boazi akamwambia Ruthuu, Mwanangu, sikiliza; wewe usiende kuokota masazo katika shamba lingine, wala usiondoke hapa, lakini ukae papa hapa karibu na wasichana wangu.
Cantique 1.7-1.8 Philippiens 4.8 Matthieu 9.2 Matthieu 9.22 Matthieu 10.7-10.11
9 Macho yako na yaelekee konde walivunalo, ufuatane nao; je! Sikuwaagiza vijana wasikuguse? Tena, ukiona kiu, uende kwenye vyombo, nawe uyanywe waliyoyateka hao vijana.
1 Jean 5.18 Matthieu 10.42 Job 19.21 Proverbes 6.29 Genèse 20.6
10 Ndipo aliposujudia, akainama mpaka nchi, akamwambia, Jinsi gani nimepata kibali machoni pako, hata ukanifahamu, mimi niliye mgeni?
1 Samuel 25.23 Romains 12.10 2 Samuel 9.8 2 Samuel 19.28 Luc 1.48
11 Naye Boazi akajibu, akamwambia, Nimeelezwa sana yote uliyomfanyia mkweo, tangu alipokufa mumeo; na jinsi ulivyowaacha baba yako na mama yako, na nchi yako uliyozaliwa, ukawafikilia watu usiowajua tangu hapo.
Ruth 1.14-1.22 Hébreux 11.24-11.26 Luc 14.33 Ruth 1.11 Psaumes 37.5-37.6
12 Bwana akujazi kwa kazi yako, nawe upewe thawabu kamili na Bwana, Mungu wa Israeli, ambaye umekuja kukimbilia chini ya mabawa yake.
Psaumes 91.4 Psaumes 36.7 Psaumes 17.8 Psaumes 57.1 Psaumes 61.4
13 Ndipo aliposema, Bwana wangu, na nipate kibali machoni pako; kwa sababu wewe umeniburudisha moyo, na kumwambia mema mjakazi wako, ingawa mimi si kama mmojawapo wa wajakazi wako.
1 Samuel 1.18 Genèse 33.15 Genèse 33.10 Proverbes 15.33 1 Samuel 25.41
14 Tena wakati wa chakula huyo Boazi akamwambia, Karibu kwetu, ule katika mkate wetu, na ulichovye tonge lako katika siki yetu. Basi akaketi pamoja na wavunaji, nao wakampitishia bisi, naye akala akashiba, hata akasaza.
Ruth 2.18 Deutéronome 8.10 Luc 14.12-14.14 Matthieu 14.20 2 Rois 4.43-4.44
15 Naye alipoinuka tena ili aende kuokota masazo, huyo Boazi aliwaagiza vijana wake akisema, Mwacheni aokote hata kati ya miganda, wala msimkemee.
Jacques 1.5
16 Tena mtoleeni kidogo katika matita na kukiacha, na akiokote, wala msimkataze.
Romains 12.13 1 Jean 3.17-3.18 Hébreux 6.10 2 Corinthiens 8.5-8.11 Deutéronome 24.19-24.21
17 Basi Ruthuu akaokota masazo kondeni hata jioni; kisha akazipura zile nafaka alizoziokota, zikawa yapata efa moja ya shayiri.
Exode 16.36 Proverbes 31.27 Ezéchiel 45.11-45.12
18 Akajitwika, akaenda zake mjini. Akamwonyesha mkwewe zile alizoziokota; akavitoa vile vyakula alivyovisaza alipokwisha kushiba, akampa.
Ruth 2.14 1 Timothée 5.4 Jean 6.12-6.13
19 Basi mkwewe akamwuliza, Je! Umeokota wapi leo? Umefanya kazi wapi? Na abarikiwe yeye aliyekufahamu. Naye akamwarifu mkwewe ni nani ambaye alifanya kazi kwake, akasema, Yule mtu niliyefanya kazi kwake leo jina lake aitwa Boazi.
Psaumes 41.1 Ruth 2.10 1 Rois 7.21 2 Corinthiens 9.13-9.15
20 Naye Naomi akamwambia mkwewe, Na abarikiwe huyo na Bwana, ambaye hakuuacha wema wake, wala kwa hao walio hai wala kwao waliokufa. Kisha Naomi akamwambia, Mtu huyu ni wa mbari yetu, mmojawapo wa jamaa yetu aliye karibu.
Ruth 3.9-3.10 2 Samuel 2.5 Proverbes 17.17 Lévitique 25.25 Deutéronome 25.5-25.7
21 Naye Ruthuu Mmoabi akasema, Naam, akaniambia, Ukae papa hapa karibu na vijana wangu, hata watakapomaliza mavuno yangu yote.
Ruth 2.7-2.8 Ruth 2.22 Cantique 1.7-1.8
22 Kisha Naomi akamwambia Ruthuu mkwewe, Mwanangu, ni vizuri wewe ufuatane na wasichana wake, wala watu wasikukute katika konde linginelo lote.
Cantique 1.8 Proverbes 27.10
23 Hivyo yeye akafuatana na wasichana wake Boazi na kuokota, hata mwisho wa mavuno ya shayiri na mavuno ya ngano pia; naye alikuwa akikaa kwa mkwewe.
Proverbes 13.1 1 Corinthiens 15.33 Deutéronome 16.9 Ephésiens 6.1-6.3 Proverbes 6.6-6.8

Cette Bible est dans le domaine public.