Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Ruth 2.13
Bible en Swahili de l’est


Rencontre de Ruth et Boaz

1 Basi huyo Naomi alikuwa na ndugu ya mumewe, mtu mkuu mwenye mali, wa jamaa yake Elimeleki, na jina lake aliitwa Boazi.
Ruth 4.21 Matthieu 1.5 Ruth 3.2 Ruth 3.12 1 Chroniques 2.10-2.12
2 Naye Ruthuu Mmoabi akamwambia Naomi, Sasa niende kondeni, niokote masazo ya masuke nyuma yake yule ambaye nitaona kibali machoni pake. Akamwambia, Haya, mwanangu, nenda.
Lévitique 23.22 Lévitique 19.9 Deutéronome 24.19-24.21 Lévitique 19.16 Ruth 2.7
3 Basi akaenda, akaja akaokota masazo kondeni nyuma ya wavunaji; na bahati yake ikamtukia kwamba akaifika sehemu ya shamba iliyokuwa mali yake huyo Boazi, ambaye alikuwa wa jamaa yake Elimeleki.
2 Thessaloniciens 3.12 Esther 6.1-6.2 2 Rois 8.5 Matthieu 10.29 1 Thessaloniciens 4.11-4.12
4 Na tazama, Boazi akaja kutoka Bethlehemu kawaamkia wavunaji, akasema, Bwana akae nanyi. Nao wakamwitikia, Bwana na akubariki.
2 Thessaloniciens 3.16 Psaumes 129.7-129.8 Luc 1.28 Juges 6.12 2 Timothée 4.22
5 Kisha Boazi akamwuliza mtumishi aliyewasimamia wavunaji, Na huyu je! Ni msichana wa nani?
Ruth 4.21 1 Chroniques 2.11-2.12
6 Yule msimamizi aliyewasimamia wavunaji akajibu, akasema, Ni yule msichana Mmoabi aliyerudi pamoja na Naomi, kutoka nchi ya Moabu;
Ruth 1.22 Genèse 15.2 Ruth 1.16 Genèse 39.4 Genèse 24.2
7 naye akasema, Tafadhali niruhusu kuokota masazo, na kukusanya nyuma ya wavunaji kati ya miganda; basi akaja, naye ameshinda tangu asubuhi hata sasa, isipokuwa alikaa nyumbani kitambo kidogo.
Proverbes 13.4 Proverbes 18.23 Proverbes 15.33 Proverbes 22.29 1 Pierre 5.5-5.6
8 Basi Boazi akamwambia Ruthuu, Mwanangu, sikiliza; wewe usiende kuokota masazo katika shamba lingine, wala usiondoke hapa, lakini ukae papa hapa karibu na wasichana wangu.
Matthieu 10.7-10.11 1 Samuel 3.16 1 Samuel 3.6 2 Rois 5.13 Cantique 1.7-1.8
9 Macho yako na yaelekee konde walivunalo, ufuatane nao; je! Sikuwaagiza vijana wasikuguse? Tena, ukiona kiu, uende kwenye vyombo, nawe uyanywe waliyoyateka hao vijana.
1 Jean 5.18 Matthieu 10.42 Psaumes 105.15 Jean 4.7-4.11 Job 19.21
10 Ndipo aliposujudia, akainama mpaka nchi, akamwambia, Jinsi gani nimepata kibali machoni pako, hata ukanifahamu, mimi niliye mgeni?
1 Samuel 25.23 2 Samuel 9.8 Romains 12.10 Ruth 2.2 Matthieu 25.35
11 Naye Boazi akajibu, akamwambia, Nimeelezwa sana yote uliyomfanyia mkweo, tangu alipokufa mumeo; na jinsi ulivyowaacha baba yako na mama yako, na nchi yako uliyozaliwa, ukawafikilia watu usiowajua tangu hapo.
Hébreux 11.24-11.26 Ruth 1.14-1.22 Hébreux 11.8-11.9 Luc 5.23 Luc 18.29-18.30
12 Bwana akujazi kwa kazi yako, nawe upewe thawabu kamili na Bwana, Mungu wa Israeli, ambaye umekuja kukimbilia chini ya mabawa yake.
Psaumes 91.4 Psaumes 36.7 Psaumes 63.7 1 Samuel 24.19 Psaumes 17.8
13 Ndipo aliposema, Bwana wangu, na nipate kibali machoni pako; kwa sababu wewe umeniburudisha moyo, na kumwambia mema mjakazi wako, ingawa mimi si kama mmojawapo wa wajakazi wako.
1 Samuel 1.18 Genèse 33.15 Genèse 33.8 Philippiens 2.3 2 Samuel 16.4
14 Tena wakati wa chakula huyo Boazi akamwambia, Karibu kwetu, ule katika mkate wetu, na ulichovye tonge lako katika siki yetu. Basi akaketi pamoja na wavunaji, nao wakampitishia bisi, naye akala akashiba, hata akasaza.
Ruth 2.18 Matthieu 14.20 2 Rois 4.43-4.44 Deutéronome 8.10 Luc 14.12-14.14
15 Naye alipoinuka tena ili aende kuokota masazo, huyo Boazi aliwaagiza vijana wake akisema, Mwacheni aokote hata kati ya miganda, wala msimkemee.
Jacques 1.5
16 Tena mtoleeni kidogo katika matita na kukiacha, na akiokote, wala msimkataze.
1 Jean 3.17-3.18 Romains 12.13 Philémon 1.7 Matthieu 25.40 Psaumes 112.9
17 Basi Ruthuu akaokota masazo kondeni hata jioni; kisha akazipura zile nafaka alizoziokota, zikawa yapata efa moja ya shayiri.
Ezéchiel 45.11-45.12 Exode 16.36 Proverbes 31.27
18 Akajitwika, akaenda zake mjini. Akamwonyesha mkwewe zile alizoziokota; akavitoa vile vyakula alivyovisaza alipokwisha kushiba, akampa.
Ruth 2.14 1 Timothée 5.4 Jean 6.12-6.13
19 Basi mkwewe akamwuliza, Je! Umeokota wapi leo? Umefanya kazi wapi? Na abarikiwe yeye aliyekufahamu. Naye akamwarifu mkwewe ni nani ambaye alifanya kazi kwake, akasema, Yule mtu niliyefanya kazi kwake leo jina lake aitwa Boazi.
Ruth 2.10 Psaumes 41.1 2 Corinthiens 9.13-9.15 1 Rois 7.21
20 Naye Naomi akamwambia mkwewe, Na abarikiwe huyo na Bwana, ambaye hakuuacha wema wake, wala kwa hao walio hai wala kwao waliokufa. Kisha Naomi akamwambia, Mtu huyu ni wa mbari yetu, mmojawapo wa jamaa yetu aliye karibu.
2 Samuel 2.5 Ruth 3.9-3.10 Proverbes 17.17 Lévitique 25.25 Deutéronome 25.5-25.7
21 Naye Ruthuu Mmoabi akasema, Naam, akaniambia, Ukae papa hapa karibu na vijana wangu, hata watakapomaliza mavuno yangu yote.
Cantique 1.7-1.8 Ruth 2.7-2.8 Ruth 2.22
22 Kisha Naomi akamwambia Ruthuu mkwewe, Mwanangu, ni vizuri wewe ufuatane na wasichana wake, wala watu wasikukute katika konde linginelo lote.
Cantique 1.8 Proverbes 27.10
23 Hivyo yeye akafuatana na wasichana wake Boazi na kuokota, hata mwisho wa mavuno ya shayiri na mavuno ya ngano pia; naye alikuwa akikaa kwa mkwewe.
Deutéronome 16.9 Ephésiens 6.1-6.3 Proverbes 6.6-6.8 Proverbes 13.20 Proverbes 13.1

Cette Bible est dans le domaine public.